Hongera Jerry Muro. Sasa tuambie hili!

Hongera Jerry Muro. Sasa tuambie hili!

banyimwa

Senior Member
Joined
Mar 1, 2011
Posts
116
Reaction score
25
Kwanza nikupongeze Jerry Muro kwa kushinda kesi yako dhidi ya Jamhuri, na baadae kujipatia tuzo ya ubora wa kazi zako na kile kilichoitwa ujasiri wako katika kufichua maovu yaliyopo ndani ya jamii.

Sasa baada ya habari hizi njema, ni wakati muafaka sasa kuueleza umma wa watanzania matumizi ya zile pingu ulizokiri kuzimiliki na hata kutuonyesha stakabadhi ya manunuzi ya pingu hizo. Tunakuomba ufanye hivyo kwa sababu wewe Jerry Muro sasa umeingia kwenye rekodi za dunia kama mwandishi pekee wa habari duniani mwenye kumiliki kifaa ambacho ni vyombo vya ulinzi na usalama pekee ndiyo wana mamlaka ya kumiliki na matumizi. Au unataka kutuambia kwamba kazi zako za uandishi zinahitaji kujihami na wakati mwingine ku-effect arresting powers za wahalifu mbalimbali? Je, mamlaka hii umeipata wapi wakati hata Polisi waliostahili kukukasimu wamekukana na kukuchukulia hatua?

Bila majibu fasaha, sitashangaa siku nyingine nikisikia unamiliki mahakama (lakini siyo hii iliyokuachia huru katika mazingira ya utata) na hata magereza na vituo vyako vya polisi.

Muro please, come out clean!
 
Muro anajua alivyoshinda ile kesi halafu leo anajifanya kumwaga chozi la furaha kwa kitu alichokitarajia. Wenye akili wanajua mpaka kiasi alichopewa Hakimu ili kununua uhuru wako. Fadhila hizi zimefanywa na mafisadi ambao wewe unawatumikia na sasa wanakuandalia mipango ya kurudi TBC na hilo likishindikana unapelekwa kwenye moja ya mitandao ya habari za mafisadi kufanya kazi.
 
Ajabu wametoa amri arudishiwe Bastola na Pingu zake!!Kweli this is Tanzania where i live!
 
Kwanza nikupongeze Jerry Muro kwa kushinda kesi yako dhidi ya Jamhuri, na baadae kujipatia tuzo ya ubora wa kazi zako na kile kilichoitwa ujasiri wako katika kufichua maovu yaliyopo ndani ya jamii.

Sasa baada ya habari hizi njema, ni wakati muafaka sasa kuueleza umma wa watanzania matumizi ya zile pingu ulizokiri kuzimiliki na hata kutuonyesha stakabadhi ya manunuzi ya pingu hizo.
Tunakuomba ufanye hivyo kwa sababu wewe Jerry Muro sasa umeingia kwenye rekodi za dunia kama mwandishi pekee wa habari duniani mwenye kumiliki kifaa ambacho ni vyombo vya ulinzi na usalama pekee ndiyo wana mamlaka ya kumiliki na matumizi. Au unataka kutuambia kwamba kazi zako za uandishi zinahitaji kujihami na wakati mwingine ku-effect arresting powers za wahalifu mbalimbali? Je, mamlaka hii umeipata wapi wakati hata Polisi waliostahili kukukasimu wamekukana na kukuchukulia hatua?

Bila majibu fasaha, sitashangaa siku nyingine nikisikia unamiliki mahakama (lakini siyo hii iliyokuachia huru katika mazingira ya utata) na hata magereza na vituo vyako vya polisi.

Muro please, come out clean!

umeshachunguza waandishi wote dunia nzima?
 
Kwanza nikupongeze Jerry Muro kwa kushinda kesi yako dhidi ya Jamhuri, na baadae kujipatia tuzo ya ubora wa kazi zako na kile kilichoitwa ujasiri wako katika kufichua maovu yaliyopo ndani ya jamii.

Sasa baada ya habari hizi njema, ni wakati muafaka sasa kuueleza umma wa watanzania matumizi ya zile pingu ulizokiri kuzimiliki na hata kutuonyesha stakabadhi ya manunuzi ya pingu hizo. Tunakuomba ufanye hivyo kwa sababu wewe Jerry Muro sasa umeingia kwenye rekodi za dunia kama mwandishi pekee wa habari duniani mwenye kumiliki kifaa ambacho ni vyombo vya ulinzi na usalama pekee ndiyo wana mamlaka ya kumiliki na matumizi. Au unataka kutuambia kwamba kazi zako za uandishi zinahitaji kujihami na wakati mwingine ku-effect arresting powers za wahalifu mbalimbali? Je, mamlaka hii umeipata wapi wakati hata Polisi waliostahili kukukasimu wamekukana na kukuchukulia hatua?

Bila majibu fasaha, sitashangaa siku nyingine nikisikia unamiliki mahakama (lakini siyo hii iliyokuachia huru katika mazingira ya utata) na hata magereza na vituo vyako vya polisi.

Muro please, come out clean!

Jamaa nilikuwa namheshimu sana kwa habari zake moto moto lakini baada ya tukio hili, integrity yake nimeitilia mashaka makubwa sana. Hivi hizi pingu bado zinauzwa kwa raia? Nadhani nahitaji nakala moja.
 
Kweli kabisa hata mimi najisikia kujua kwa nini amiliki pingu au bastola huku yeye ni mwandishi.Pia mazingira ya kuachiwa kwake bado yananipa shaka sana pamoja na kujifanya eti amewasamehe waliomsababishia,is it possible kuwasamehe kirahisi hivi au ndo mambo ya JAIRO ili hoja isiendelee na kugundua yaliyojificha?Binadamu tumeumbwa na hasira na kulipa kisasi ni sehemu ya character ya binadamu ndo maana mahakamani waliweka malipo kwa ajili ya mtu kuchafuliwa jina
 
umeshachunguza waandishi wote dunia nzima?

Siyo swali langu lakini kwa hakika hii haijawahi kusikika popote. Jamaa alikuwa akitumia pingu kutapelia halafu watu wanamchekea. Tuache kuchekelea mmomonyoko wa maadili na waandishi wanaoamini katika blackmail.
 
hivi pingu au bastola/bunduki/sime/mkuki kipi ni hatari zaidi , sioni tofauti ya pingu na kamba nene iayoweza kumfunga mtu kama pingu ilivyo

kipi kiuzwe na kipi kisiuzwe?
 
Muro anajua alivyoshinda ile kesi halafu leo anajifanya kumwaga chozi la furaha kwa kitu alichokitarajia. Wenye akili wanajua mpaka kiasi alichopewa Hakimu ili kununua uhuru wako. Fadhila hizi zimefanywa na mafisadi ambao wewe unawatumikia na sasa wanakuandalia mipango ya kurudi TBC na hilo likishindikana unapelekwa kwenye moja ya mitandao ya habari za mafisadi kufanya kazi.

Kama una uhakika na Habari Hizi tafadhali BE OPEN;
 
hivi pingu au bastola/bunduki/sime/mkuki kipi ni hatari zaidi , sioni tofauti ya pingu na kamba nene iayoweza kumfunga mtu kama pingu ilivyo

kipi kiuzwe na kipi kisiuzwe?
Mkuu hupo!!!ahaaaaaaaaaaaaaaa!
 
Mkuu hupo!!!ahaaaaaaaaaaaaaaa!

Kwa maoni yangu mimi siyo suala la kipi ni hatari kuliko kingine. Suala hapa ni nini motive ya mwandishi wa habari kumiliki pingu? Ukiona hilo ni la kawaida, kuna siku tutamkuta na sare za moja kati ya majeshi yetu ya ulinzi na usalama. Mbona kumiliki filimbi haijawahi kuwa issue ya ajabu? Ukiona watu wanashangaa ujue this is uncommon!
 
Jamaa nilikuwa namheshimu sana kwa habari zake moto moto lakini baada ya tukio hili, integrity yake nimeitilia mashaka makubwa sana. Hivi hizi pingu bado zinauzwa kwa raia? Nadhani nahitaji nakala moja.

Nakala ya nini?
Pingu utapenda kupata "jozi" moja siyo nakala moja.
 
Pale mwanzo tuliaminishwa kwamba hivi vilikuwa ni visasi vya Kova na askari wake kwa kile kilichoitwa kuumbuliwa kwao katika kipindi cha usiku wa habari. Sasa leo kila mtu hapati mantiki ya mwandishi kuji-equip na pingu (labda na zana zingine za kijeshi ambazo hazijagunduliwa). Kijana huyu ame-ruin carrier yake ambayo ilioneka kuwa na very nright future. Labda atakuwa muungwana kutuambia zaidi ili apate tuzo nyingine bora zaidi kwa kitendo chake hiki.
 
Nyie askari wapelelezi na waendesha mashtaka, si mkate rufaa kuliko kuja kulalama hapa?
Siku nyngine mfanye kazi zenu safi/vizuri maana mmezidi kuzembea kazi.Acheni kusumbua wananchi,
hasa nyie askari wa barabarani.Kama Jerry alitoa kitu kidogo, katika nchi ya kitu kidogo na watu wake wadogo, kuna la ajabu lipi ikiwa nanyi mnavutaga kitu kidogo?Au kesi hii mliogopa kuvuta?Huwa mnashangaza sana.Kitu kidogo nyie huwa mnaongoza na hizo mahakama sasa msituletee hapa.
 
Nyie askari wapelelezi na waendesha mashtaka, si mkate rufaa kuliko kuja kulalama hapa?
Siku nyngine mfanye kazi zenu safi/vizuri maana mmezidi kuzembea kazi.Acheni kusumbua wananchi,
hasa nyie askari wa barabarani.Kama Jerry alitoa kitu kidogo, katika nchi ya kitu kidogo na watu wake wadogo, kuna la ajabu lipi ikiwa nanyi mnavutaga kitu kidogo?Au kesi hii mliogopa kuvuta?Huwa mnashangaza sana.Kitu kidogo nyie huwa mnaongoza na hizo mahakama sasa msituletee hapa.

Sasa hapa unaharibu sifa yako ya uzalendo. Hii jozi ya pingu tujulishwe ilikuwa na kazi gani bana!
 
Back
Top Bottom