Sijui hata nisemeje! Anyway......!
Dunia ina walimu wengi sana kwa uzoefu wa maisha yangu mafupi niliyoishi. Napenda watu wajifunze kutoka katika pande zangu zote,nzuri na zile ambazo mi naona sawa ila kwa baadhi ya watu sio sawa na zile ambazo ni mbaya hata kwangu mwenyewe.
Katika kila hatua ya maisha tunajifunza na kubadilika.....nilipotoka kwa wazazi kwenda bording school nilibdilika,nilipoenda chuo nikabadilika,nilipoanza kazi na kujitegemea kabisaaa nikabadilika,unasoma vitabu unabadilika,tamthiliya hizi,kutembea,mitandao ndo usiseme...nadhani ni sehemu ya maisha.
Kwa kuiga yaliyo mema na mabaya kote nilijifunza na nitaendelea kujifunza. Sipendi na sitaki kuishi maisha ya mtu mwingine, ila tunaweza jifunza na kufundisha watu wengine kwa mazuri na mabaya yetu.
Ukweli sina namna ambayo ninawaza kujitambulisha kwa vijana wenzangu....ILA mambo muhimu kwangu, kujipenda mwenyewe,kuwapenda wenzangu,kusaidia jamii kwa kile nilicho nacho kama ni information,ujuzi,network nk,kuheshimu watu,kufanya kazi kwa bidii na uaminifu na zaidi ya yote kujitahidi kumpenda Mungu kwa uwezo wangu mdogo ninao weza. Atakayeona ni sawa hivyo ewaaaa na ajifunze hayo kutoka kwangu.
Walimu wa maisha wamekuwa mno wengi,nitatoa mfano mdogo....hapo nyuma niliwahi mwambia aunt yangu kwamba nina rafiki wa kiume,akaniuliza kabila na kazi yake nikamwambia.....hakufurahi,akaniambia wewe shule umeenda ila umetoka bure,akanipa mfano wa kaka mwingine ambaye yeye kwa maono yake ndio ananifaa.....nikamsikiliza nikatulia,nikaenda kwa mama akaona tofauti na sababu akatoa.....marafiki zangu nao kwa experience zao wakajieleza....mwisho wa siku nikagundua,mwalimu wetu si mmoja,lililo jema kwangu,la busara silo la aunt wala marafiki,kila mtu apime na ajifunze kutokana na makosa.... at the end of the day....amua tu uonavyo sawa....ila uwe na furaha na usiumize mtu kwa kukusudia.