Katika dunia tunayoishi kuna watu wamejaliwa kuwa matajiri na wengine ni masikini. Wapo mameneja wengine wahudumu. Huku mfyagizi kule CEO. nk nk.
Kuna wakurugenzi na walinzi. Huku makarani kule maafisa. Hapa makamanda kule makuruta. Huku wachungaji kule wanakwaya. Ilimradi watu wapo katika madaraja tofauti.
Ndio hadithi ya maisha ilivyo. Wengine wapewa maisha mazuri wakati wengine ni walalahoi.
Bill Gates anasema life is not fair. Get used to it. Tofauti za maisha zitakuwapo siku zote lakini zisitufanye tunyanyasane. Ingawa tunasema binadamu wote ni sawa lakini ukweli ni kwamba tuko sawa lakini 'sio sawasawa'
Familia nyingi kuanzia tabaka la juu, kati na hata la chini huajiri house girls ili kusaidia kazi za nyumbani.
Sehemu kadhaa wasichana hawa wamekumbana na mateso na manyanyaso kutoka kwa akina mama tena wengine wenye heshima katika jamii wakiwemo wachungaji nk.
Wasichana hawa huishia kutukanwa na kusimangwa kila mara. Kunyimwa chakula au kupewa makombo. Sehemu zingine hawaruhusiwi kukaa kwenye makochi!
Familia nyingi dada wa kazi huwa wa kwanza kuamka na wa mwisho kulala. Hutengwa wakati familia inakula na ni mara chache sana wanaruhusiwa kutoka.
Hulazimika kufanya kazi nyingi sana ingawa mshahara ni mdogo sana na kulipwa kwake kwa manati. Inashangaza kuona baadhi ya akina mama wanaonyanyasa house girls ni Wakristo au Waislamu. Wanafiki!
Tatizo kubwa ni kwamba kisaikolojia, jamii inawaona house girls kama ni watu daraja la pili. Hili ni kosa kubwa. Kuwa house girl au house boy hakumfanyi mtu kuwa binadamu nusu.
Ni fate tu imewafanya dada hawa kufanya kazi hizi. Wasinyanyaswe. Mama muone dada wa kazi kama binti yako.
Ni ujinga kumnyanyasa mtu anayekupikia chakula na au kukutunzia watoto wako. Unajiweka katika mazingira ya hatari. Usijenge uadui na house girl. She can be your doom.
House girl sio punching bag. Sio mtu wa kumalizia hasira zako za kazini au kero za mume. Wewe si binadamu bora zaidi kuliko huyo msichana.
Wewe pia ungeweza kuwa house girl shukuru tu fate imeamua vinginevyo. Aliyekupa wewe ndio aliyewanyima wasichana wa kaazi.
Anaitwa msichana wa kazi sio mtumwa. Alipwe ujira wake na heshima ya utu wake ithaminiwe kama watoto wako.
Ingawa nimesema kidunia binadamu sio sawasawa, mbele ya Mungu watu wote ni sawa. Tunaunganishwa na kifo. Uwe mkurugenzi uwe nani utakufa kama huyo msichana unayemnyanyasa.
Acheni kuwafanya house girls watu daraja la pili. Acha visingizio. Kama umeshindwa kuishi nae kwa upendo na staha mrudishe kwao. Period.