Hongereni STRABAG! Dar Rapid Transit imefana mno!

Si user friendly kwa mtu anaekwenda kwenye mitaa ya pembeni kwani mingi haina inlet na outlet. Inabidi ugeuzie mbali sana.
Kweli kazi nzuri sana kwa miji ya kisasa
Kasoro ndogo tu ni kwamba Sio rafiki kwa walemavu wavuka njia.
Fuatilia Kipindi alichorusha Zembwela Jpili iliyopita sehem za kuvukia hasa kwa walemavu ndio utapata jibu.
 

Ni kweli, inabidi vipato viongezeke ili kumudu gharama za kusafiri jijini. Barabara ya kawawa ikikamilika, mtu anayetoka buguruni kwenda kawe/masaki atapanda Mara tatu hadi kufika mwisho wa safari. Mwenge kwenda kimara atabadili mara mbili, mwenge-sinza kwenda k.koo atabadili mara tatu...nahisi haya vipato inabidi viongezeke...
 
ndio itakuwa slogan ya kampeni za uraisi na wabunge 2015, hiyo na daraja la kigamboni, mie naona tatizo la foleni bado halijatatuliwa, hiyo barabara ilitakiwa itanuliwe at least iwe na 6 lanes kila upande, sasa lanes 2 -2 unategemea foleni zitashuka, hell no,
 

unakata tiketi moja tu mahali unapoanzia safari mpaka mwisho wake.....pia unaweza kukata tiketi ya siku/wiki/mwezi/mwaka kulingana na mahitaji yako....kwa mfano uko buguruni unaenda masaki unakata tiketi ya buguruni masaki single/return ambayo utatumia kwenye mabasi yote yatakayihusika na connection zako....sehemu ambazo hizo barabara za dart hazifiki wataweka mabasi yao ndio yatakuwa yanaleta watu hadi barabara kubwa za dart....ila nauli itakuwa juu kidogo sio 400/= kwa route.......kizuri gharama.
 
Kazi nzuri, ila naona kasoro kwenye bus stops walizoziweka, naona ziko nyingi na karibu sana, mfano kutoka Kimara mpaka Fire kuna vituo vingi sana, na sehemu kubwa wamechukua vitu vile vile vya zamani. Sasa hapo maana ya mabasi ya mwendo kasi naona haitakuwepo sana.
 
Are you serious? Kwa hiyo kutakuwa na mabasi yanauounganisha njia za Dart? Lets say mtu anatoka sinza-kariakoo, anakuwa na junctions tatu..sinza-sheki, sheki-fire(dart)then fire-kariakoo...huyu ananunua ticket ticket moja tu? Then itapinguza kidogo mzigo wa nauli kuongezeka. Japo nina wasiwasi mabasi ya dart nje ya njia zake yatakuwa machache sana..anyway, tusubiri tuone...!
 

thats how it works...unaona kile kituo cha shekilango rd ni kwa ajili ya feeder buses from shekilango road...ukipita magomeni moroko hotel kipo ile njia inayotoka kwa mtogole kwa ajili ya feeder buses from kwa mtogole....ukija kinondoni nyuma ya puma petrol station kipo kwa ajili ya feeder buses kutoka m'nyamala..pale magomeni butiama hotel kipo kwa ajili ya feeder buses kutoka kigogo hivyo ndivyo itakavyokuwa na feeder buses ni kubwa kama yale ya mbagala moja washalifanyia majaribio watu wakafikiri ndio mabasi yao.

fire-kariakoo-kamata dart main inapita kwahio yale makubwa yatafika huko,connection ndio hizo kama unatokea sinza unakuja shekilango....mwenge/kawe unakuja hadi moroko...mwananyamala unakuja hadi nyuma ya puma pale mwanamboka etc
 

Kiongozi, nimekupata kwa uzuri kabisa. Hata sikufikiria vile vituo ni kwa ajili ya feeder buses, Jana nikawa naongea na mke wangu akasema ati aliyaona hayo mabasi...kama ya mbagala, nadhani ndo hayo walikuwa wanafanuia test...na yeye kafikiri ndo mabasi yatayotumika na dart..lakini nilibisha coz mie nafaham sample yake..sio kama ya mbagala...
Thanx kwa ufafanuzi!!
 

Si kwamba hayo mabasi yatakwenda kwa kasi hapana, lengo ni kwamba yatakua hayasimami kwenye foleni kama magari mengine na unaweza panga safari yako toka kimara hadi fire, utakua unajua kua utafika hapo firw mda gani
 
Si kwamba hayo mabasi yatakwenda kwa kasi hapana, lengo ni kwamba yatakua hayasimami kwenye foleni kama magari mengine na unaweza panga safari yako toka kimara hadi fire, utakua unajua kua utafika hapo firw mda gani

hiyo ndio maana yake. ni kama uamue kuruhusu daladala ipite kwenye njia ya bus (zege) toka Kimara hadi Posta hata kama itasimama kila kituo bado itaokoa muda mwingi sana kwa kuwa haitakaa foleni sehemu yoyote!
 

Hash ! Vipato vitaongezeka sababu tutaonana muda...
 
Wanaoongopaga foleni kubwa kumbe wapo gesti wataanza kuumbuka.
 

Mimi nawalaumu designers wa barabara na siyo mjenzi. Ningemlaumu mjenzi kama mradi ungekuwa ni Design and Build ambapo mjenzi anakuwa ni designer mwenyewe. Barabara ya magari ya kawaida imefinywa kiasi kwamba huwezi kulipita gari lililo mbele yako. Kwenye kona ndo usiseme,barabara ni nyembamba sana! Jambo lingine ni uwepo wa curves( kona) ambazo zimewekwa nyingi bila sababu!
 
Yatasimama sana kwenye mataa ,labda yawekewe fly-overs.
 


Bongo tambarare.
 
Mkuu umenichekesha sana hapo uliposema kutembea ni changamoto dah, kwa kusema kweli kuna nchi nyingi watu utembea kwenda kwenye vituo vya mabasi (hasa kwenye miji mikubwa mfano london) kuna baadhi ya sehemu kupata usafiri wa umma inaghalimu kutembea dakika kadhaa, maana sio kila mahali utakuta kuna usafiri wa route yake au hakuna kabisa usafiri wa umma kwa umbali furani, nadhani hii itasaidia kuimalisha afya za wana Dar es-salaam , yaani utakuta mtu mnazi mmoja amekaa nusu saa nzima anasubiria gari la kwenda post au mtu yuko post anasubiria gari ya mnazi mmoja au karikoo .
tunatakiwa kubadilisha mitazamo yetu, mifumo bora ya usafiri ni pamoja na kutembea au kutumia biskeli na sio mabus yafutuate mpaka miguuni au sebereni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…