Bukyanagandi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2009
- 11,626
- 18,227
Haiwezekani afunge safari yote hiyo kuja Kigali, na Kagame asijue. Sitashangaa kama yeye ndo kamruhusu ili Dunia ijue ukweli juu ya vita vya DRC
Huu ni mchezo wa kuigiza ulio chongwa na Utawala wa Rwanda kutaka kuadaa Dunia, hivi inaingia akilini kwamba mtu wanted dead or alive anaweza kuingia mjini Kigari bila ya kujulikana? mimi naona jamaa huyu kuna kitu ametumwa ili a-pre empty akiojiwa ICC i.e kuwakingia kufua watu fulani na kusingizia wengine; hasa hasa atataka kuonyesha kwamba vita vya Congo haviwezi kwisha kwa kutumia majeshi ya nje specifically kutoka nchi za SADC - mission yake nikutaka ku-instill FEAR kwa kusema mambo ya kutunga tu ili wapate kisingizio cha kuendelea kuikalia Congo.
Alafu Wamerikani walivyo wa ajabu wala hilo hawajarigundua wanafikili jamaa kazungumza na Mungu na kupewa amri ya kujisalimisha, mtakuja kuona kadiri siku zinavyo kwenda ndio ukweli utadhihilika kwamba kisanga kizima na michezo ya kuigiza tu.
Hata huyu aliye andika article hii ni mtu wa usalama wa Rwanda anaandika vitu ambavyo viko incoherent kwa kuwa alikuwa ajajipanga vizuri azungumze nini ahache nini!! Akili zake zote ziko geared kujaribu kuonyesha kwamba Zuma hafahi, Kikwete hafahi majeshi yao yana walakini, in short yuko obsessed na nchi hizi mbili za SADC kutokana na uwezo wao kijeshi na msimamo husiyo yumba, hivyo anafikili akijaribu kutisha watu eti mzozo wa Congo DRC utakuwa a mini-world war kwenye Region basi hilo tu litawakatisha tamaa wahusika, binafsi namuona ni scare monger tu ambaye amekwisha ng'amua kwamba mchezo yao inakaribia ukingoni. Hata hiki kisa cha wanajeshi 13 wa Africa Kusini kuuwawa huko Africa ya kati kinatia shaka sana, kwa nini kitokeee wakati UN imetoa kibali cha majeshi ya Tanzania na Africa Kusini kwenda DRC, kumbuka Africa ya kati na DRC zimekaribiana - je hii ilikuwa ni bahati mbaya au ni tactics za kujaribu kutisha Africa Kusini, I hope Zuma atapeleleza kwa kina na kujua the brains behind ya unyama huo.