Elections 2010 HUJUMA dhidi ya SLAA katika mdahalo wa JK leo

Ndugu zanguni,


Taarifa nilizopata leo ni kuwa 'mdahalo' utakaoneshwa na ITV leo usiku kuhusu mgombea Urais wa CCM Jakaya Kikwete, umeingiliwa na mafisadi kuhakikisha kuwa unakuwa ni mkutano wa kampeni badala ya mdahalo.

Kwanza kabisa, jukumu la kualika waandishi wa habari na washiriki wengine halifanywi na waandaaji wa mdahalo huo (Rose Mwakitwange na Vox Media ya Ansbert Ngurumo) bali limepewa timu ya kampeni ya Kikwete.

Sielewi kwa nini waandaji wa mdahalo huu wameruhusu uhuni huu haswa ikizingatikwa kuwa Ngurumo yupo kwenye campaign team by Dk. WILLIBROD SLAA wa Chadema.

Waandishi watakaoalikwa kwenye mdahalo huo ni wale tu waliokuwepo kwenye kampeni ya Kikwete. Waandishi hawa ndiyo wale walikuwa wanalipwa posho ya shilingi laki 1 kila siku na CCM na kuvishwa nguo zimeandikwa "KIKWETE PRESS."

Taarifa nilizopata ni kuwa tayari campaign team ya Kikwete, akiwemo Abdulrahman Kinana, January Makamba, Prince Bagenda na Muhingo Rweyemamu, wameandaa maswali ya kumbeba JK ambao waandishi hawa wamepewa waulize kwenye mdahalo.

Waandishi hawa wamepewa maswali ya kumpamba Kikwete na kumponda SLAA kwenye mdahalo huo na tayari Kikwete ameandaliwa majibu ambayo atayasoma.

Hivi sasa, mwandishi wa Tanzania Daima, anayeitwa IRENE MARK, ndiye amebeba bahasha kubwa yenye mialiko ya waandishi wa Kikwete watakao hudhuria mdahalo huu. Mwandishi huyu amepewa pesa azunguke newsroom zote na kugawa mialiko hiyo kwa "carefully selected journalists" ambao walikuwa kwenye kampeni za Kikwete.

Cha ajabu mwandishi huyu yuko kwenye gazeti linalomilikiwa na Freeman Mbowe, mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA.

Waandishi hawa wa Kikwete ambao tutawaona kwenye mdahalo leo usiku wamepanga kufanya party kubwa ambayo itafadhiliwa na CCM ili kujipongeza kwa mchango wao kwenye ushindi wanaotarajia wa Kikwete.

Pia, CCM wamefanya hila makusudi ili mdahalo uliotia fora sana wa SLAA usirudiwe tena kwenye TV yeyote hapa nchini mpaka uchaguzi upite.

Timu ya Kinana imewarubuni waandaaji wa mdahalo huu ili Kikwete awe mgombea wa mwisho kuzungumza kwenye TV leo ili ujumbe wake ubaki kwenye akili za Watanzania siku ya kupiga kura Jumapili.

SWALI: Ngurumo wa Vox Media ambao wanaandaa mdahalo huu kwa nini anaruhusu hujuma hii yote dhidi ya SLAA?

Naomba kuwasilisha...

B careful bro/sisy, taarifa za uhakika zinasema mdahalo huu umeandaliwa na ccm wenyewe ndo maana wanachagua watu wa kuattend. akina mwakitwange kazi yao itakuwa kubroadcast tu......
amekuwepo clouds asbh, nahisi wote/wengi mmesikia ,hakuna jipya kabisa.
2010 tz is for change.....be confident and vote Dr Slaa
 
Kutokana na ripoti tuliyoipata leo kwenye mdahalo na Clouds, labda aweanasoma majibu kama wasoma taarifa ya habari. Otherwise, kigugumizi na kucheua mara kwa mara vitamuumbua.
 
Kwani ataongea nini zaidi ya kile aliongea na clouds leo . Pumba pumba hadi mwisho.
 
Nadhani wamechelewa saaaana kumhujumu Slaa kwa njia hiyo. Sidhani kama mtu mwenye akili timamu utambadilisha sasa hivi hata utumie njia gani kumwambia kwamba eti madini yetu hayaibiwe, eti Kagoda hakukomba EPA, at Mererani hakuna wizi uliofanyika , eti mafisadi hawalindwi na JK. Wanapoteza muda na kujiburudisha na kumkaririsha majibu yasio na kichwa wala miguu kilaza JK
 
B careful bro/sisy, taarifa za uhakika zinasema mdahalo huu umeandaliwa na ccm wenyewe ndo maana wanachagua watu wa kuattend. akina mwakitwange kazi yao itakuwa kubroadcast tu......
amekuwepo clouds asbh, nahisi wote/wengi mmesikia ,hakuna jipya kabisa.
2010 tz is for change.....be confident and vote Dr Slaa

Coming Sunday change is needed
 
Huyo kikojozi kikwete ata akiiba kura ajue kuwa watanzania wamemchoka
kilichobaki sasa kukabidhisha madaraka
 
Sidhani kama Kikwete ataweza kushawishi kama alivyofanya Slaa, after all watu wengi tayari wameshaamua nani wa kumpigia kura. Sana sana Kikwete atapunguza baadhi ya kura za watu makini ambao walikuwa hawana uhakika na uwezo wake

Kwa interview yake ya leo asubuhi na kituo cha redio cha clouds fm amenisababisha ni mchukie mpaka baba wa taifa wanayesema ndio aliyemlea na kumkuza kimadaraka,jamaa anahojiwa na watu wadhaifu,na maswali ya kupangwa alafu bado anapata kigugumizi,je,angekurupushwa ingekuwaje?Amin amin nawaambia,kamaa mtampa ridhaa nyingine mtu huyu nitafanya kila njia kuachana na uraia wa taifa letu hili la vipofu!!
 
Taarifa nilizonazo ni kwamba mbali ya waandishi waliokuwa katika msafara wa kampeni za Kikwete kualikwa, wengine walioalikwa ni wahariri wakuu na watendaji wa vyombo vyote vya habari nchini. Aidha ni kweli pia kwamba anayeratibu mialiko ya waandishi wa habari waliokuwa katika msafara wa kampeni za Kikwete ni Irene Mark wa Tanzania Daima ambaye wakati wa mizunguko hiyo alichaguliwa na wana habari wenzake kuwa Katibu wa waandishi wa habari aliyekuwa akiratibu masuala yote yaliyokuwa yakihusu posho, malazi, chakula na mambo mengine yaliyokuwa yakiwazonga wanahabari.

Taarifa nilizopata kutoka kwa Irene Mark mwenyewe zinaeleza kuwa pamoja na kupewa bahasha zenye kadi za mialiko ya waandishi wa habari hao hajapewa fedha zozote za kuzungukia katika vyumba vya habari na badala yake ameshawasiliana kwa simu na wenzake hao ambao wamekuwa wakifika Tanzania Daima kuchukua mialiko yao.

Nimewasiliana na wahariri watendaji wa magazeti ya Majira na Mwananchi na wote wameniambia kuwa walikuwa hawajapata mialiko yao ingawa mimi mwenyewe na Saed Kubenea tumeshapata mialiko yetu kupitia kwa Muhingo Rweyemamu aliyekuwa mratibu mkuu wa waandishi wa habari wakati wa kampeni hizo za Kikwete.

Nimeshindwa kuthibitisha taarifa za kuandaliwa kwa maswali na majibu kwa mgombea huyo. Hata hivyo katika hali ya kawaida ninaamini pia kwamba ni lazima Kikwete atakuwa amejiandaa kujibu baadhi ya hoja ambazo wanaamini zitazaa maswali kutoka kwa waandishi wa habari
 
Ndugu zanguni,


Taarifa nilizopata leo ni kuwa 'mdahalo' utakaoneshwa na ITV leo usiku kuhusu mgombea Urais wa CCM Jakaya Kikwete, umeingiliwa na mafisadi kuhakikisha kuwa unakuwa ni mkutano wa kampeni badala ya mdahalo.

Kwanza kabisa, jukumu la kualika waandishi wa habari na washiriki wengine halifanywi na waandaaji wa mdahalo huo (Rose Mwakitwange na Vox Media ya Ansbert Ngurumo) bali limepewa timu ya kampeni ya Kikwete.

Sielewi kwa nini waandaji wa mdahalo huu wameruhusu uhuni huu haswa ikizingatikwa kuwa Ngurumo yupo kwenye campaign team by Dk. WILLIBROD SLAA wa Chadema.

Waandishi watakaoalikwa kwenye mdahalo huo ni wale tu waliokuwepo kwenye kampeni ya Kikwete. Waandishi hawa ndiyo wale walikuwa wanalipwa posho ya shilingi laki 1 kila siku na CCM na kuvishwa nguo zimeandikwa "KIKWETE PRESS."

Alaah

Taarifa nilizopata ni kuwa tayari campaign team ya Kikwete, akiwemo Abdulrahman Kinana, January Makamba, Prince Bagenda na Muhingo Rweyemamu, wameandaa maswali ya kumbeba JK ambao waandishi hawa wamepewa waulize kwenye mdahalo.

We ulitaka wampe ya kumkweza?

Waandishi hawa wamepewa maswali ya kumpamba Kikwete na kumponda SLAA kwenye mdahalo huo na tayari Kikwete ameandaliwa majibu ambayo atayasoma.

Hivi sasa, mwandishi wa Tanzania Daima, anayeitwa IRENE MARK, ndiye amebeba bahasha kubwa yenye mialiko ya waandishi wa Kikwete watakao hudhuria mdahalo huu. Mwandishi huyu amepewa pesa azunguke newsroom zote na kugawa mialiko hiyo kwa "carefully selected journalists" ambao walikuwa kwenye kampeni za Kikwete.

Hizo fitna mwacheni mdada wa watu ajilie vyake alah!

Cha ajabu mwandishi huyu yuko kwenye gazeti linalomilikiwa na Freeman Mbowe, mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA.

Waandishi hawa wa Kikwete ambao tutawaona kwenye mdahalo leo usiku wamepanga kufanya party kubwa ambayo itafadhiliwa na CCM ili kujipongeza kwa mchango wao kwenye ushindi wanaotarajia wa Kikwete.

Pia, CCM wamefanya hila makusudi ili mdahalo uliotia fora sana wa SLAA usirudiwe tena kwenye TV yeyote hapa nchini mpaka uchaguzi upite.

Unadhani watu wapo intrested kusikiliza maneno yasiyokuwa na takwimu?

Timu ya Kinana imewarubuni waandaaji wa mdahalo huu ili Kikwete awe mgombea wa mwisho kuzungumza kwenye TV leo ili ujumbe wake ubaki kwenye akili za Watanzania siku ya kupiga kura Jumapili.

SWALI: Ngurumo wa Vox Media ambao wanaandaa mdahalo huu kwa nini anaruhusu hujuma hii yote dhidi ya SLAA?

Siku zote watu tunatakiwa tuangalie mkate uliopakwa siagi jamaa amesoma alama za nyakati amejua kuwa ni ndoto za mchana kwa mgombea wetu kushinda.

Naomba kuwasilisha...

Wasilisha na mjiandae kwa matokeo.
 
Wana JF what i want to know, ni kwa jinsi gani haya maoni yetu yanaweza kuwafikia hawa " Majuha" mbumbumbu na wavivu wa kufikiri? Mwenye email ya white house jamani tupeane nitajitoa mhanga kuwa natuma hizi posts.
 
Unfortunately mleta hoja..kwenye siasa hayo yapo, sina ubaya nayo, ninachoogopa ni wizi wa kura tu!!! Kwani mwizi wa kura anaweza kuiba hata moyo au figo yako ili abaki madarakani

hayo ya midahalo hamna kitu kwani hata kikwete akisemea mwezini hana hoja, hana nguvu, amechoka, anasahausahau, ana flights of ideas na anahitaji kupumzika

wanamuonea bure wanaompeleka kwenye midahalo

binafsi bado naamini kikwete ameshikwa pabaya, ni mtu mzuri sana na anaitakia mema nchi, tatizo ni waliomzunguka
 
Nimepata taarifa kutoka kwenye chanzo ninachokiamini kuwa katika hali iliyojitokeza mkoani shinyanga jana, mwanza tena nako ni mambo yale yale. Wilayani ilemela, nyamagana ni zaidi ya wapiga kura 3000 wamejitokeza mara mbili. kiambatanisho ni hiki hapa. chekeni wenyewe.

My take, kwa nini vyama vya upinzani visiweke pingamizi uchaguzi usifanyike?? Au sheria nayo imejaa viraka hata hapo kweupe?
 

Attachments

  • Doc1.docx
    712.1 KB · Views: 36
Unfortunately mleta hoja..kwenye siasa hayo yapo, sina ubaya nayo, ninachoogopa ni wizi wa kura tu!!! Kwani mwizi wa kura anaweza kuiba hata moyo au figo yako ili abaki madarakani

hayo ya midahalo hamna kitu kwani hata kikwete akisemea mwezini hana hoja, hana nguvu, amechoka, anasahausahau, ana flights of ideas na anahitaji kupumzika

wanamuonea bure wanaompeleka kwenye midahalo

binafsi bado naamini kikwete ameshikwa pabaya, ni mtu mzuri sana na anaitakia mema nchi, tatizo ni waliomzunguka

Contradiction. Hujielewi.
 
Tunaomba kura zenu tutimize ahadi zetu tulizowapa.
 

Attachments

  • ccm ccm.jpg
    ccm ccm.jpg
    10.6 KB · Views: 22
  • chagua kikwete.jpg
    chagua kikwete.jpg
    11.6 KB · Views: 23
mi nadhani kila kitu kinafahamika. tumechoka kutawaliwa na chama kilichoshindwa kumhudimia mtanzania wa kawaida. we need a change, lets not be fooled jamani
 
Huwezi kufanya mdahalo na waandishi wa habari!!! unafanya mdahalo na mpinzani
 
Back
Top Bottom