Ndugu zanguni,
Taarifa nilizopata leo ni kuwa 'mdahalo' utakaoneshwa na ITV leo usiku kuhusu mgombea Urais wa CCM Jakaya Kikwete, umeingiliwa na mafisadi kuhakikisha kuwa unakuwa ni mkutano wa kampeni badala ya mdahalo.
Kwanza kabisa, jukumu la kualika waandishi wa habari na washiriki wengine halifanywi na waandaaji wa mdahalo huo (Rose Mwakitwange na Vox Media ya Ansbert Ngurumo) bali limepewa timu ya kampeni ya Kikwete.
Sielewi kwa nini waandaji wa mdahalo huu wameruhusu uhuni huu haswa ikizingatikwa kuwa Ngurumo yupo kwenye campaign team by Dk. WILLIBROD SLAA wa Chadema.
Waandishi watakaoalikwa kwenye mdahalo huo ni wale tu waliokuwepo kwenye kampeni ya Kikwete. Waandishi hawa ndiyo wale walikuwa wanalipwa posho ya shilingi laki 1 kila siku na CCM na kuvishwa nguo zimeandikwa "KIKWETE PRESS."
Taarifa nilizopata ni kuwa tayari campaign team ya Kikwete, akiwemo Abdulrahman Kinana, January Makamba, Prince Bagenda na Muhingo Rweyemamu, wameandaa maswali ya kumbeba JK ambao waandishi hawa wamepewa waulize kwenye mdahalo.
Waandishi hawa wamepewa maswali ya kumpamba Kikwete na kumponda SLAA kwenye mdahalo huo na tayari Kikwete ameandaliwa majibu ambayo atayasoma.
Hivi sasa, mwandishi wa Tanzania Daima, anayeitwa IRENE MARK, ndiye amebeba bahasha kubwa yenye mialiko ya waandishi wa Kikwete watakao hudhuria mdahalo huu. Mwandishi huyu amepewa pesa azunguke newsroom zote na kugawa mialiko hiyo kwa "carefully selected journalists" ambao walikuwa kwenye kampeni za Kikwete.
Cha ajabu mwandishi huyu yuko kwenye gazeti linalomilikiwa na Freeman Mbowe, mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA.
Waandishi hawa wa Kikwete ambao tutawaona kwenye mdahalo leo usiku wamepanga kufanya party kubwa ambayo itafadhiliwa na CCM ili kujipongeza kwa mchango wao kwenye ushindi wanaotarajia wa Kikwete.
Pia, CCM wamefanya hila makusudi ili mdahalo uliotia fora sana wa SLAA usirudiwe tena kwenye TV yeyote hapa nchini mpaka uchaguzi upite.
Timu ya Kinana imewarubuni waandaaji wa mdahalo huu ili Kikwete awe mgombea wa mwisho kuzungumza kwenye TV leo ili ujumbe wake ubaki kwenye akili za Watanzania siku ya kupiga kura Jumapili.
SWALI: Ngurumo wa Vox Media ambao wanaandaa mdahalo huu kwa nini anaruhusu hujuma hii yote dhidi ya SLAA?
Naomba kuwasilisha...
B careful bro/sisy, taarifa za uhakika zinasema mdahalo huu umeandaliwa na ccm wenyewe ndo maana wanachagua watu wa kuattend. akina mwakitwange kazi yao itakuwa kubroadcast tu......
amekuwepo clouds asbh, nahisi wote/wengi mmesikia ,hakuna jipya kabisa.
2010 tz is for change.....be confident and vote Dr Slaa