How are you examplifying yourself to the younger generation?

How are you examplifying yourself to the younger generation?

Umemnukuu mtu aliyeninukuu mimi na ukazungumzia jambo nililolizungumzia mimi hapo awali.

Au kuna mwingine alilizungumzia hilo jambo zaidi ya mimi?
So???Unataka kumjibia ama???Mimi sijaongea na ww ningedhamiria kukuandikia ww ningekuandikia ww!!Mbona sehem nyingine zote nimekujibu nilipotaka kukujibu??
 
Kuna watu wapumbavu kabisa humu. Kwa kuangalia tu mabandiko ya watu kwao inatosha kujifanya wanaujua umri wa mtu.

Na kudhihirisha zaidi upumbavu wao, mtu unaweza hata ukatunga stori tuseme ya mwaka 1983 ukiwa Canada ukisoma shahada yako yako ya uzamili na hao wapumbavu wakaingia mkenge na kujifanya wanaujua umri wako kwa kuona tu umeandika hivyo.

Na hapo hata hawakujui, hawajawahi hata kukuona, hata ulichokiandika hawana uhakika nacho, lakini wanafikia hitimisho la kujifanya wanaujua umri wako.

Kibaya zaidi unakuta wanajiaminisha kabisa kuwa wanachokisadiki ndicho sahihi. Huo ni zaidi ya ujuha na ujinga. Ni upumbavu maradufu.

hivi Ngabu huwa unasamehe? Au hata kupuuza? Hii kitu ni kama ilikugusa sana maana kila itokeapo fursa huwa unakumbushia. Ni mtu tu alikuwa anajaribu kukisia haiba za watu kwa kuangalia miandiko/michango yao. Sasa kama aliona michango yango imeshiba uzoefu na hekima akaona uko kwenye 60s kumbe labda uko 30s. Sidhani kama ni jambo la kuudhi namna hiyo. Ilikuwa changamsha genge tu wala si thesis. Take it easy. (hapa nshachuchumaa...maana...)
 
I usually don't put much stock into first impressions.


Think about it, what if you meet me on a day when things aren't going well and I'm kind of discombobulated and all that jazz.

hahahahaaaaa....."discombobulated" Aisee you are not even in 60s but in 70s. Ni vijineno kama hivi tu vinafanya wenzio wakuone babu. Wengine humu wakiandika zile "xana" zao tunahisi ni teeagers hata threads zao hatuendelei kusoma kumbe si ajabu ni watu wa 50s wanagoma kuzeeka!
 
unaweza kuelezea nini maana ya kujitambua na ueleze ni vigezo gani unavitumia kujua kuwa huyu anajitambua au hajitambui
rafiki, kujitambua kwa maana, kuishi kutokana na elimu, mazingira na umri wako, hapo ni kwa ufahamu mdogo tu...
 
Nimejifunza mengi kupitia huu uzi,
Sina lakuongezea maana mmeongea ya muhimu sana
 
That is very true. I know myself better than anyone else and I know I have the responsibility of doing good to the youngsters. That said, I try my best to have an honest and simple life, without provoking the ones under me morally.

I do not accept the idea that someone should look up to me and aspire to be like me. Singling me out as an example limits his/her breadth and capability. Furthermore, since they arent in my shoes they might probably be selective of the aspects of my life that inspire them without really knowing what it takes and what it costs. This is a blunder as the two sides go together. In fact, most people who have role models are not informed about this sector of their role model's life or career or success. They simple generalize hastily that they want to be like whoever it is. Unless you know that person (or his/her relevant career or success story e.t.c) comprehensively and he or she has been completely honest and open with you all along, you can not and should not dare use him/her as a role model.

Otherwise, misleading statements like "Do as I say and not as I do" or "Copy the favorable and discard the others" will prevail.

I would rather tell a kid to create his own dream and build it rather than folllow someone's or my own footsteps without extensive and doubtless knowledge of the path. Circumstances always differ.

My inglish is maimuna so i will speak kiswahili. Nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa hasa aya ya kwanza. Hiyo ndo "role modeling" yenyewe. Mimi sasa kama mtu mzima na kama mama nimegundua kuwa haiba ya mtu inachangiwa kwa kiasi kikubwa na anachokiona kwa macho yake kuliko anachoambiwa afanye. Mfano , nikiwa mdogo nilikuwa nikimuona mlezi wangu aking'oa magugu mabaya (makengere) kwenye mashamba ya watu asiowajua. Tukipita tu karibu na shamba akiona hilo gugu anaingia shambani, analitoa, tunaendelea na safari. Akiona uchafu anaoweza kuuokota na kutupa panapofaa zaidi anafanya. Leo hii mimi nikiona taka zimezagaa nakasirika, nikiona mtu anatupa taka hovyo namtoa maanani, nikikuta maji yanamwagika sehemu kama ni koki imeachwa wazi nitafunga, kama ni taa nitazima. Sikufundishwa kwa mdomo bali niliona. Na wakati ule sikujua kama ubongo ulikuwa ukirekodi kwa matumizi ya baadae. Jana nikiwa mahali na mtoto wangu wa miaka 7 nilinunua gazeti. Wakati wa kuondoka nikabeba pochi gazeti nikaliacha. Mtoto wangu akaniambia kwa sauti ya juu "hili gazeti unamwachia nani?" Nikamjibu "si wewe?" Akaniambia "mimi nina mikono mingapi? nitabebaje gazeti wakati naenda washroom?" Waliokuwa karibu wakageuka kuniangalia. Mie kwa aibu nikaenda kuchukua gazeti huku nikimwambia mtoto "sikujua kama unataka kwenda washroom". Hili tukio lilinisononesha sana. Mtoto wangu hakuzaliwa hivyo. Ameiga hiyo tabia toka kwangu. Hivyo ndivyo ambavyo huwa namsemesha - kwa ukali ukali. Tulivyofika nyumbani ilibidi nimuombe radhi kwa tabia yangu hiyo, nikakiri kuwa ni mbaya na asiige na mimi nitajitahidi kubadilika.

Kujua kuwa role models wetu walipitia vichochoro gani mpaka wakafika hapo walipo sidhani kama ni jambo la msingi sana. La msingi ni kuwa tayari wako pale na kuna mtu anataka kuwa kama wao. Mimi katika taaluma yangu kuna watu watatu ninaoweza kusema wamenifanya niwe nilipo. Mmoja nilimuona nikiwa darasa la 3, mwingine nikiwa la 6 na mwingine nikiwa chuo kikuu. Sijui walikopitia ila niliwakuta wameshakuwa, na mimi nimeshakuwa kama wao ila kivyangu na wawili kati yao nimeshawaacha mbali. Sikuwa kama hawa watu watatu kwa sababu yao, la hasha, nilikuwa na ndoto yangu lakini katika kuifanya ndoto iwe ukweli kunatakiwa kuwa na mazingira rafiki ikiwa ni pamoja na watu wa kukusaidia moja kwa moja au kwa mbali.

Wazazi na walezi wengi kwa kutojua nafasi ya "modeling" kwa watoto wetu tumeishi maisha mabaya ambayo yamesababisha vidonda na kuzaa tabia mbaya kwa watoto. Wengine athari hizi za malezi tunazigundua tumeshakuwa wakubwa na pengine tukiwa tumeshaharibu na ni wachache sana wanaoweza kutafuta chanzo na kurekebisha. Kutokana na mimi kutokea kuwapenda watu fulani kiasi cha kupenda nije kuwa kama wao, nimejifunza kuishi kwa uangalifu kwani sijui nani mwingine ananiangalia ukiacha mtoto wangu ila ni hakika kuwa yupo. Pengine tumeshaharibu maisha ya watu bila kujua na tumeshajenga maisha ya watu bila kujua.

La muhimu kabisa ni kulea vizuri watoto waweze kujitambua. Kuna mtu kasema aliona watoto wamelelewa vizuri walipofika vyuoni wakabadilika kiasi cha kuwashangaza walezi. Hao watoto hawakulelewa vizuri bali kwa woga. Mtoto afundishwe jema na baya na matokeo ya kila moja.Tuwape misingi ambayo haitatuweka roho juu watakapoanza kujua mitandao au kwenda vyuo. Ni ngumu lakini tukitambua uzito wa nafasi yetu kama walezi tutatafuta kila njia tuweze kufanikisha.
 
Are we brainwashed?

Ofcourse we are brainwashed. Tukubali au tukatae, mambo tunayoyaona kwenye TV na internet yanatufanya tutake kuyafanya na mengi yake sio mazuri. About ten years ago, ilikua taboo kuzungumzia sex shuleni, ila now everyone; girl or boy wanaona ni order of the day. Boys are bragging about their conquests and girls gossip day in day out about their encounters with different men.

Kubadilisha sio rahisi, ingawa na mimi nashare na wewe hayo mawazo na masikitiko, tulipofika kureverse is very hard. Wengi yanaingilia sikio moja, yanatokea sikio lingine, na utandawazi ndo unazidi kuja kwa kasi. We can try to set good examples, but how many of us will last? Masikini sisi...
 
Mwalimu Mkuu wa mtoto ni maisha.

Kama hakupenda kusoma hata kwa viboko, maisha yatamfundisha pole pole kila siku umuhimu wa elimu.

Kama tabia yake ni mbaya, maisha yatamnyoosha.

Mzazi ana wajibu wa kufundisha tabia nzuri kwa vitendo. Mzazi ana wajibu wa kumpa mtoto elimu, mazingira mazuri na salama ya kuishi, upendo na chakula bora.

Lakini mwisho, Mwalimu Mkuu wa mtoto ni maisha.
 
Mwalimu Mkuu wa mtoto ni maisha.

Kama hakupenda kusoma hata kwa viboko, maisha yatamfundisha pole pole kila siku umuhimu wa elimu.

Kama tabia yake ni mbaya, maisha yatamnyoosha.

Mzazi ana wajibu wa kufundisha tabia nzuri kwa vitendo. Mzazi ana wajibu wa kumpa mtoto elimu, mazingira mazuri na salama ya kuishi, upendo na chakula bora.

Lakini mwisho, Mwalimu Mkuu wa mtoto ni maisha.

Nakubaliana na wewe sana isipokuwa mstari wa mwisho. Siyo kwamba mwalimu mkuu ni mzazi?labda na taasisi zingine za socialization halafu maisha ni mtihani? Kujifunza kutoka kwenye maisha kunatakiwa kuchukue sehemu ndogo sana. Utafanya mambo mangapi kwenye hayo maisha ili ujifunze? nadhani tunahitaji kanuni tu maana kweli hakuna mzazi/mlezi anayeweza kutupa a, b, c,d za kila kitu. Kama mzazi kuna wakati unachoka kumuambia mtoto acha. Ukiona habadiliki unapima hatari ya kile kitu unachomuambia aache. Ukiona kwa mfano unahofia ataanguka na ataumia lakini hatavunjika unamuacha tu apande, aanguke, aumie ili ajifunze. Taratibu mtoto ataanza kujua kuwa kila kitu atakachofanya kina matokeo. Lakini kuna mambo ya msingi sana huwezi kumuachia mtoto afunzwe na maisha. Mfano huwezi kumuacha aonje sumu au hata kuikaribia ili aone kukata roho kunavyouma. Aisee hata kama jela itasaidia kumfundisha hicho kitu kama unajali utampeleka. Mtoto anayefunzwa na ulimwengu anaumia sana ukilinganisha na mtoto ambaye mzazi/mlezi amempa uwezo wa kupambana na maisha.
 
Nakubaliana na wewe sana isipokuwa mstari wa mwisho. Siyo kwamba mwalimu mkuu ni mzazi?labda na taasisi zingine za socialization halafu maisha ni mtihani? Kujifunza kutoka kwenye maisha kunatakiwa kuchukue sehemu ndogo sana. Utafanya mambo mangapi kwenye hayo maisha ili ujifunze? nadhani tunahitaji kanuni tu maana kweli hakuna mzazi/mlezi anayeweza kutupa a, b, c,d za kila kitu. Kama mzazi kuna wakati unachoka kumuambia mtoto acha. Ukiona habadiliki unapima hatari ya kile kitu unachomuambia aache. Ukiona kwa mfano unahofia ataanguka na ataumia lakini hatavunjika unamuacha tu apande, aanguke, aumie ili ajifunze. Taratibu mtoto ataanza kujua kuwa kila kitu atakachofanya kina matokeo. Lakini kuna mambo ya msingi sana huwezi kumuachia mtoto afunzwe na maisha. Mfano huwezi kumuacha aonje sumu au hata kuikaribia ili aone kukata roho kunavyouma. Aisee hata kama jela itasaidia kumfundisha hicho kitu kama unajali utampeleka. Mtoto anayefunzwa na ulimwengu anaumia sana ukilinganisha na mtoto ambaye mzazi/mlezi amempa uwezo wa kupambana na maisha.

Kama ulivyosema, wazazi hatuwezi kuwapa a,b,c,d za kila kitu. Kuna watoto wengine ni wabishi, hawafundishiki na hawasemesheki.

Siyo watoto wote wana ujuzi wa kunyonya elimu kutoka kwa mzazi. Siyo wazazi wote wana elimu ya kuwapa watoto.

Mtoto anaweza kulikimbia na kulidharau somo la mzazi lakini hata siku moja hawezi kulikimbia na kulidharau somo la maisha.

Hapo mwanzo aliweza kuondoka/ kutoroka nyumbani kifua mbele akijua atayaweza peke yake huku akikufokea moyoni.

Maisha yalimfundisha. Mzazi kama mwalimu hawezi kushindana na mwalimu dunia. Kuna watoto wabishi, hawakuelewi, hasa hawa wa kizazi hiki cha FB na Whatsapp, lakini, mbele ya mwalimu dunia, wananyooka na kutubu au wanakwenda na maji.
 
Back
Top Bottom