Hotuba ya Nyerere kwenye mkutano wa wakuu wa nchi huru za Africa mwaka 1964. Nyerere alikuwa na bifu kali sana na Rais Kwame Nkrumah wa Ghana

Hotuba ya Nyerere kwenye mkutano wa wakuu wa nchi huru za Africa mwaka 1964. Nyerere alikuwa na bifu kali sana na Rais Kwame Nkrumah wa Ghana

Bwana Mwenye Kiti, nataka kuongeza neno langu moja kuunga mkono wale waliokwisha toa ombi hili, nami nafurahi kuona kwamba ombi hili lilitolewa na Rais wa Ghana, kwamba tufikirie kwa makini kabisa uwezekano wa kugawanya baadhi ya viwanda kwa kufuata hali ya Kontinenti letu, au, japokuwa kwa kufuata majimbo. Jambo hili litatuwezesha kujifaidia kwa biashara inayofanywa na watu millioni 250 wa Afrika, biashara ambayo sasa inawafaidia watu wengine; na hasa watu walio matajiri zaidi katika ulimwengu.

Mbona kama alikuwa ana mkubali Rais wa Ghana Kwame Nkrumah,
By then Africa nzima watu walikuwa milioni 250 tu, leo hii Nigeria pekee yake hapatoshi 😳 😎
 
Na mwisho, Bwana Mwenye Kiti, hebu niombe dua. Dua kwa sisi tuliokusanyika hapa; dua kwa watu wengi sana Waafrika wanao hangaika sana, wote tutumie nafasi tulizopata kwa uhuru wetu na ufundi wa kisasa, tujikomboe katika makombo ya ukoloni, na tuwainue watu wetu kwa kuwafungulia pingu za umasikini, ujinga na maradhi.

Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni Mwl JK Nyerere hakuwa mbinafsi saaaana😎
 
Bara La Afrika kuungana na kuwa nchi moja isingewezekana, haiwezekani, na haitokuja wezekana.

Miaka miwili baada ya hiyo hotuba, Waghana wakamtimulia mbali huyo aliyekuwa anaupigia chapuo huo muungano wa Afrika.

Mwaka uliofuata, Nigeria wakaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe.

Karibu kila kona ya Afrika hakukuwepo na amani.

Vinchi vidogo vidogo vyenye idadi ndogo ya watu vilishindwa kuelewana seuze bara zima kuungana na kuwa nchi moja?

Kuna nchi zinazidiana utajiri wa maliasili. Matunda ya mgawanyo wa hizo maliasili yangekuwaje?

Papo hapo nani angeunda hiyo serikali ya Afrika?

Kama Nkrumah tu Waghana wenzake walimchoka na kumtimua kutokana na udikteta wake, pata picha jinsi ambavyo Wanyarwanda wangemchukulia!

Rwanda tu hapo hata milioni 14 hawafiki lakini walichinjana wao kwa wao kutokana na kutoelewana.

Hiyo nchi moja ya Afrika ndo ingekuwa na amani, utulivu, na maendeleo gani?

Nyerere alikuwa sahihi na mpaka sasa bado yuko sahihi kwenye hilo, hata Kama baadaye alikuja kubadili mtazamo wake.

Afrika kuungana na kuwa nchi moja ni ndoto za Alinacha.
Kwanini haiwezekani kuungana? Kwanini Marekani, India, Urusi, China n.k. wameweza kuungana lakini Afrika isiwezekane?
 
Africa haiwez kuungana kamwe ni mawazo ya kipumbafu hayo.. angalia EAC community ilivyo ya kipumbafu imeshindwa kuwa kitu kimoja ndiyo africa ije iwe nchi 1?

Kwanini haiwezekani kuungana? Kwanini Marekani, India, Urusi, China n.k. wameweza kuungana lakini Afrika isiwezekane?
Unajua tofauti ya bara na nchi?

Afrika ni nchi au bara?

Marekani ni nchi au bara?

Kuna nchi inayoitwa Asia?

Kuna nchi inayoitwa Marekani ya kaskazini?

Unajua kuna mabara mangapi hapa duniani?

Unalinganisha matufaha na machungwa.

Afrika siyo nchi. Ni bara.

India na China ni nchi zilizopo bara la Asia.

Marekani ni nchi iliyopo bara la Marekani ya kaskazini.

Jiografia ya darasa la tatu hiyo.
 
Na kwa kumaliza mfululizo huu wote wa upuuzi; baada ya kuleta hoja hizi za ajabu kupinga umoja katika Afrika Mashariki sasa twaambiwa kwenye kinara hiki hiki tena kwamba wale walio tayari waungane. Ajabu, ati sasa twapewa ruhusa tuungane. Kwamba Umoja wa Nchi za Amerika ulianza na nchi kumi na tatu; Urusi ilianza na nchi tano. Kama ningalikuwa mtu wa kujali ningesema kuwa sisi wa Jamhuri ya Mwungano wa Tanganyika na Unguja tuko tayari; na tungaliiomba Ghana ijiunge na Jamhuri yetu ya Mwungano. Lakini mimi si mtu wa kujali. Najua ni vigumu ya kutosha kuleta mwungano katika Afrika Mashariki bali ya maneno maneno ya watu wa nchi za nje kuyaleta ili wazuie mwungano huo.
😳 😎
 
Unajua tofauti ya bara na nchi?

Afrika ni nchi au bara?

Marekani ni nchi au bara?

Kuna nchi inayoitwa Asia?

Kuna nchi inayoitwa Marekani ya kaskazini?

Unajua kuna mabara mangapi hapa duniani?

Unalinganisha matufaha na machungwa.

Afrika siyo nchi. Ni bara.

India na China ni nchi zilizopo bara la Asia.

Marekani ni nchi iliyopo bara la Marekani ya kaskazini.

Jiografia ya darasa la tatu hiyo.
Kumbe wewe ni mbumbumbu kiasi hicho!! Marekani ni muunganiko wa nchi (States) mbalimbali. Hata kwenye hiyo hotuba ya Mwalimu Nyerere ameeleza hivyo. Pia Urusi, China na India ikiwemo UK zimeungana na kuwa nchi moja kama tulivyoungana sisi Tanganyika na Zanzibar.
 
Kumbe wewe ni mbumbumbu kiasi hicho!! Marekani ni muunganiko wa nchi (States) mbalimbali. Hata kwenye hiyo hotuba ya Mwalimu Nyerere ameeleza hivyo. Pia Urusi, China na India ikiwemo UK zimeungana na kuwa nchi moja kama tulivyoungana sisi Tanganyika na Zanzibar.
States ni majimbo tu. Hata Tanzania ina mikoa.

Tanzania yenye mikoa ipo ndani ya bara la Afrika.

Nigeria nayo ina majimbo [states] kama Marekani. Nigeria ni nchi ndani ya bara la Afrika.

Marekani ina majimbo. Je, Marekani ni bara au ni nchi?

Kama Marekani ni nchi, ipo ndani ya bara gani?

Unalinganisha nchi na bara.

Au hujui tofauti ya nchi na bara?

Kuna mabara mangapi hapa duniani?
 
States ni majimbo tu. Hata Tanzania ina mikoa.

Tanzania yenye mikoa ipo ndani ya bara la Afrika.

Nigeria nayo ina majimbo [states] kama Marekani. Nigeria ni nchi ndani ya bara la Afrika.

Marekani ina majimbo. Je, Marekani ni bara au ni nchi?

Kama Marekani ni nchi, ipo ndani ya bara gani?

Unalinganisha nchi na bara.

Au hujui tofauti ya nchi na bara?

Kuna mabara mangapi hapa duniani?
Endelea kujielimisha hujui vitu vingi. Rudia kusoma tena hotuba ya Nyerere hapo juu labda utaelewa. Hayo Majimbo unayoyaita wewe yalikuwa nchi na kwa mujibu wa Nyerere Marekani ilianza na muungano wa nchi 13.
 
Endelea kujielimisha hujui vitu vingi. Rudia kusoma tena hotuba ya Nyerere hapo juu labda utaelewa. Hayo Majimbo unayoyaita wewe yalikuwa nchi na kwa mujibu wa Nyerere Marekani ilianza na muungano wa nchi 13.
Kuna tofauti kubwa sana kati ya vinchi vidogo vidogo vilivyopo ndani ya bara kuungana na kuunda nchi moja na bara zima lenye nchi kadhaa kuungana na kuunda nchi moja.

Ni sehemu gani hapa duniani ambapo bara moja liliungana na kutengeneza nchi moja?

Unajua hata bara ni nini wewe?
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya vinchi vidogo vidogo vilivyopo ndani ya bara kuungana na kuunda nchi moja na bara zima lenye nchi kadhaa kuungana na kuunda nchi moja.

Ni sehemu gani hapa duniani ambapo bara moja liliungana na kutengeneza nchi moja?

Unajua hata bara ni nini wewe?
Marekani ilipata uhuru ikiwa ni muungano wa nchi 13 kutoka kwa Waingereza mwaka 1776, baadae muungano umeongezeka na kuwa nchi 50 wewe unaita majimbo. Hayo majimbo yalikuwa na utawala wake. Hivyo usishangae siku moja Afrika ikaungana na kuwa Taifa moja kiutawala.
 
Marekani ilipata uhuru ikiwa ni muungano wa nchi 13 kutoka kwa Waingereza mwaka 1776, baadae muungano umeongezeka na kuwa nchi 50 wewe unaita majimbo. Hayo majimbo yalikuwa na utawala wake. Hivyo usishangae siku moja Afrika ikaungana na kuwa Taifa moja kiutawala.
Marekani iko bara gani?
 
mambo ya kuungana ungana haya nyerere aliyakumbatia sana anajifunza vitu kule ngambo halafu hafanya uchunguzi.mfano huu muungano huu mungano mpaka sasa sijaona faida yake zaid ya kuona wazanzibar wakija kupewa nyadhifa mbali huku afu watanganyika wakinyimwa kule
 
mambo ya kuungana ungana haya nyerere aliyakumbatia sana anajifunza vitu kule ngambo halafu hafanya uchunguzi.mfano huu muungano huu mungano mpaka sasa sijaona faida yake zaid ya kuona wazanzibar wakija kupewa nyadhifa mbali huku afu watanganyika wakinyimwa kule
Ni kweli. Wakati mwingine unaweza kuungana na mamba ilhali wewe u mjusi kama ilivyo mgongano wetu na zenj unaotufanya tunyonywe na upande mwingine
 
Back
Top Bottom