Hotuba yangu jimboni Kigoma

Duuu,

Yaani una maana kuwa hata vizazi vijavyo watakuwa kama sisi? Kumbe hii historia ni kweli:
Mao Zedong, JKN na Borris Yeltsin wameenda kwa Mungu ili kuuliza kule kwao hali itakuwaje in future:

1. Mao Zedong akaambiwa kuwa China inakwenda safi sana baada ya miaka 100, inakuwa super power duniani kwa kila kitu.

2. Borris Yeltsin akaambiwa Russia mambo yatakuwa bomba baada ya miaka kama 150 hivi.

3. Alipokuja Nyerere na swali hilohilo, Mungu akamwangalia na bila kusema neno akaanza kulia.

MASA,
Hapa jibu mwenyewe.
Nikijibu mimi naweza kuandika zaidi ya maneno millioni 10 nikimuonyesha umuhimu wa historia na kumbukumbu.
 
Duuu,

Yaani una maana kuwa hata vizazi vijavyo watakuwa kama sisi? Kumbe hii historia ni kweli:
Mao Zedong, JKN na Borris Yeltsin wameenda kwa Mungu ili kuuliza kule kwao hali itakuwaje in future:

1. Mao Zedong akaambiwa kuwa China inakwenda safi sana baada ya miaka 100, inakuwa super power duniani kwa kila kitu.

2. Borris Yeltsin akaambiwa Russia mambo yatakuwa bomba baada ya miaka kama 150 hivi.

3. Alipokuja Nyerere na swali hilohilo, Mungu akamwangalia na bila kusema neno akaanza kulia.

Mzee usisahau History gives glimpse into the future! upo hapo ...
http://www.runnersgazette.com/results/whal02.htm
 
Mkuu mimi sijui wewe ni mwenyeji wa wapi..lakini kama umekulia 'porini' kama wengi wetu ungemuelewa Mh. Zitto. Kwa mtu wa Kigoma hiyo barabara ina manufaa zaidi kuliko ya kwenda Tabora. Why? kwa sababu mtu wa Kigoma anafanya biashara na mtu wa Burundi na Congo..wengine wanazaliwa mpaka wanazeeka hajavuka mkoa wake wa Kigoma. Ingawa Burundi, Congo nk anakujua vyema kabisa. The same applies kwa mikoa mingine..kwa mfano mtu wa Ngara, Karagwe, Sirali nk..wanazijua nchi jirani kuliko watanzania wenzao. Na hii ni historical kwa sababu hiyo mikoa imesahaulika..viongozi wanaenda huko kuomba kura na kutoza ushuru tuu. .

Hivi unajua wakati mimi nakua..radio niliyokuwa naipata kwa uhakika ni KBC ya Kenya? ndo maana akina Mambo Mbotela mpaka leo nawakumbuka sana kuliko watangazaji wetu (majira ilikuwa inatufikia ila kwa taabu sana, mpaka uweke radio juu ya kichuguu). Sasa hapo unategemea nini?

Ukweli ni kwamba Tanzania haina vipaumbele..huwezi kudumisha 'umoja na mshikamano' kama watu hawana fursa sawa. Alichoongea Zitto si rahisi kumuelewa kama hujaishi hayo maisha in practical terms. Infact enzi hizo..ukienda Kigoma..hata bidhaa za Tanzania zilikuwa hazifiki...(hata siku hizi bia nadhani wanakunywa Primus ya Burundi zaidi kuliko bia za Tanzania..) kila kitu kilikuwa kinatoka Burundi na biashara ilikuwa inavuma sana. Muulize Zitto atakwambia... Kwa mtu kama huyo ukimuwekea barabara...mmemalizana..maana atafanya biashara zake...after all huko Tanzania iliko alishasahauliwa.

So in real world..barabara ya Mwandiga-Manyovu ina umuhimu mkubwa sana. Sasa hao wabunge wa mikoa ya kati ndo na wao wangehangaika wakapata barabara za kuwaunganisha na mikoa ya pembezoni kusudi wapiga kura wao wafanye biashara. Sijua RA mbunge wa Ndugu Sikonge anasikia huu ushauri wa bure?

Plan ya hii barabara ikikamilika itakuwa ni bomba sana; ila bado ujenzi wake ni mwendo wa kujikongoja; maana mpaka sasa sehemu kubwa ipo ktk kiwango cha kusawazisha (kuweka level) kwa kumwaga vifusi/udongo, kujenga madaraja/makalavati n.k.
Vile vile process hii imesogea hatua si kubwa sana kama watu wanavyodhani,maana mpaka sasa wala haina dalili ya kufika wilaya ya kasulu ambayo ndio ina mpaka na burundi.

Mheshimiwa mbunge anastahili pongezi zake kwa jitihada zake pamoja na wapiga kura wake but tusiwasahau Wakandarasi (China Hinen km cjakosea) wa hii barabara, wale wachina wamejitahidi sana ktk supervision ya hii project na wapo makini sana.

Vilevile kama mh. mbunge ataweza wakutane na wabunge wenzake kina nzasugwanko na wengineo cjui kina nani hao, wahakikishe ile barabara ya kasulu-kibondo-kahama itengenezwe, maana ndio kiungo muhimu cha kuingilia mkoa wa kigoma kutokea mikoa mingine ya Tanzania.

Tuvute subira nadhani baada ya muda si mrefu wakazi wa kigoma na mikoa jirani wataisahau adha ya TRL, watasafiri na NBS, Adventure, Saratoga at el kwa raha mustarehe bila ya kuonekana wamepakaa poda nyekundu (vumbi jekundu) wakifika safari zao.
Usafiri wa KGM/DSM, KGM/TBR na KGM/MWZ unataka moyo; vinginevyo uwe na nguo za spea ili mwisho wa safari yako ubadili vinginevyo ni kituko!!!

Mkuu ndo maana naamini mazingira tunayokulia yanatu-affect mbeleni. Ndo maana sielewi kwa nini watu waliokulia kwenye shida, WAKASOMA SHULE ZA WAMISSIONARY..leo tunawapa madaraka wanatusaliti. Kwa sababu hawa jamaa..na jeuri yao sasa..lakini walistruggle sana (baadhi) kufika walipo. Kwanini wasikumbuke walikotoka? Imagine mtu kama Mkapa..leo eti ni fisadi..Huyu Chenge..ni jirani yangu kabisa..anatoka familia choka mbaya kama wengi wetu humu..duh..hali inatisha..

Hii inanifanya niogope...itakuwaje hii nchi wakikabidhiwa watoto wa hawa mafisadi ambao wamekulia Oysterbay na Masaki? Kusoma wamesoma IST na Ulaya?? TANZANIA yao wanaoijua ni ile ya Dar Es Salaam? (akienda mbali ni Moshi na Arusha?). KAZI TUNAYO WADANGANYIKA...

Huu mjadala wa barabara ya Mwandiga na Manyovu..una expose mambo mengi sana. Watanzania wengi Tanzania halisi hatuijui. Mtu anadhani TZ ni Dar-Tanga-Moshi-Arusha. na sana sana Mwanza...Jamani kuna Tanzania nyingine ambayo ndo mh. Zitto anaiongelea hapa...na hiyo haijulikani!

na kuna Mwandiga-Manyovu nyingi tuu..sema hazina akina Zitto wa kuzisemea kunakohusika..

Ni kweli mkuu; watu hawatembei kabisa kuyajua maeneo ya nchi yetu.
 
MASA,
Hapa jibu mwenyewe.
Nikijibu mimi naweza kuandika zaidi ya maneno millioni 10 nikimuonyesha umuhimu wa historia na kumbukumbu.

Mkuu Makyao,

Huo ujumbe wa Masa ilikuwa JOKE. Kama haoikuwa JOKE basi mimi sioni hata haja ya kuweka kwenye VITABU. Ingelibidi iwepo Maktaba ya Taifa na Museum ya Taifa na hizi habari zote ziwe kwenye DVD, Blueray na HDs. Hizi zitadumu milele na milele zaidi ya mavitabu ambayo hata space yanachukua kubwa sana.

Sijui maktaba na Museum ya Taifa tunayo kweli na wanatunza habari kama hizi. Ila itabidi tuweke hadi za akina Kigunge wakipinga waraka wa Wakatoliki ili kuwaonyesha wajukuu zetu jinsi enzi hii watu kwa kupenda UFISADI, wanaweza kusema PUMBA hadi zinaleta RAHA. Hii ni kama lile jengo BAYA la UK ambalo wanafunzi wa Archetecture huwa wanapelekewa kwenda kuangalia jengo la OVYO na kuwaonya wasije wakawa wanafanya makosa ya namna hiyo.
 
MkamaP,

Kwenye SIASA mambo yako hivyo mkuu. Ukisikia mtu anasema mie sintampigia magoti fulani kwa kuwa yeye ni BIG MAN basi ujuwe magoti yake hadi yameota SIJIDA kwa kuyapiga. Heri ya Zitto kakiri waziwazi waliomsadia. Ila ya Cameroon ni kali maana hata kutoa Hongo inabidi uandike OMBI? Likikubaliwa ndiyo unatoa na hapo unapotoa unapiga magoti kuomba Mungu jamaa asibadili mawazo. Akipokea asante nyingi sanaa.

MkamaP, field ya Civil Engineering ukubali au ukatae, ni field moja ambayo MAFISAD. Kule kuna PESA na utafiti wake ni mgumu sana hasa kama wI wanaipenda sanaala 10%. Inapofika sehemu kwamba zipo pesa kidogo na mahitaji mengi, wakikupa wewe na kuendelea kumsahau Mkandara na Sikonge, basi inabidi uwape ASANTE. Kumbuka wengine tulipiga pia magoti na kuomba tutowe Hongo ila tukakataliwa vilevile. Matokeo yake Ukerewe na Sikonge ni Ndugu mmoja. Vipi kule kwenu, ile lami aliacha Nyerere bado ipo au ndiyo kuna mashimo kama vile mwajiandaa kujenga mahandaki?

Mkuu hapo ndipo panapogomba ngoma kama Chenge ije ikupe madili kwamba kuna vijifisadi vinataka kukufisadi .teh teh teh teh
Hako ka mstari haujakaona nini?.

Nikwambie neno Fisadi RA kafanya mambo makubwa jimboni kwake kupita karibu wabunge wote.wenda naye anamfuko wakusaidia yatima wengi ,tumpe makofi RA kwa hilo kwakwa kwa kwa kwa!!!

Kule kwetu mwaibara hatupokei misaada ya masharati ndio maana wengi wanatuona kama wakorofi
 
Ahsante Kichuguu kwa kuliona hilo, aksante.

Zaidi ya Mkapa na Vithlani, hakuna kichwa kinachotafutwa Tanzania kikajibu shutuma za ubadhilifu kama kichwa cha Andrew Chenge.

Zitto Kabwe, mbunge kiongozi wa upinzani, ameenda kuwaambia wananchi kwamba kwa kushirikiana na Ephraem Mrema aliyeilipisha TANROADS Sh bilioni 3.3 kwa kampuni illegal ya Norconsult na Zhakia Meghji aliyesaini makaratasi ya Billal wa EPA, Andrew Chenge amewajengea mabarabara!

Kana kwamba kina Zhakia Meghji na Chenge walifanya hisani kutoa hela, hela zinazopita kwa idhini ya Bunge.

Unalalamika Buzwagi, Buzwagi, Buzwagi halafu wakina Chenge waliosaini mikabata unaenda kuwauza kwa watu? Unasimama mbele za wananchi wenye disapointment na frustration unataja ``Chenge`` kwa ufahari kabisa?

Labda ni Waganda walikasirika mwaka '79 wakatutafutia dawa, au Wakenya walinyunyiza kimiminika na helikopta ili tupwelee tuwaachie ardhi, lakini kuna mkono wa mtu, hatuwezi kuwa wazima. Anamsifu Chenge hadharani?
Dilunga acha kutupa wasi wasi na uwezo wako....ina mana haujui kama kuna wakati shukrani inahitajika kwa watu waliofanya meme?... Dilunga kutuambia kuwa Zitto amewaambia wakazi wa Kigoma Kaskazini kuwa mafisadi wote ni wasafi?... Ina mana umesahau kuwa hata mabaniani walio wabaya lakini viatu vyao vinaweza kuwa dawa....

Katika hili Zitto ameonyesha ushujaa mkubwa sana wa kisiasa kwa kuthamini michango ya watu bila ya kujali tofauti zao za kimaadili..

Dilunga unatakiwa ku-call spade a spade siku zote..

Ulitaka awashukuru kina nani sasa kwa msaada wao?... Hivi Kigoma kuna majimbo mangapi ambayo hayana lami miaka nenda miaka rudi...

Ulipashwa umpongeze kwa nguvu zako zote na sio kushushia mzigo wa lawama.. Katika hilo zitto wewe ni shujaa na utaendelea kuwa shujaa... Chapa kazi watanzania wenzako tunakuunga mkono kwa ukarimu wako..

Dilunga unapashwa kufahamu kuwa mtu yeyote anapongezwa kwa mazuri yake na analaumiwa kwa mabaya yake...

Keep it up Zitto
 
Je, ilikuwa lazima kuwashukuru hao, hasa Chenge na Mrema? Jamani alama za nyakati zinasemaje?

Yes! it wa absolutely necessary, especially as a "Statesman" ni vizuri kukiri kuwa ulipata msaada hata kama siyo wakati mwafaka. Kwa sababu moja muhimu kuwa wakati wanafanya hivyo walikuwa wanatimiza wajibu wa kazi zao kitaifa, siyo kichama!
Ni sawasawa na akikubali kuwa anapohitaji msaada wa ulinzi wa Polisi anapewa na anashukuru sana.

Hapa ndipo mambo mengi huharibika sana wakati wabunge wanapoteuliwa kuwa mawaziri.
 
Mkuu hapo ndipo panapogomba ngoma kama Chenge ije ikupe madili kwamba kuna vijifisadi vinataka kukufisadi .teh teh teh teh
Hako ka mstari haujakaona nini?.

Nikwambie neno Fisadi RA kafanya mambo makubwa jimboni kwake kupita karibu wabunge wote.wenda naye anamfuko wakusaidia yatima wengi ,tumpe makofi RA kwa hilo kwakwa kwa kwa kwa!!!

Kule kwetu mwaibara hatupokei misaada ya masharati ndio maana wengi wanatuona kama wakorofi

Mwaibara ni wapi tena?!
 
Back
Top Bottom