Hoteli / Lodge nzuri jijini Tanga

Hoteli / Lodge nzuri jijini Tanga

nenda mtaa wa chuda karibu na ofisi ya mkuu wa mkoa lodge nyingi sana
Huko vurugu sana mkuu ye anataka palipotulia mi tanga napajua vizur kuliko mzaliwa wa kule coz naenda nakaa mwezi na zaid narud au mwezi au wiki nazunguka tu
 
Tanga beach dola 75 tuu mkuu ukakutane na rangi za ughaibuni kama ni mtu wa high class na vitu visafi.
 
Nyinda classic ya raskazone ndo hua nafikia siku zote kumetulia sana na huduma zake nzur numerud last week tu nilikua huko
Kuna ile nyingine inaitwa Nyinda Tourist Hotel namba zao ni 0677 204 696. Tatizo hizo Nyinda nazo zipo nyingi nyingi hivyo kwa mtazamo wangu naona zinachanganya sana wageni. Kuna Nyinda Tourist hotel, Nyinda Respective hotel, Nyinda Executive 1 hotel, Nyinda Executive 2 hotel, Nyinda Classic hotel n.k. Yaani ni total confusion. Sehemu nyingine nilipowahi kupaona pametulia na bei yake ikiwa ni ya kawaida ni New Kwetu hotel. Baadae nikasikia pamepigwa mnada mwaka huu kutokana na mzozo wa kifamilia.

Kwa nyongeza tu pamoja na msaada utakaopata hapa si vibaya tukajenga mazoea ya kutumia apps kama Booking.com, TripAdvisor na HotelTonight kupata maelezo mengi ya hotel zilizopo huko unakotarajia kwenda mfano jina la hotel, picha ya hotel, mawasiliano yao, umbali kutoka katikati ya mji, bei na picha za vyumba, uwepo wa nafasi yaani chumba, mazingira ya ndani na nje ya hotel, comments za wateja wengine waliowahi kufikia hapo hotelini n.k.
 
Kwa bajeti hiyo sehemu kibao tu..ushindwe mwenyewe tu...Karibu Tanga mkuu.
 
Tanga mi naijua Mkonge hotel tu, basi.
Ngabu, mbona hivyo. Mkonge ni tourist hotel.. yeye ana 30,000-50,000 Tsh wakati mkonge ni over 100,000 Tsh. per night
Kuna Tanga beach Resort.. over 200,000 Tsh per night!
 
Huko vurugu sana mkuu ye anataka palipotulia mi tanga napajua vizur kuliko mzaliwa wa kule coz naenda nakaa mwezi na zaid narud au mwezi au wiki nazunguka tu
Et Unakaa mwezi tu unageuza then unapajua vizuri kuliko wazawa!kwan unatembeleaga sehem gan mkuu kwa huo mwezi mmoja ambazo wenyeji wa huku hawazijui
 
Wakuu nna shida kidogo naomba msaada. Nategemea kwenda Tanga wiki ijayo kwa shughuli binafsi. Naomba mwenye kujua hoteli au lodge nzuri ya kisasa ambayo naweza kufikia. Bajeti yangu ni 30,000 - 50,000 na napendelea sehemu tulivu, safi na yenye huduma nzuri. Kuna thread ipo humu ila ni ya zamani sana 2012 sasa mi napenda sehemu mpya mpya ndio zinakuwaga nzuri. Natanguliza shukrani
Tanga Beach resort
 
Nenda Macarious Hotel mtaa WA Chuda Good Cond.
Hii si iko nyuma kidogo ya Mtendele hotel? Tatizo hotel zingine ni za zamani na hazifanyi maboresho yoyote ili kwenda na wakati. Eti unakuta hotel bado ina TV za vichogo vyumbani!
 
Et Unakaa mwezi tu unageuza then unapajua vizuri kuliko wazawa!kwan unatembeleaga sehem gan mkuu kwa huo mwezi mmoja ambazo wenyeji wa huku hawazijui
Sijaanza kwenda juz au jana nimeanza kwenda tanga toka mwaka 2002 mkuu napajua vizur sana tena saana kuna kipindi nilikaa miezi minne nilikaa appatment kabisa raskazone kwa mzee mmoja anaitwa ally raskazone karibu kabisa na harbous club mkuu
 
Nenda waridi wapo PW, hawa wapo, chuda hukitoka nyinda, hunavuka hupande wa pili.
 
Wakuu nna shida kidogo naomba msaada. Nategemea kwenda Tanga wiki ijayo kwa shughuli binafsi. Naomba mwenye kujua hoteli au lodge nzuri ya kisasa ambayo naweza kufikia. Bajeti yangu ni 30,000 - 50,000 na napendelea sehemu tulivu, safi na yenye huduma nzuri. Kuna thread ipo humu ila ni ya zamani sana 2012 sasa mi napenda sehemu mpya mpya ndio zinakuwaga nzuri. Natanguliza shukrani
Karibu utapata,inabidi utembezwe utakaporidhia unachukua room
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom