Hongera Jerry Muro. Sasa tuambie hili!

Hongera Jerry Muro. Sasa tuambie hili!

Kazi ya uandishi wa habari ni ngumu kuliko mnavyofikiria. Jerry na waandishi wengine wazuri hawatakiwi kumiliki pingu tu, bali ni vizuri watembee daima na mkasi, bisibisi (screw drivers), wembe, pamoja na vifaa vingine vinavyofanana na hivyo. Mwandishi si busara na vizuri kumiliki na kutembea na bastola. Hivyo vingine huwa vinamsaada ambao nitaweza kuwaelekeza mkini PM.

Mwandishi anatakiwa kuandika UKWELI. Katika mazingira ya kawaida, ukitaka kuishi maisha marefu USIWE MKWELI. Ukichunguza sana, wengi (wenye dhambi) wanaishi maisha marefu na kinachowasaidia sana ni [woga, umbea, fitna, majungu na unafiki, huwa wanatoa shikamoo nyingi sana hata pasipohitajika].

Si rahisi wala vizuri kwa jerry muro kueleza sababu za kutembea na pingu, japokuwa kama matumizi yake ni mabaya atakuwa anakusea. Kuna namna anaweza kuitumia pingu vizuri kama mwandishi atakapolazimika. Kama maoni yangu unadhani ni utani, jaribu kuwa mkweli sana katika naafisi yako ya maisha.
 
Siyo swali langu lakini kwa hakika hii haijawahi kusikika popote. Jamaa alikuwa akitumia pingu kutapelia halafu watu wanamchekea. Tuache kuchekelea mmomonyoko wa maadili na waandishi wanaoamini katika blackmail.

mie nina pingu, lakini sijawahi kutishia mtu wala sijawahi kuchekewa na mtu yoyote na wala sijawahi kutapeli, naitumia kwenye satisfactions zangu nyumbani,

unaamini kila mwenye pingu anfanya uliyoandika?
 
kwani ni kosa kumiliki hivyo vitu yaani pingu na bastola na kama ni kosa kwanini duka la silaha pale upanga wanaviuza?

hata mie mashangaa.... pingu ina kazi za kutosha tu kama ukiwa mbunifu, na kumiliki bastola si ujambazi, inategemea matumizi
 
mie nina pingu, lakini sijawahi kutishia mtu wala sijawahi kuchekewa na mtu yoyote na wala sijawahi kutapeli, naitumia kwenye satisfactions zangu nyumbani,

unaamini kila mwenye pingu anfanya uliyoandika?
Mate, watu hawajui kuwa pingu ni kifaa murua sana kwenye mapenzi.....
 
Hahahaah...babu hapa unaua! Ushaanza uchakachuzi wa hii sredi!
Kwangu mie naona bastola ni hatari zaidi ya pingu. Sasa kama bastola inauzwa inakuwaje pingu zisiuzwe? Mabomu yangekuwa yanauzwa ningeogopa lakini pingu? khaa! watu wanafungana pingu wakati wanamegana kwa raha zao bana!
 
Kwangu mie naona bastola ni hatari zaidi ya pingu. Sasa kama bastola inauzwa inakuwaje pingu zisiuzwe? Mabomu yangekuwa yanauzwa ningeogopa lakini pingu? khaa! watu wanafungana pingu wakati wanamegana kwa raha zao bana!
afadhali hata hayo mabomu kamanda........ utu unauzwa siku hizi, tena kwa bei ya chee!!! we angalia wanasiasa wanavyonunuliwa kwa bei ya baiskeli ya swala

we cheki aishababu walivyoingia procuerment contract na serikali/polisi kuamua ni mikutano gani washambulie na ipi wasishambie wala kutoa tishio

BTW, NAUZA PINGU MPYA KABISA KUTOKA PAKISTANI, BRABD ANAYOTUMIA BILL CLINTON KWA PLEASURE ZAKE
 
Ni vema basi tuelimishwe tusiojua, kwani wanaouza pingu madukani wateja waliokusudiwa kuuziwa hizo pingu hasa ni watu gani?
 
Mnachoshangaa Jerry kumililiki pingu na bastola ni nini?au mleta thread hii ni mwathirika wa vipindi alivyowahi kuvirusha Jerry na vikawaumbua?tujiulize kidogo kwa makini,hizi pingu zinauzwa kisheria au si kisheria na kama ni kisheria sheria hiyo iliwekwa na Muro?na kama si kisheria kwa nini mahakama imeamua arudishiwe pingu zake?

Na kama haziuzwi kisheria hao wanaoziuza kwa nini hawachukuliwi hatua?wewe kama hupendi kumiliki pingu usioanishe dislike zako na za Muro kisha ukataka humu jamnvini ushawishi watu kujengea wasiwasi Muro.Juu ya hukumu yake ya rushwa sina cha kujadili maadam mahakama imeshatoa hukumu, lakini hoja ya pingu na bastola ni ufinyu wa fikra kulazimisha kusa wakati zinauzwa kwa kila anaehitaji ili mradi tu atimize matakwa ya kuuziwa.

Leo Muro kama anapenda kumiliki pingu ni hiari yake na mwingine anapenda kula kitimoto ni hiari yake anaependa kugonga castle bariki ruksa leo tukianza kuulizana eti tuambie unapokunywa bia ni za nini,tutakuwa tunaingilia uhuru binasfi,na Jerry kwa kuwa pingu zinauzwa kisheria na alizinunua kisheria hiyo sasa inatosha.

Na hata hivyo kama mtu anaandika habari za kiuchunguzi kwa mtazamo wangu ni mtu ambaye anatazamiwa kukutana na changamoto nyingi katika utendaji wake. Sasa kama lizinunua kwa ajili ya kujihami sioni ajabu maana mbona huwa tunawafunga kamba wahalifu kisha tunawapeleka vituoni,japo kuna wakati mwingine raia wanajichukulia sheria mkononi kwa kuwachoma moto.hatujawahi kushuhudia watu wakiwafunga kamba wahalifu?
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Mnachoshangaa Jerry kumililiki pingu na bastola ni nini?au mleta thread hii ni mwathirika wa vipindi alivyowahi kuvirusha Jerry na vikawaumbua?tujiulize kidogo kwa makini,hizi pingu zinauzwa kisheria au si kisheria na kama ni kisheria sheria hiyo iliwekwa na Muro?na kama si kisheria kwa nini mahakama imeamua arudishiwe pingu zake?

Na kama haziuzwi kisheria hao wanaoziuza kwa nini hawachukuliwi hatua?wewe kama hupendi kumiliki pingu usioanishe dislike zako na za Muro kisha ukataka humu jamnvini ushawishi watu kujengea wasiwasi Muro.Juu ya hukumu yake ya rushwa sina cha kujadili maadam mahakama imeshatoa hukumu, lakini hoja ya pingu na bastola ni ufinyu wa fikra kulazimisha kusa wakati zinauzwa kwa kila anaehitaji ili mradi tu atimize matakwa ya kuuziwa.

Leo Muro kama anapenda kumiliki pingu ni hiari yake na mwingine anapenda kula kitimoto ni hiari yake anaependa kugonga castle bariki ruksa leo tukianza kuulizana eti tuambie unapokunywa bia ni za nini,tutakuwa tunaingilia uhuru binasfi,na Jerry kwa kuwa pingu zinauzwa kisheria na alizinunua kisheria hiyo sasa inatosha.

Na hata hivyo kama mtu anaandika habari za kiuchunguzi kwa mtazamo wangu ni mtu ambaye anatazamiwa kukutana na changamoto nyingi katika utendaji wake. Sasa kama lizinunua kwa ajili ya kujihami sioni ajabu maana mbona huwa tunawafunga kamba wahalifu kisha tunawapeleka vituoni,japo kuna wakati mwingine raia wanajichukulia sheria mkononi kwa kuwachoma moto.hatujawahi kushuhudia watu wakiwafunga kamba wahalifu?

Unalinganisha bia na pingu? We kweli kiboko.
 
Wengine hatumtetei Jerry bali tunapinga mfumo mzima uliotumika kumshtaki na kumhukumu Jerry ndani na nje ya vyombo vya haki.Wewe kama una uyajuayo kuhusu Crime buster Jerry, mwaga humu usafishe wanaotuhumu Polisi kwa kumfanyizia.Vinginevyo lawama zitaendelea tu.Tunazidi kukosa imani na askari siku hadi siku.Imefkia mahala mtu akiona askari anashtuka na kukimbia kama vile kakutana na jambazi.Hii ni mbaya sana

Tausi nimekupata.. Kama na wewe umenisoma vizuri ni kwamba binafsi siamini kuwa Jeri alisingiziwa
wala alibambikiwa kesi na Polisi bali baada ya kunyoshea kidole waovu wenzie walijiambia tu kwamba mbona hii issue ni simple tu..... wakamfuata kwenye njia yake (yeye muro) na wakampata kwakuwa ni mwenzao.... though papara zikategua mtego ambao ulikuwa haujanasa vizuri, na udhaifu huo pamoja pamoja na rushwa vikamtoa kwenye hatia. I hope i have made myself very clear!
 
Kwa maoni yangu mimi siyo suala la kipi ni hatari kuliko kingine. Suala hapa ni nini motive ya mwandishi wa habari kumiliki pingu? Ukiona hilo ni la kawaida, kuna siku tutamkuta na sare za moja kati ya majeshi yetu ya ulinzi na usalama. Mbona kumiliki filimbi haijawahi kuwa issue ya ajabu? Ukiona watu wanashangaa ujue this is uncommon!

kama siyo hatari kwa nini unakiogopa?
 
Kweli vilaza wapo wengi
Wewe kama ungekuwa na nia ya kutaka kujua ungeenda mahakamani kusikiliza hukumu ama upatiwe nakala ya hukumu.Hapo ingekuwa rahisi kujua kuwa pingu ilikuwa ni ya kwake na alikuwa nayo kwa matumizi gani.
Eti na wewe ni Great thinker....!
Kwanza nikupongeze Jerry Muro kwa kushinda kesi yako dhidi ya Jamhuri, na baadae kujipatia tuzo ya ubora wa kazi zako na kile kilichoitwa ujasiri wako katika kufichua maovu yaliyopo ndani ya jamii.

Sasa baada ya habari hizi njema, ni wakati muafaka sasa kuueleza umma wa watanzania matumizi ya zile pingu ulizokiri kuzimiliki na hata kutuonyesha stakabadhi ya manunuzi ya pingu hizo. Tunakuomba ufanye hivyo kwa sababu wewe Jerry Muro sasa umeingia kwenye rekodi za dunia kama mwandishi pekee wa habari duniani mwenye kumiliki kifaa ambacho ni vyombo vya ulinzi na usalama pekee ndiyo wana mamlaka ya kumiliki na matumizi. Au unataka kutuambia kwamba kazi zako za uandishi zinahitaji kujihami na wakati mwingine ku-effect arresting powers za wahalifu mbalimbali? Je, mamlaka hii umeipata wapi wakati hata Polisi waliostahili kukukasimu wamekukana na kukuchukulia hatua?

Bila majibu fasaha, sitashangaa siku nyingine nikisikia unamiliki mahakama (lakini siyo hii iliyokuachia huru katika mazingira ya utata) na hata magereza na vituo vyako vya polisi.

Muro please, come out clean!
 
Jerry Muro si investigative journalist wa kwanza nchini na duniani lakini hatujawahi kusikia hiki kituko popote pale. Kuwa investigative journalist si kuwa na vitu ambavyo katika hali ya kawaida watu hawatakiwi kuwa navyo. In this case bwana huyu alikuwa tayari ame-solicit rushwa akijiita ni mwanausalama. Tuwekewe bayana hili siyo kuishi kwa "ifs".
Kwamba aliomba rushwa nadhani hayo ni mawazo yako tu. mahakama, baada ya kuisikiliza kesi hii imemuona Jerry na wenzaake kuwa hawana hatia ya kosa lolote waliloshitakiwa nalo, likiwamo hilo la kuomba rushwa.
Pia kumbuka kuwa investigative reporter hafanyi kazi zake in a cionventional journalism way, ni lazima kuwe na mambo mengine ya ziada ambayo yanaweza kujumuisha impersonation pia wakati mtu anatafuta taarifa nyeti.
KUna wakati JF ilipokuwa ikiitwa jamboForum tulikuw tunatupiwa nondo kali sana humu, rejea thread hizo (maana bado zipo) halafu waulize waliozileta walipataje hizo docs walizokuwa wanazishusha na utaelewa namaanisha nini
 
Jerry Muro sasa umeingia kwenye rekodi za dunia kama mwandishi pekee wa habari duniani mwenye kumiliki kifaa ambacho ni vyombo vya ulinzi na usalama pekee ndiyo wana mamlaka ya kumiliki na matumizi.
Ulifanikiwa kuwakagua waandishi wote waliokuwa wakiripoti habari za vurugu huko Afrika ya Libya, hasa wa vyombo vya CNN, BBC, Al Jazeera, nadhalika ili kudhibitisha rekodi hii ya Mr. Muro?
 
Ulifanikiwa kuwakagua waandishi wote waliokuwa wakiripoti habari za vurugu huko Afrika ya Libya, hasa wa vyombo vya CNN, BBC, Al Jazeera, nadhalika ili kudhibitisha rekodi hii ya Mr. Muro?

Mpaka sasa hivi wale wote aliotoa utetezi kuhusu Jerry, hawajatueleza with precision madhumuni ya zile pingu za Jerry. Hicho mnachoita sex pleasure na uppuzi mwingine ni namna ya kudogodesha hoja hii ambayo inazua maswali mengi kuliko majibu kuhusu usafi wa mwandishi huyu ambaye kabla ya hapo alikuwa amejizolea sifa lukuki kamwa mtoboa siri.

Nadhani mnamzungumzia huyu huyu Jerry Muro ambaye huwa namkuta pale Mango Garden akiwa na wenzake wakipanga michongo ya namna ya kutapeli watu. Muro awe na ujasiri wa kutueleza alichotarajia kufanya na pingu hizo katika kazi yake ya uandishi. Asituache tukafanya speculation juu ya alichokusudia kufanya na hizo pingu.

Mimi nadhani hatujadili uhalali wa manunuzi ya pingu hizo au kwa nini zinauzwa kwenye maduka ya silaha. Jerry atueleze mahusiano ya pingu na kazi zake za uandishi. Kama alipanga kuzitumia kwa ngono kama baadhi ya watetezi wake mnavyodai, basi atujulishe hilo bila utata ili tujue hakukuwa na uhusiano kati ya kazi zake na hizo pingu.
 
Back
Top Bottom