Huduma za Anuani za Makazi zinalipiwa?

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
617
1,799
Wakuu,

Nimekutana na hii stakabadhi mahali. Sina uelewa wowote kuhusu suala la malipo kwa huduma hii. Je, niandae buku tatu (3000) kwa ajili ya zoezi hili?

Anuani za Makazi.jpg
 
Nimelisikia hili huku mtaani kwetu, wananchi tunachangishwa 3000 elfu kwa ajili ya vibao vya namba vya anuanwi na postikodi ..Je wananchi wenzangu hii ni sawa ?
 
Watuambie kwanza pesa za kuzunguka na helcopta zinapatikana wapi, na pesa za vibao vya postcode zinakosekana wapi.
 
Nimelisikia hili huku mtaani kwetu, wananchi tunachangishwa 3000 elfu kwa ajili ya vibao vya namba vya anuanwi na postikodi ..Je wananchi wenzangu hii ni sawa ?
Hii sio sawa

Yule msigwa aliruka kweli aliposikia watu wanalipishwa.

Nape yupo kimyaaaa

Inabidi hawa watendaji wa chini walipwe mishahara.
 
Hapo hapo bado mwannchi anatakiwa achangie ujenzi wa shule 22 K , kituo cha polisi 10k> , bado kuna tozo huku za miamala, nafikiri maisha ya Tz kwa sasa ni magumu kuliko ya New york
 
Nimelisikia hili huku mtaani kwetu, wananchi tunachangishwa 3000 elfu kwa ajili ya vibao vya namba vya anuanwi na postikodi ..Je wananchi wenzangu hii ni sawa ?
Binafsi sitachangia chochote kwenye hili.

Tufikie kipindi tuwawajibishe hawa viongozi wetu.
 
Back
Top Bottom