Hotuba ya dhihaka!

mzee wa inshu

Member
Jan 25, 2011
49
0
Kwa mara nyingine tena nitoe pole kwa watanzania wenzangu waliopatwa na janga la mlipuko wa mabomu hapo juzi. Namuopmba mwenynezi Mungu awape faraja kwa rehema zake!

Nirejeree kauli ya serikali iliyotolewa na mh rais usiku wa kuamkia leo juu ya msiba wa kitaifa uliosababishwa namlipuko wa mabomu kwenye kambi ya JWTZ maeneo ya gongo la mboto.

Nimwsikiliza sana hotuba hii na kwa makini, cha kusikitisha ni kuwa inaonyesha ni kwa kiasi gani ambavo raisi wetu hayuko makini ama bado anaendekeza mizaha katika mambo mazito yanayo gharimu uhai wa watanzania wenzake.

1.Nilitegemea angetangaza hatua kali kuchukuliwa kwa watu wote watakao bainika ama kwa makusudi au kwa uzembe kusababisha tukio hili.

2.Nilitegemea kutangaza kulipa fidia kwa majeruhi na ndugu wa marehemu na sio kifuta machozi kama alivo ahidi kwani hiyo ni lugha ya kisanii haiko wazi. kifuta j machozi inaweza kuwa hatt shiligi alufu moja(1000/=)

3.Sikutegemea raisi kumwaga sifa lukuki kwa uongozi wa JWTZ kwa wakati huu ilihali akifahamu fika kuwa uzembe nakiburi cha kufanya kazi kwa mazoea ndivyo sababu ya majanga haya.

Sikutegemea kuona mkuu wa majeshi na waziri wa ulinzi wanaendelea kukaa meza moja na mheshimiwa raisi mpaka muda huu. Wanaendelea vipi na kazi wasiyo iweza? Kiburi cha kutokujiudhuru wanakipata wapi? Kama hawataki kujiudhuru kwanini asiwatimue? je, wanafanya kazi kwa maslahi ya nani, wananchi au maslahi ya mtu binafsi?

4.Nilitegemea rais na Baraza iake la usalama la taifa wangekaa usiku huo huo wa tukio na kuamka asubuhi ya jana na mkakati mzito nasio kulala na wake zao huku wananchi wakiteseka kwa uzembe wao.

5.Rais anakumbuka leo kuomba msaada kutoka nchi rafiki juu ya namna bora ya kuhifadhi silaha na zana za kijeshi, hivi kumbe baada ya tukio la mabomu ya mbagala mlikuwa mnakunywa mvinyo bila ya kuchukua hatua yoyote ?

6. Anaomba imani ya wananchi kwa serikali yake na jeshi na kutoa ahadi ya kuto kutokea tena kwa tukio kama hili.
Je, ni mtanzania gani hivi leo ataamini ahadi hewa za vioongozi wasio aminika? Mheshimiwa unasahau kuwa wewe na mtoto wa mzee rukhsa mlisha wahi kutoa ahadi kama hizi wakati wa tukio la mbagala?

Je, inapotokea kuwa mmeshindwa kusimamia kile mlicho ahidi kwa wananchi, nini tena mnasubiri au mnataka wananchi wawafanye nini?

Mh Rais, wananchi wako tunakupenda sana ila aibu, upole, ukimya na kuwaonea haya watu wanao kuangusha na kuishi kwa gharama ya damu za watanzania wenzetu inatufanya na wewe tupatw na fikra za kukujengea chuki kama kikwazo kwetu.

Mh, hao wanajeshi ni watanzania wenzetu, kama wanavurunda wachukulie hatua mara moja bila woga wasa kusita kwani hizo silaha hawanunui kwa pesa yao ya mfukoni, ni kodi zetu sisi masikini tuliojinyima kununua madawa ya hosipitali na vitabu vya watoto wetu mashuleni.

TUNAJENGA NCHI KWA JASHO NA DAMU, WANAOBOMOA WASIACHIWE KAMWE''
 
mimi simpendi km una mpenda ni wewe usiwasemee wananchi eti sisi wananchi wako tunakupenda nani anampenda mtu anayevurunda kila kitu. na wewe acha kuuma na kupulizia keshachemka basi tena.
 
Damu waliyomwaga ni Kafara kwa taasisi ya Freemasons ambayo tunasikia 50% yao wanaabudu huko!

Kila kitu kilikuwa calculated jamani, ndio maana hamtakaa msikie mtu kuwajibishwa, ndiyo masharti ya Ibada za huko!
 
Mh Rais, wananchi wako tunakupenda sana ila aibu, upole, ukimya na kuwaonea haya watu wanao kuangusha na kuishi kwa gharama ya damu za watanzania wenzetu inatufanya na wewe tupatw na fikra za kukujengea chuki kama kikwazo kwetu.


Mkuu hapo kwenye nyekundu hatupo pamoja!!
 
Damu waliyomwaga ni Kafara kwa taasisi ya Freemasons ambayo tunasikia 50% yao wanaabudu huko!
Kila kitu kilikuwa calculated jamani, ndio maana hamtakaa msikie mtu kuwajibishwa, ndiyo masharti ya Ibada za huko!
Kwa hiyo JK ni member wa freemansons?
 
Nawapa pole wahanga wote waliothirika directly au indirectly.

Nashindwa kuelewa kabisa,ila hii nchi yetu ni ya ajabu..kama huwezi ku-act basi bora unyamaze,unachosema kinaumiza watu zaidi.

Kweli kuna sababu ya kulipongeza jeshi?hii inatoka kwa dhati kabisa moyoni mwake?-hata kama wasingepongezwa hivi kweli kabisa kuna mwanajeshi hata mmoja angelalamika kweli kwa kutopongezwa?

Kweli Mwenyezi Mungu ametuumbia watu, daah!
 
Kwa mara nyingine tena nitoe pole kwa watanzania wenzangu waliopatwa na janga la mlipuko wa mabomu hapo juzi. Namuopmba mwenynezi Mungu awape faraja kwa rehema zake!n

Nirejeree kauli ya serikali iliyotolewa na mh rais usiku wa kuamkia leo juu ya msiba wa kitaifa uliosababishwa namlipuko wa mabomu kwenye kambi ya JWTZ maeneo ya gongo la mboto.

Nimwsikiliza sana hotuba hii na kwa makini, cha kusikitisha ni kuwa inaonyesha ni kwa kiasi gani ambavo raisi wetu hayuko makini ama bado anaendekeza mizaha katika mambo mazito yanayo gharimu uhai wa watanzania wenzake.

1.Nilitegemea angetangaza hatua kali kuchukuliwa kwa watu wote watakao bainika ama kwa makusudi au kwa uzembe kusababisha tukio hili.

2.Nilitegemea kutangaza kulipa fidia kwa majeruhi na ndugu wa marehemu na sio
kifuta machozi kama alivo ahidi kwani hiyo ni lugha ya kisanii haiko wazi. kifuta j machozi inaweza kuwa hatt shiligi alufu moja(1000/=)

3.Sikutegemea raisi kumwaga sifa lukuki kwa uongozi wa JWTZ kwa wakati huu ilihali akifahamu fika kuwa uzembe nakiburi cha kufanya kazi kwa mazoea ndivyo sababu ya majanga haya.

Sikutegemea kuona mkuu wa majeshi na waziri wa ulinzi wanaendelea kukaa meza moja na mheshimiwa raisi mpaka muda huu. Wanaendelea vipi na kazi wasiyo iweza? Kiburi cha kutokujiudhuru wanakipata wapi? Kama hawataki kujiudhuru kwanini asiwatimue? je, wanafanya kazi kwa maslahi ya nani, wananchi au maslahi ya mtu binafsi?

4.Nilitegemea rais na Baraza iake la usalama la taifa wangekaa usiku huo huo wa tukio na kuamka asubuhi ya jana na mkakati mzito nasio kulala na wake zao huku wananchi wakiteseka kwa uzembe wao.

5.Rais anakumbuka leo kuomba msaada kutoka nchi rafiki juu ya namna bora ya kuhifadhi silaha na zana za kijeshi, hivi kumbe baada ya tukio la mabomu ya mbagala mlikuwa mnakunywa mvinyo bila ya kuchukua hatua yoyote ?

6. Anaomba imani ya wananchi kwa serikali yake na jeshi na kutoa ahadi ya kuto kutokea tena kwa tukio kama hili.
Je, ni mtanzania gani hivi leo ataamini ahadi hewa za vioongozi wasio aminika? Mheshimiwa unasahau kuwa wewe na mtoto wa mzee rukhsa mlisha wahi kutoa ahadi kama hizi wakati wa tukio la mbagala?

Je, inapotokea kuwa mmeshindwa kusimamia kile mlicho ahidi kwa wananchi, nini tena mnasubiri au mnataka wananchi wawafanye nini?


Mh Rais, wananchi wako tunakupenda sana ila aibu, upole, ukimya na kuwaonea haya watu wanao kuangusha na kuishi kwa gharama ya damu za watanzania wenzetu inatufanya na wewe tupatw na fikra za kukujengea chuki kama kikwazo kwetu.

Mh, hao wanajeshi ni watanzania wenzetu, kama wanavurunda wachukulie hatua mara moja bila woga wasa kusita kwani hizo silaha hawanunui kwa pesa yao ya mfukoni, ni kodi zetu sisi masikini tuliojinyima kununua madawa ya hosipitali na vitabu vya watoto wetu mashuleni.

''TUNAJENGA NCHI KWA JASHO NA DAMU, WANAOBOMOA WASIACHIWE KAMWE''



Muheshimiwa umeanza vizuri sana maana hata mimi ile hotuba yake imenikera sana sana sana.

Inaendelea kutuonyesha how shallow the president is, he can not be bold on serious issues like this, in short he is incompetent. Sasa hapo kwenye blue muzee ume-generalize.

Nakuhakikishia mimi simpendi hata kidogo, simpendi hata kumuona wala kusikia maneno yake. In fact i hate him with passion.
 
hawezi, tena hatawezi, na hatokuja kuweza kuwatimua hao mafirauni kwa maana hilo ndilo kundi lililoiba
kura pamoja so do we think it can be possible
 
Muheshimiwa umeanza vizuri sana maana hata mimi ile hotuba yake imenikera sana sana sana. Inaendelea kutuonyesha how shallow the president is, he can not be bold on serious issues like this........in short he is incompetent. Sasa hapo kwenye blue muzee ume-generalize. Nakuhakikishia mimi simpendi hata kidogo, simpendi hata kumuona wala kusikia maneno yake. In fact i hate him with passion.

Hata Mimi sikupendi JK lakini imeandikwa tuwaombee adui zetu, nitaendelea kukuombea uache upuuzi wako
 
Damu waliyomwaga ni Kafara kwa taasisi ya Freemasons ambayo tunasikia 50% yao wanaabudu huko!
Kila kitu kilikuwa calculated jamani, ndio maana hamtakaa msikie mtu kuwajibishwa, ndiyo masharti ya Ibada za huko!

Bwn PJ kwa kuongezea wandugu si mnakumbuka mnajimu mkuu nchi hii ya Wadanganyika Sheik Yahaya kipindi cha uchaguzi si alihaidi kumlinda Mh Raisi kwa majini?

Sasa huyo mkuu kwennye njego wa Magogoni aliwahi kuakanusha hiyo kauli ya kulindwa na majini?

Kama analindwa na majini je, yatafanya kazi bila sadaka?

Kwa hiyo majibu ya maswali tunayo majini yanakunywa damu ya watu, matambiko sadaka lazima zitolewe, haijalishi kivipi, kama tulikuwa hatujui funguka macho. Huo ni ulimwengu wa kiroho, mapepo yanavuna watoto na watu wa Tanzania!

Huyo Raisi wetu akanushe kulindwa na majini, aruhusu ibada za nguvu zifanyike kuondoa hayo majini Ikulu, KWA KIBALI CHAKE na yeye mwenyewe ashiriki, watu wa Mungu aliye hai wataomba na kufanya ibada huko Ikulu, kutimua hayo madudu yanayoleta mabaraa na maangamivu ya watu.

Na kwa jina la Bwn Yesu nakuhakikishia majini yataondoka na nchi itapona majanga ya ajabu!
 
Hata kama ubavu wa kuwatimua hana, kulikuwa na haja gani ya kuwasifia?? Maana mtu anasifiwa kwa kufanya jambo jema. kwa maana hiyo hawa JW kuacha mobomu yalipuke yenyewe na kuua watu ni jambo jema hadi kusifiwa na mkuu wa nchi, kwekli??
 
'' wananchi wakidai haki yao,risasi, mabomu ya machozi vinatumika dhidi yao na hata kuwajeruhi na kuwauwa''

ila ''wakubwa wakivurunda mambo na kusababisha hasara na vifo kwa wananchi wanapongezana kwa kugonga bilauri za mvinyo na bia''
 
Hata kama ubavu wa kuwatimua hana, kulikuwa na haja gani ya kuwasifia?? Maana mtu anasifiwa kwa kufanya jambo jema. kwa maana hiyo hawa JW kuacha mobomu yalipuke yenyewe na kuua watu ni jambo jema hadi kusifiwa na mkuu wa nchi, kwekli??
Ni jema kwa Kikwete na Serikali yake......
 
Moyo wangu hauamini kabisa kama mabomu haya yamelipuka bahati mbaya... Something fishy is going on!...
Ona sasa, tushasahau Dowans....waziri mkuu kudanganya bunge... Upepo wa
Nguvu ya uma...
 
''stand with any body who stands wright, stand with him while he is wright but part him when he goes wrong'
 
swala la kikwete kupendwa kupendwa na wananchi asahau labda hao mapopompo wenzake. Jk ni janga la kitaifa, pasua kichwa. alipofikia sasa panatosha unasifia wauaji wa raia!!! This is beyond the tolerable.
 
Back
Top Bottom