Ningependa kujadili zaidi suala la Madaktari kufanya uamuzi wa kusitisha mgomo na kuamua kubaki kuendelea na huduma, la sivyo hawakubaliani na ridhaa ya seriakali, basi waondoke na kwenda huko wanaokofikiria watapata mafao yanayodai. Kwamba serikali imehusika katika kifo cha Dr. Stephen au la mimi sijui, na kinachoongelewa hapa ni tetesi zisizothibitishwa mpaka sasa.
Serikali ina idara nyingi na njia mbalimbali za kumaliza matatizo, ukianza kufatili utaumiza kichwa bure kwani hayo ni mipango migumu kuifumbua wakati waliopanga wana njia zote za kufifisha kiini cha ukweli. Cha kumshukuru Mungu waliomteka Dr. Stephen hawakumwua na imesaidia kupata ukweli fulani. Huenda hao watekaji wamekiuka kagizo la wakuu wao, mkinzano huo wanaujua wao na kwa sababu zao wenyewe. Ndio maana serikali ye yote duniani ina kitendo cha siri cha inteligensia, hakuna asiyejua hili. Tutalalamika hatimaye tutapoa. Kwa wenye uelewa hatupotezei muda kujadili hilo, na kama madaktari wangekuwa na uungwana na utu katika kudai haki zao na kupima kwa busara hayo pengine yasingetokea.
Kosa ambalo madaktari wamelifanya kuwekea rahani uhai wa wagonjwa ili kuishinikiza serikali jambo ambalo halikubaliki. Utaona hospitali za mashirika ya dini ndizo za kwanza kutekeleza uamuzi wa sirikali kuwafukuza madaktari walio kwenye mgomo kwa vile mashirika ya dini yanajali kwanza uhai wa binadamu na dhana nzima ya kuwajibikaji.
Kadiri ya Hotuba ya Rais, kiasi kikubwa cha madai ya madaktari yalishashatekelezwa, na sitegemea kwamba madai yote yangekubalika kwa vile mengine yako nje ya uwezo wa serikali. Kumbuka unaporatibu mishahara ni kitu cha kutumu kwa maisha, katu siku serikali haiwezi kupunguza kiwango cha mishahara ila kukipaisha. Kwa hiyo busara na uratibu wa kiuchumi katika idara ya utumishi na hazina ndio wenye kupima kiwango sahihi kinachoweza kulipwa kadiri ya uwezo wa serikali, hali ya uchumi wa nchi na uwezo wa idara ya utumishi kadiri ya uchumi wa nchi. Vinginevyo ni kudai bila kujua taratibu na sheria za ajira na uchumi wa nchi. Tukumbuke pesa nyinzi zinazoahidiwa toka kwenye bajeti ya serikali haziko hazina bali ni pesa hewa zinazotegemewa kutoka matarajio ya vyanzo mbalimbali, kwa maana hiyo malengo yanaweza kufikiwa au yasifikiwe.