Mkuu ukweli ni kwamba hakuna shamba la serikali Tz hii kwa sasa lina uhakika wa kuwepo kwa HF pure breed. Kuna ranchi moja ipo Kagera, zamani ilikuwa na pure breeds lakini hata yenyewe sasa inaaminika imeshachakachua. Kitulo pia waliopo sio pure breed, japokuwa kwa kiasi fulani wanakaribia.
Kwa maoni yangu ni kuwa ufugaji wa ng'ombe sio kitu cha kuanza leo na kuona mafanikio kesho. kwa hiyo kama ni ng'ombe wanaotoa maziwa kwa wingi, then ni bora mtu ukjitahidi kuwazalisha mwenyewe kwa kufanya selection na planned breeding. Kwa maana hiyo, ni bora mtu ukanunua tu ngombe (chotara may be) kwenye shamba ambalo lina historia ya kuwa na ng'ombe wanaotoa maziwa mengi (hata karibu na Dar siku hizi yapo), then ukaenda kufanya breeding kwa kupandikiza kwa chupa, hadi ukapata line ya ng'ombe wanaotosheleza malengo yako...
ASAS Iringa wanaweza kuwa nao, tatizo ni namna ya kupata bahati ya kumpata japo mmoja. Kilolo kulikuwa na shamba la mitamba la serikali, sijui kama bado lipo au ndio kama kawa.