Hongera Taifa Stars!

Hongera Taifa Stars!

Huwezi kufuzu bila kushinda, na kushinda ni hatua muhimu kuelekea kufuzu. Hivyo ni muhimu kujipongeza katika kila hatua.
Ni sawa na mama mjamzito unamwambia hongera wakati bado hajajifungua?
 
kichwa cha mwendawazimu kimebahatisha wala hatuna kiwango cha kwenda cheza brazil tuwaache tu kina chamack marudiano tutakunya hata 5 kwao

Kiwango kipo ndiyo maana walidhibitiwa barabara mpaka wakashindiliwa hizo tatu!
 
Unawapongeza kwani wamefuzu?
Hili ndo jambo linalowafanya wa tz kuonekana waajabu! Kazi kupongeza
hata kitu ambacho hakijatekelezwa..
Acheni ushamba wa kijinga

Hivi unajua maana ya neno USHAMBA mi naona we ndo mshamba
 
Unawapongeza kwani wamefuzu? Hili ndo jambo linalowafanya wa tz kuonekana waajabu! Kazi kupongeza hata kitu ambacho hakijatekelezwa..
Acheni ushamba wa kijinga
acha hila wanapofanya vizuri lazima wapewe sifa labda wewe simtanzania ndo mtu pekee unayebeza timu yako ya taifa wakati imefanya vizuri!
 
Unawapongeza kwani wamefuzu? Hili ndo jambo linalowafanya wa tz kuonekana waajabu! Kazi kupongeza hata kitu ambacho hakijatekelezwa..
Acheni ushamba wa kijinga
Kuwa muungwana, unadhani timu itafuzu bila kushinda? wakifungwa maneno wakishinda watu wengine roho zinawauma. Daah Tz MUNGU atusaidie.
 
Unawapongeza kwani wamefuzu? Hili ndo jambo linalowafanya wa tz kuonekana waajabu! Kazi kupongeza hata kitu ambacho hakijatekelezwa..
Acheni ushamba wa kijinga
Hivi nyie mamburura mna akilki kweli?
Kwa hiyo kwa sababu bwanaako DJ kasema muandamane basi hata kwenye threads za kuleta faraja mnaingiza ujinga wenu
NG'OMBE KASORO MKIA
 
Kwa mtu kama wewe Hata wakifuzu Utasema Hawaja chukua kombe.
Hata wakichukua Kombe utasema ndio mara ya kwanza.
Hata wakichukua mara ya pili utasema. Hawajacjhukua mara Tatu.

Kifupi watu kama nyie mpo na mtaendelea kuwepo.
Pole sana!

Ndoto za mwendawazimu. Watu wa sampuli yako ndie mnafanya tusisonge mbele kwenye mpira. Mkibahatisha kamechi kamoja mnapiga kelele utafikiri mna vichaa. Wewe kwa kuangalia mchezo wanaocheza timu ya taifa unaweza kweli kufurahia na kujitapa eti hongera. Kesho maumuvi yanakurudia halafu unasikia eti tunajiuliza tumefikaje hapa jamani... kumbe ubishi usio na msingi
 
Hakika Hawa Watu Lazima Wawepo Ili Dunia Iendelee Kuzunguka Mhimili Wake......HONGERA TAIFA STARS.....WE R PROUD OF YOU!
 
Najua hili ni jukwaa la siasa lakini hatuna budi kuipongeza taifa stars kwa ushindi ilioupata dhidi ya timu ya taifa ya moroco.
Tukumbuke angalau huu ndo upande unaotuunganisha watanzania kwa pamoja hivi sasa na ni habari njema tumepiga hatua moja mbele. tuwape moyo vijana wetu tuondoe sihasa huku zisije zikaharibu kila kitu.


MUNGU IBARIKI TANZANIA
Mkubwa tunaomba utujuze ngap[i ngapi na tunaingiwa raundi ipi
 
Kiwango kipo ndiyo maana walidhibitiwa barabara mpaka wakashindiliwa hizo tatu!

Haa haa haa. Katika watu wenye ubishi wa kijinga duniani Watanzania wanaongoza. Kweli unaweza kutamba timu ya taifa ina kiwango?
 
Pamoja na pongezi ila kamati ya ufundi imezidisha mvua maana nasikia tabata kuna mafuriko....
 
sasa tuna point sita naomba mnikumbushe matokeo ya mechi ya kwanza tuliifunga timu gani na goli ngapi
 
wewe ndio una akili
hebu tuletee threads ya kusifia mabwana zako wa matamko na maandamano

Basi. Nimesarenda. Nisamahe. Kuanzia sasa nasema ''Timu ya taifa ni nzuri inacheza kwa kiwango cha hali ya juu sana. Itachukua kombe la dunia mwaka ujao.''
 
Back
Top Bottom