Hongera waseminari mliomaliza mtihani

Hongera waseminari mliomaliza mtihani

bonem

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2015
Posts
235
Reaction score
55
Kwa taarifa tu ni kwamba waseminari zaidi ya ishirini wamefanya mtihani wa kuongea (oral examination) leo katika seminari kuu ya mt Paulo, Kipalapala. Wamehitimisha mtihani wa baccalaureate waliouanza siku ya Jumanne.

Kwa hatua hii wanahitimisha maandalizi yao kitaaluma kuelekea upadri. Ndugu mafrate, kwa niaba ya taifa lote la Mungu hapa JamiiForums nawatakia kila jema katika kujiandaa kupokea majukumu haya matakatifu ya upadri.

Ndugu wanajukwa tuwaunge mkono vijana hawa katika maamuzi yao ya kishujaa kuwa mapadri.

Ni mimi padri mtarajiwa
 
Ebu nielimishe mkuu,mpaka uwe padri unaanzia hatua gani?
 
Kwa taarifa tu ni kwamba waseminari zaidi ya ishirini wamefanya mtihani wa kuongea (oral examination) leo katika seminari kuu ya mt Paulo, Kipalapala. Wamehitimisha mtihani wa baccalaureate waliouanza siku ya Jumanne.

Kwa hatua hii wanahitimisha maandalizi yao kitaaluma kuelekea upadri. Ndugu mafrate, kwa niaba ya taifa lote la Mungu hapa JamiiForums nawatakia kila jema katika kujiandaa kupokea majukumu haya matakatifu ya upadri.

Ndugu wanajukwa tuwaunge mkono vijana hawa katika maamuzi yao ya kishujaa kuwa mapadri.

Ni mimi padri mtarajiwa

Umenikumbusha mbali ndugu yangu, mie nilifukuzwa nikiwa mwaka wa kichungaji parokia moja ya jimbo la musoma, sitokaa nimsahau marehemu askofu justine samba kwa aliyonitendea. :msela:
 
Umenikumbusha mbali ndugu yangu, mie nilifukuzwa nikiwa mwaka wa kichungaji parokia moja ya jimbo la musoma, sitokaa nimsahau marehemu askofu justine samba kwa aliyonitendea. :msela:

Ulikuwa Makoko mkuu mwaka gani?
 
Mleta mada naomba ku-declare kwamba mm ni m-kristo ila naomba kujua ni kwa nini Ma-Padri hamuoi!? (Only that).
 
Umenikumbusha mbali ndugu yangu, mie nilifukuzwa nikiwa mwaka wa kichungaji parokia moja ya jimbo la musoma, sitokaa nimsahau marehemu askofu justine samba kwa aliyonitendea. :msela:

ulipitia seminary gani?? kipalapala au segerea. this vocation has no guarantee or security whatsoever. naamini umeweza kupambana kuwa mkristu mwema huko uliko. unajishughulisha na nini kwa sasa???
 
ulipitia seminary gani?? kipalapala au segerea. this vocation has no guarantee or security whatsoever. naamini umeweza kupambana kuwa mkristu mwema huko uliko. unajishughulisha na nini kwa sasa???

Nilifukuzwa pastoral year, nikatoka nikaenda UDSM kufanya LLB kwa sasa wenzangu ni mapadri na kwa darasa letu tuna askofu mmoja. ( marafiki zangu Fr, werema(marehemu), Fr. Manyonyi, Fr. Bilingi, Nk)
 
Duh...nimekumbuka mbali sana,anyway ni mipango ya Mungu niwe hivi nilivyo,Hongereni sana mafrateri kwa hatua hiyo
 
Mbona Baccalaureate maana yake ni mtihani wa sekondari, inakuwaje hapa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom