Hongera Taifa Stars!

Hongera Taifa Stars!

Katika hali ya kushangaza na kusikitisha, vyombo vyetu vya habari hasa television vimeshindwa kuwaonyesha watanzania mechi ya mpira wa miguu kati ya timu yetu ya Taifa (Taifa Stars) iliyokuwa ikicheza dhidi ya Moroco.

Wakati vituo vya binafsi vikiendelea kurusha vipindi vyao vya kawaida, Television ya Taifa (TBC) wao walijikita uwanja wa ndege wa Julius Nyerere kurusha matangazo ya moja kwa moja juu ya ujio wa raisi wa China.

Hivi kweli watanzania tumefika mahali pa kuwathamini wageni kuliko timu yetu ya Taifa? Naamini watanzania walioko Tarime, Tandahimba, Kakonko, Pemba, Namanyele ama Tunduru wangetamani kuishuhudia timu yao ya Taifa kuliko raisi wa China asiye na maslahi yoyote na maisha yao.

Ni dhahiri kuwa viongozi wetu wa sasa wameishiwa kabisa na uzalendo, na ndio maana wanaendelea kufanya mambo ya kijinga huku wananchi wakiwakodolea macho bila kuchukua hatua.

Tuwe na shukrani jamani, umeshasahau hata huo uwanja wa mpira wamejenga kwa ufundi na pesa yao (baada ya Mkapa kutembeza bakuli:A S shade🙂...Huyu ataondoka na hatarudi kwa mda mrefu, wakati mechi zinachezwa kila wiki...Tuache kulalamika kwa kila jambo.
 
Ni sawa na mama mjamzito unamwambia hongera wakati bado hajajifungua?
Unampa hongera kwa kushika mimba na kuikubali maana wengi wanatoa angali changa. Na akijifungua unampa hongera kwa kupata mtoto!
 
Tuwe na shukrani jamani, umeshasahau hata huo uwanja wa mpira wamejenga kwa ufundi na pesa yao (baada ya Mkapa kutembeza bakuli:A S shade🙂...Huyu ataondoka na hatarudi kwa mda mrefu, wakati mechi zinachezwa kila wiki...Tuache kulalamika kwa kila jambo.


F***k!!! shukrani ya uwanja wa mpira ambao kodi za wamachinga tu wa mtaa wa kongo wanajenga?

Bora Mwl Nyerere walimjengea reli!!
 
Haa haa haa. Katika watu wenye ubishi wa kijinga duniani Watanzania wanaongoza. Kweli unaweza kutamba timu ya taifa ina kiwango?

Haina kiwango ila imeonesha kiwango. Ni kweli watanzania wana ubishi wa kijinga ndiyo maana unaendelea kubisha!
 
Vijana wametupa faraja kubwa wametusahaulisha japo kwa muda siasa za maji taka,tutafika tu
 
Ndoto za mwendawazimu. Watu wa sampuli yako ndie mnafanya tusisonge mbele kwenye mpira. Mkibahatisha kamechi kamoja mnapiga kelele utafikiri mna vichaa. Wewe kwa kuangalia mchezo wanaocheza timu ya taifa unaweza kweli kufurahia na kujitapa eti hongera. Kesho maumuvi yanakurudia halafu unasikia eti tunajiuliza tumefikaje hapa jamani... kumbe ubishi usio na msingi

Mkuu hii ni mechi ya tatu tunashinda tena ngumu, tumewafunga Zambia wakiwa mabingwa wa Africa, Cameroon timu ngumu sana, na sasa Morocco tena goli tatu bado unabeza. Unataka tumfunge nani ndio tuwape pongezi
 
Tuwe na shukrani jamani, umeshasahau hata huo uwanja wa mpira wamejenga kwa ufundi na pesa yao (baada ya Mkapa kutembeza bakuli:A S shade🙂...Huyu ataondoka na hatarudi kwa mda mrefu, wakati mechi zinachezwa kila wiki...Tuache kulalamika kwa kila jambo.

Wewe hata hujijui unachoandika.

China haikutupatia msaada wa ujenzi wa uwanja wa taifa bali tulikopa na hata sasa bado tunalipa deni.

Pili utambue kwamba hatuna nafasi ya kuwaona wachezaji wetu wakicheza na morocco katika michuano ya world cup 2014.

Tatu watanzania hawana shida ya kuona live ujio wa raisi wa china taarifa za habari saa 2 usiku ni habari tosha.

Ushauri wako wa kutaka tuache kulalamika ni wa kipuuzi na inaonyesha jinsi gani watu mlivyotindikiwa uzalendo na kuwa na ufinyu wa kujua maslahi ya taifa dhidi ya maslahi ya watu wachache.
 
Katika hali ya kushangaza na kusikitisha, vyombo vyetu vya habari hasa television vimeshindwa kuwaonyesha watanzania mechi ya mpira wa miguu kati ya timu yetu ya Taifa (Taifa Stars) iliyokuwa ikicheza dhidi ya Moroco.

Wakati vituo vya binafsi vikiendelea kurusha vipindi vyao vya kawaida, Television ya Taifa (TBC) wao walijikita uwanja wa ndege wa Julius Nyerere kurusha matangazo ya moja kwa moja juu ya ujio wa raisi wa China.

Hivi kweli watanzania tumefika mahali pa kuwathamini wageni kuliko timu yetu ya Taifa? Naamini watanzania walioko Tarime, Tandahimba, Kakonko, Pemba, Namanyele ama Tunduru wangetamani kuishuhudia timu yao ya Taifa kuliko raisi wa China asiye na maslahi yoyote na maisha yao.

Ni dhahiri kuwa viongozi wetu wa sasa wameishiwa kabisa na uzalendo, na ndio maana wanaendelea kufanya mambo ya kijinga huku wananchi wakiwakodolea macho bila kuchukua hatua.
Kwa hili muraa nakuunga mkono.
Kama hawajaonyesha hii mechi live ni kukosa uzalendo.
Lazima tuwe proud na nchi yetu, ina maana walikosekana wadhamini kabisa?
 
Na TBC je?badala ya kutuonyesha mpira wa taifa star wakakata nakutuonyesha rais wa china,imeniudhi sana maana mchina kaja kupora tu,tulitaka tuiangalie timu yetu na sisi tulioko huku mikoani.kweli uzalendo kazi....
 
Kwa hili muraa nakuunga mkono.
Kama hawajaonyesha hii mechi live ni kukosa uzalendo.
Lazima tuwe proud na nchi yetu, ina maana walikosekana wadhamini kabisa?

Taifa stars inao udhamini mnono wa Kilimanjaro Premium Lager ambao wasingeshindwa kudhamini matangazo ya mechi ya leo kwakuwa mechi zilizotangulia wamekuwa wakizidhamini na kuonyeshwa live kwa watanzania.

Ni lazima tuwe proud na vitu vyetu wenyewe. Ni fedheha kumpa kipaumbele mchina kuliko timu yetu ya Taifa.
 
Hongera sana Taifa Stars...yani kuna watu wanashangaza sanaaaaaa tukishinda wanaponda tukifungwa wanafurahi halafu wanajiita wanamapinduzi...nilikuwa naangalia BBC Sports mtangazaji wa BBC timu pekee aliyoisifia ni Tanzania sio tu kwa ushindi wa leo bali na kwa iliyopita
 
Unawapongeza kwani wamefuzu? Hili ndo jambo linalowafanya wa tz kuonekana waajabu! Kazi kupongeza hata kitu ambacho hakijatekelezwa..
Acheni ushamba wa kijinga

Ww ni mtu wa ajabu sana ndg yangu yaani unawaona wenzio ni watu wa ajabu kwa kupongeza ushindi wa stars,labda ni kukosekana kwa uzalendo ndiko kunakosababisha uchukie stars kupongezwa,kaka mm nilikuwepo uwanjani nikishuhudia kazi waliyofanya wachezaji wetu.
Hakika nikwambie kwa kipindi cha miaka mitano nyuma cjawahi ona aina ya soka lililopigwa taifa leo,leo tumeona soka la spain.
Viva Taifa Stars,
Viva Kim Paulsen.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Wakati mwingine watu wenginge wanashangaza sana, sasa huyo Bangoo alitaka watu walie? Mbona wakifungwa huwa 'wanalaumiwa' hata kama ni gemu moja au mbili? Kwa sababu watu wanachotaka ni ushindi..haijalishi watafuzu au la. Je, ukiwa na mtoto akifaulu darasa la kwanza, utamnunulia zawadi ya kumpongeza au utasubiri afaulu darasa la saba?

Ni vizuri kujifunza kupongeza..timu inapofanya vizuri!
 
Back
Top Bottom