Hotuba za Rais Magufuli za kichwani zinakera, asome hotuba anayoandaliwa

Speech za Rais Magufuli zinashida kidogo, Rais akizungumza anazungumza kama mtu aliyejaa visasi na sifa nyingi, hana utaratibu mzuri katika kupangilia kile anachokisema.

Kama rais anapaswa kuzungumza kwa utaratibu na mpangilio hata kama ni sehemu anasisitiza jambo, vijembe kwa walio chini yake ni kutafuta tu kick kwa wananchi ambao mwenyewe keshatujua na amejawa na sifa tunazompa kila siku. Rais ni reflection ya watu alionao.
Inaonekana hutend haki wale wote ambao hawatend haki lazima umchukie magufuli,siung hoja hata kidogo
 
Wa
Exactly.


Exactly. Wanaopinga style ya Rais kufikisha ujumbe ni wanafiki na huenda ni majipu. Rais anazungumza kwa lugha tunayoelewa na hiyo ndiyo maana ya KAZI TU na siyo michakato, mipango mkakati, upelelezi haujakamili kamnunulia nk. Tawala zilizopita ndizo zimetufukisha hapa tulipofika. How can you pay a CEO of a public Corporation pay himself 35m/=m salary per month in a poor country like ours. Acheni mzaha!
wapo wengi wanalipwa mshahara huo huo tena pia ni Mafisadi yaani hawashibi bado wanataka zaidi, wasomi wa Tanzania ni Tofauti na wasomi wa Nchi zingine ambao hutumika kuleta maendeleo kwenye Nchi zao,wasomi wa Tanzania kazi yao ni kuiba pesa kwa njia za kalamu wanasomea Ufisadi ni Hatari sana.
 
Hatutaki maspeech yasiyo na tija. kama serikali yake inafanya madudu si amalizane nao aje kutupa feedback?
 
Sina hakika kama nakubaliana na wewe Mkuu. Watu wengi wanamwelewa sana, pengine ni tatizo lako tu. Tumuunge mkono kwani mengi anayofanya yana maslahi ya Taifa.
 
hiyo mipangilio ndio imetufikisha hapa, nyingi zenye mipangilio huwa hazijajaa uhalisia.

anachotaka watu wake wajue ni kuwa chini ya magufuli wanaoption mbili. kuwa msafi au kuondoka.
Nakumbuka hotuba za ben za mwisho wa mwezi hata ukiulizwa alikuwa anaongelea nini watu wengi walisha sahau wanakumbuka misamiati maalufu kama MICHAKATO na TIJA

Unachosema Mkuu ni sawa na ni muhimu. Tukirudi kwenye context ya mleta hoja, Mkuu wetu anajisahau, anatoa amri/maagizo ya kisiasa kwa mambo ya kitaaluma. Mfano: Unapomwambia Jaji Mkuu watu hawa wafungwe, wakati wewe ni boss wa jaji huyohuyo kwangu mimi mtu wa kawaida ina maana Rais amekwishatangaza hukumu kwa mtuhumiwa huyo na anapaswa afungwe tu. Aidha unapomwambia Jaji mkuu kuwa wafungwe watu hao ili nipate tril.1 na nikiipata nitakupa 250bil si anawahimiza majaji na mahakimu kupindisha mambo ili tu waambulie 250bil? Ana sense of humor nzuri, anazungumz vizuri, kiingereza cha kuchomekea kibovu, anaonyesha uzalendo kwa nchi yake, anachukia uhalifu, anataka sheria zifuatwe huku yeye mwenyewe akzivunja! anaingilia mhimili mwingine wa dola. Kuwa Rais si kuwa juu ya sheria zote
 
Hotuba zenye mpangilio za mtangulizi wake ndo zimetufikisha hapa,ebu ngoja na yeye ajaribu hiyo style tuone kama kama tunaweza kusogea kidogo.
 
Mtanyooka tu,
alikuwepo jk anawaongelesha kwa upole na kuwapet pet.mkamwita dhaifu.

Sasa kaja mkakamavu,mtulie mnyolewe
 
Speech za Rais Magufuli zinashida kidogo, Rais akizungumza anazungumza kama mtu aliyejaa visasi na sifa nyingi, hana utaratibu mzuri katika kupangilia kile anachokisema.

Kama rais anapaswa kuzungumza kwa utaratibu na mpangilio hata kama ni sehemu anasisitiza jambo, vijembe kwa walio chini yake ni kutafuta tu kick kwa wananchi ambao mwenyewe keshatujua na amejawa na sifa tunazompa kila siku. Rais ni reflection ya watu alionao.

Kwa uzoefu upi ulionao? Uliwahi kuwa Rais wa kitu gani huku duniani au unaongea nadhari na njozi tupu? Kwa hiyo kejeli, mipasho na ngonjera za boys 2 men wa msoga kwako ndio uongeaji unaokonga roho yako?! JPM anaongea kwa hisia kwa sababu ya madudu yaliyolelewa na boyz 2 men wa msoga; na hicho ndio kinachokonga nyoyo za watu wengi wenye akili safi na wasio wanufaika wa miaka 10 ya ufisadi, rushwa na ujangili kama wewe! Tulia msumari ukuingie!
 
Mwaka huu speech za mbwembwe watu hawazitaki wamechoka kusikia Maneno Maneno yasiyo na tija huku mlundikano wa kesi na wafungwa ukiwa mkubwa, kwenye kero kubwa zaidi ni kero ya Kesi za Ardhi, viwanja na nyumba huko kuna usumbufu mkubwa kesi nyingi huchukua miaka mingi sana kumejaa Rushwa na kila aina ya Uozo, tunashukuru Magufuli kwa kuyaona hayo tunaomba hayo Maneno uliyotoa yafanywe kwa Vitendo wasiendelee kupiga tarehe kila kesi kama kawaida ya mahakimu na majaji wengi wafanyavyo.tunakuomba Mh Rais kila Mahakama zifungwe cctv camera na Mfumo wa file uangaliwe kwa jicho la tatu kutokana na makarani kugeuza file ni miladi yao ya kujipatia fedha za rushwa.
 
Wabongo nyie vilaza kweli mntaka muongozwe na wasanii? JPM sio msanii wala mpga dili wala sio tapeli kama wahuni wenu waliopita.
Hapa lazima nchi iende kimadili uswahili na uhuni wote lazima tuuzike rasmi,

Kinachotusumbua watz ni hiki unachosema hapa! Hoja iliyoletwa haina uhusiano na unayosema! Soma vizuri anayosema mleta hoja kisha zungumza kwa hoja. Hakuna aliyesema JK ni mzuri. Hakuna aliyesema tunamhitaji msanii mwingine, hakuna aliyesema JPM ni mpiga dili na tapeli bali ndugu anazungumzia speech yake haijakaa kirais rais... anapayuka mno! Anatoa maagizo pasipostahili, anajaribu kujisifia au kutafuta sifa za watu wengine. Aache watu wamsifie kwa kazi zake. Azungumzie vitu material sawa na Rais.
 
Katika watu waliotengeneza uchumi wa Kenya ni Rais Mwai Kibaki.

Hana kipaji cha kutoa hotoba za kufarahisha genge. Ni aina ya watu wa Hapa Kazi tu. Waanafikia na watu wakujipendekeza hawakutaka hata kidogo. Hotuba nyingi zilijaa neno mavi ya kuku, akiwatukana watendaji wabovu. Sasa wanaye Uhuru Kenyatta. Hotuba nzuri zenye mpangilio mzuri wa maneno lakini rushwa imepaa kweli kweli Kenya.

Watanzania tuchague tunataka nini. Hotuba nzuri zenye bla bla nyingi lakini hamna hata moja linatimizwa au hotuba "mbovu" lakini matunda yake kiuchumi na kijamii yaonekane.

Sijui katuloga nani, kufurahia ujinga usio na tija.
 
Kweli ss watanzania tuna shida kichwani..... Cjui akae nani asiletewe dosari.
nidaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa hivi naomba kuuliza mbona vitambulisho vya kura was rely simple kutupatia hivi vya uraia tatizo ni nini au ndo kutengeneza mazingira ya kula pesa za watanzania?



huu mradi ufungwe maana hauna tija
 
Tuna mitazamo na uelewa tofauti,kwangu mimi ukiondoa baba wa taifa hakuna raisi mwingine ambaye ningeweza kukaa na kusikiliza hotuba yote hadi mwisho bila kuwa bored,kwangu Magufuli akianza kuhutubia natamani asimalize,hotuba zake zina uhalisia na zinagusa hisia tofauti na hotuba za zenye lengo la kufurahisha audience ambazo hazijawahi kutufikisha popote.
Sio mimi tu,jana nilikuwa kwenye bar moja kubwa sana,TV nyingine zote za mipira etc zilifungwa na watu wote walikuwa makini walimsikiliza magufuli na walikuwa wakishangilia mara kwa mara,watu walianza kuondoka bar baada ya Magufuli kumaliza hotuba yake.
 
Ila mimi hotuba zake napenda kuzisikiliza zinatia moyo hasa kwa sie wavuja jasho na inaonekana sooner or latter nchi itanyooka,inaumiza kama ulishazoea kuishi maisha ya kiujanja ujanja lakini ndio hivyo tena kasha kuwa raisi kwa hiyo tufuate sera anazozitaka,kama hotuba itaanza na point ya mwisho then amalizie ya kwanza au aanzie katikati amalizie na ya kwanza huo ni mpangilio tu lakini maessage inakuwa sent and delivered.
 
Halafu anaongea vitu irrelevant na mahala husika,inakera sana kuona mtu anahukumu mwenyewe.wewe umeshatuhumu,acha mamlaka zingine zifanye kazi


Washauri wake wamwambie ukweli. Kauli za Rais ni Decree, hivyo anachotamka ni lazima kitekelezwe, hapo ndipo umuhimu wa Mh Rais kushauriwa aina ya maneno ya kuzungumza na Public kusikia.
 
Kweli ss watanzania tuna shida kichwani..... Cjui akae nani asiletewe dosari.

Ni kweli ila si unajua JPM anaowaharibia ulaji wao pia tunao humu kwa namna moja au nyingine sisi nikumuombea tuu atende haki.
 
Back
Top Bottom