Housemaid ananipigia simu kuuliza nipo wapi!

Housemaid ananipigia simu kuuliza nipo wapi!

pakaywatek

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
4,710
Reaction score
6,372
Miezi kadhaa imepita tangu niwe nae ambapo mama alimleta ili anisaidie kwa kuwa nina mtoto mdogo ambae nilimchukua kwa mwamamke ambae alikuaga mpenzi wangu tukaachana.

Ninachomshukuru ni kwamba amekua mwema kwa mtoto kiasi kwamba sijaona pengo la mtoto kutokua na mamake karibu hata mimi nimefarijika kwa huduma za ndani ambapo nikitoka sina wasiwasi huko nyuma.

Sasa kuna tabia kaianzisha ya kunipigia simu ikifika saa 2usiku ya kuniuliza niko wapi na nitakuja saa ngapi, hii kweli ni haki? Naogopa kumfokea anaweza kimbia akaniacha na mtoto ukizingatia pia nakaa na mdogo wangu wa kiume ambae anasoma.

Naombeni mnishauri nitumie njia ipi nimkanye kabla mambo hajaharibika.
 
Dogo anakula mzigo.so anataka kukadiria muda wa wao kumaliza mambo yao hadi wewe kufika hom.
Fanya majaribio siku moja mwambie ntarudi saa tano alafu ikifika saa mbili rudi hom kimya kimya.kama una gari paki kwa jirani.utapata majibu tu.
 
Kama Anamlea Mwanao Vizuri Na Wewe Anakuonyesha Kukujali Huyo Ni Mwanamke Mwema...Muhamishie Chumbani Kwako Awe Mkeo Maisha Yenyewe Ndio Haya Haya Aisee...

Usisahau Kumuweka Sopu Sopu
 
ninachomshukuru ni kwamba amekua mwema kwa mtoto kiasi kwamba sijaona pengo la mtoto kutokua na mamake karibu hata mimi nimefarijika kwa huduma za ndani ambapo nikitoka sina wasiwasi huko nyuma.

Hapo tu ndipo kwenye tatizo.

Tofautisha kati ya Heshima na Huruma. Yeye kama ni mtumishi wako wa ndani(mheshimu lakini mipaka iwepo), Pengine ni kwa nia na lengo zuri lakini kwanini umuache kiasi kwamba ionekane hata mtoto hana pengo la kumkosa mama yake? Dont get me wrong sisemi mtoto awe mkiwa ila kwa kuanza kumfikirisha yeye ni mama wa mtoto(kwa maelezo yake) she assumes the rest!
 
She cares, whats the fuss about it?

Umezoea maisha ya ghetto, hapo ni nyumbani kwako.

She starts being responsible for you and the family.

Nasubiri aanze kukutandika bakora ukikosea au kuchelewa.
 
Hapa tutakuwa tunaeleza mambo kwa upande mmoja,maana hatujui kwa nini anafanya hivyo.
 
Dogo anakula mzigo.so anataka kukadiria muda wa wao kumaliza mambo yao hadi wewe kufika hom.
Fanya majaribio siku moja mwambie ntarudi saa tano alafu ikifika saa mbili rudi hom kimya kimya.kama una gari paki kwa jirani.utapata majibu tu.

Kula like mkuu huo ndo ukweli wenyewe
 
Si mchukue tu awe mkeo, inaonyesha anafeeling na wewe.
 
Hapo tu ndipo kwenye tatizo.

Tofautisha kati ya Heshima na Huruma. Yeye kama ni mtumishi wako wa ndani(mheshimu lakini mipaka iwepo), Pengine ni kwa nia na lengo zuri lakini kwanini umuache kiasi kwamba ionekane hata mtoto hana pengo la kumkosa mama yake? Dont get me wrong sisemi mtoto awe mkiwa ila kwa kuanza kumfikirisha yeye ni mama wa mtoto(kwa maelezo yake) she assumes the rest!
Word Mkuu...
 
Miezi kadhaa imepita tangu niwe nae ambapo mama alimleta ili anisaidie kwa kuwa nina mtoto mdogo ambae nilimchukua kwa mwamamke ambae alikuaga mpenzi wangu tukaachana.

Ninachomshukuru ni kwamba amekua mwema kwa mtoto kiasi kwamba sijaona pengo la mtoto kutokua na mamake karibu hata mimi nimefarijika kwa huduma za ndani ambapo nikitoka sina wasiwasi huko nyuma.

Sasa kuna tabia kaianzisha ya kunipigia simu ikifika saa 2usiku ya kuniuliza niko wapi na nitakuja saa ngapi, hii kweli ni haki? Naogopa kumfokea anaweza kimbia akaniacha na mtoto ukizingatia pia nakaa na mdogo wangu wa kiume ambae anasoma.

Naombeni mnishauri nitumie njia ipi nimkanye kabla mambo hajaharibika.

Mshukuru Mungu amekupa huyo dogo.

Mara nyingi sisi wanaume tukiwa na uhuru sana tunaboronga na kwa mwanao nadhani ni sahihi ukawahi kurudi home maana mzazi mwenzio hayupo huyo binti ni kiraka tu inabidi ujisogeze kwa mtoto upate muda naye siyo kila siku wewe kiguu na njia mtoto atakosa mapenzi ya wazazi siyo vzr.
 
Kama Anamlea Mwanao Vizuri Na Wewe Anakuonyesha Kukujali Huyo Ni Mwanamke Mwema...Muhamishie Chumbani Kwako Awe Mkeo Maisha Yenyewe Ndio Haya Haya Aisee...

Usisahau Kumuweka Sopu Sopu

Hahahaaa Huyu anashindwaje kusoma alama Za nyakati?
 
Labda anataka kujua kama unakaribia kurudi ili ajue mtoto alale au asubiri kidogo ili angalau akuone
Labda anataka kujua aanze kukuandalia chakula au asubiri zaidi
Labda anataka kujua utachukua muda gani ili waji vinjari na dogo

Hizo zinaweza kuwa baadhi ya sababu. Ila ukitaka kujua, akikupigia muulize kwa nini anataka kujua, halafu mwenyewe pima kama ni haki au sio.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom