mzee wa inshu
Member
- Jan 25, 2011
- 49
- 0
Kwa mara nyingine tena nitoe pole kwa watanzania wenzangu waliopatwa na janga la mlipuko wa mabomu hapo juzi. Namuopmba mwenynezi Mungu awape faraja kwa rehema zake!
Nirejeree kauli ya serikali iliyotolewa na mh rais usiku wa kuamkia leo juu ya msiba wa kitaifa uliosababishwa namlipuko wa mabomu kwenye kambi ya JWTZ maeneo ya gongo la mboto.
Nimwsikiliza sana hotuba hii na kwa makini, cha kusikitisha ni kuwa inaonyesha ni kwa kiasi gani ambavo raisi wetu hayuko makini ama bado anaendekeza mizaha katika mambo mazito yanayo gharimu uhai wa watanzania wenzake.
1.Nilitegemea angetangaza hatua kali kuchukuliwa kwa watu wote watakao bainika ama kwa makusudi au kwa uzembe kusababisha tukio hili.
2.Nilitegemea kutangaza kulipa fidia kwa majeruhi na ndugu wa marehemu na sio kifuta machozi kama alivo ahidi kwani hiyo ni lugha ya kisanii haiko wazi. kifuta j machozi inaweza kuwa hatt shiligi alufu moja(1000/=)
3.Sikutegemea raisi kumwaga sifa lukuki kwa uongozi wa JWTZ kwa wakati huu ilihali akifahamu fika kuwa uzembe nakiburi cha kufanya kazi kwa mazoea ndivyo sababu ya majanga haya.
Sikutegemea kuona mkuu wa majeshi na waziri wa ulinzi wanaendelea kukaa meza moja na mheshimiwa raisi mpaka muda huu. Wanaendelea vipi na kazi wasiyo iweza? Kiburi cha kutokujiudhuru wanakipata wapi? Kama hawataki kujiudhuru kwanini asiwatimue? je, wanafanya kazi kwa maslahi ya nani, wananchi au maslahi ya mtu binafsi?
4.Nilitegemea rais na Baraza iake la usalama la taifa wangekaa usiku huo huo wa tukio na kuamka asubuhi ya jana na mkakati mzito nasio kulala na wake zao huku wananchi wakiteseka kwa uzembe wao.
5.Rais anakumbuka leo kuomba msaada kutoka nchi rafiki juu ya namna bora ya kuhifadhi silaha na zana za kijeshi, hivi kumbe baada ya tukio la mabomu ya mbagala mlikuwa mnakunywa mvinyo bila ya kuchukua hatua yoyote ?
6. Anaomba imani ya wananchi kwa serikali yake na jeshi na kutoa ahadi ya kuto kutokea tena kwa tukio kama hili.
Je, ni mtanzania gani hivi leo ataamini ahadi hewa za vioongozi wasio aminika? Mheshimiwa unasahau kuwa wewe na mtoto wa mzee rukhsa mlisha wahi kutoa ahadi kama hizi wakati wa tukio la mbagala?
Je, inapotokea kuwa mmeshindwa kusimamia kile mlicho ahidi kwa wananchi, nini tena mnasubiri au mnataka wananchi wawafanye nini?
Mh Rais, wananchi wako tunakupenda sana ila aibu, upole, ukimya na kuwaonea haya watu wanao kuangusha na kuishi kwa gharama ya damu za watanzania wenzetu inatufanya na wewe tupatw na fikra za kukujengea chuki kama kikwazo kwetu.
Mh, hao wanajeshi ni watanzania wenzetu, kama wanavurunda wachukulie hatua mara moja bila woga wasa kusita kwani hizo silaha hawanunui kwa pesa yao ya mfukoni, ni kodi zetu sisi masikini tuliojinyima kununua madawa ya hosipitali na vitabu vya watoto wetu mashuleni.
TUNAJENGA NCHI KWA JASHO NA DAMU, WANAOBOMOA WASIACHIWE KAMWE''
Nirejeree kauli ya serikali iliyotolewa na mh rais usiku wa kuamkia leo juu ya msiba wa kitaifa uliosababishwa namlipuko wa mabomu kwenye kambi ya JWTZ maeneo ya gongo la mboto.
Nimwsikiliza sana hotuba hii na kwa makini, cha kusikitisha ni kuwa inaonyesha ni kwa kiasi gani ambavo raisi wetu hayuko makini ama bado anaendekeza mizaha katika mambo mazito yanayo gharimu uhai wa watanzania wenzake.
1.Nilitegemea angetangaza hatua kali kuchukuliwa kwa watu wote watakao bainika ama kwa makusudi au kwa uzembe kusababisha tukio hili.
2.Nilitegemea kutangaza kulipa fidia kwa majeruhi na ndugu wa marehemu na sio kifuta machozi kama alivo ahidi kwani hiyo ni lugha ya kisanii haiko wazi. kifuta j machozi inaweza kuwa hatt shiligi alufu moja(1000/=)
3.Sikutegemea raisi kumwaga sifa lukuki kwa uongozi wa JWTZ kwa wakati huu ilihali akifahamu fika kuwa uzembe nakiburi cha kufanya kazi kwa mazoea ndivyo sababu ya majanga haya.
Sikutegemea kuona mkuu wa majeshi na waziri wa ulinzi wanaendelea kukaa meza moja na mheshimiwa raisi mpaka muda huu. Wanaendelea vipi na kazi wasiyo iweza? Kiburi cha kutokujiudhuru wanakipata wapi? Kama hawataki kujiudhuru kwanini asiwatimue? je, wanafanya kazi kwa maslahi ya nani, wananchi au maslahi ya mtu binafsi?
4.Nilitegemea rais na Baraza iake la usalama la taifa wangekaa usiku huo huo wa tukio na kuamka asubuhi ya jana na mkakati mzito nasio kulala na wake zao huku wananchi wakiteseka kwa uzembe wao.
5.Rais anakumbuka leo kuomba msaada kutoka nchi rafiki juu ya namna bora ya kuhifadhi silaha na zana za kijeshi, hivi kumbe baada ya tukio la mabomu ya mbagala mlikuwa mnakunywa mvinyo bila ya kuchukua hatua yoyote ?
6. Anaomba imani ya wananchi kwa serikali yake na jeshi na kutoa ahadi ya kuto kutokea tena kwa tukio kama hili.
Je, ni mtanzania gani hivi leo ataamini ahadi hewa za vioongozi wasio aminika? Mheshimiwa unasahau kuwa wewe na mtoto wa mzee rukhsa mlisha wahi kutoa ahadi kama hizi wakati wa tukio la mbagala?
Je, inapotokea kuwa mmeshindwa kusimamia kile mlicho ahidi kwa wananchi, nini tena mnasubiri au mnataka wananchi wawafanye nini?
Mh Rais, wananchi wako tunakupenda sana ila aibu, upole, ukimya na kuwaonea haya watu wanao kuangusha na kuishi kwa gharama ya damu za watanzania wenzetu inatufanya na wewe tupatw na fikra za kukujengea chuki kama kikwazo kwetu.
Mh, hao wanajeshi ni watanzania wenzetu, kama wanavurunda wachukulie hatua mara moja bila woga wasa kusita kwani hizo silaha hawanunui kwa pesa yao ya mfukoni, ni kodi zetu sisi masikini tuliojinyima kununua madawa ya hosipitali na vitabu vya watoto wetu mashuleni.
TUNAJENGA NCHI KWA JASHO NA DAMU, WANAOBOMOA WASIACHIWE KAMWE''