HOJA MBADALA: Tuhamasishe CCM imsimamishe Membe 2015?

HOJA MBADALA: Tuhamasishe CCM imsimamishe Membe 2015?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,095
Reaction score
43,305
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho.

Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"

CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.

Ni kweli?
 
Mkuu Mwanakijiji,Subiri kashfa ya pesa za Libya ndio utawajua vizuri wanasiasa wetu wana sura gani ni mapema mno kumjadili huyu nyoka wa mdimu.Ni bora mchawi Lowasa tumkabidhi mwana.
 
Naona itawasaidia sana cdm kushinda! Hizi enzi si tu mtu anabebwa na chama kama ilivyokuwa kwa Mkapa "95, bali pia mtu nae anakibeba chama kama Dr Slaa "10! Membe doesnt fit in any how!
 
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"

CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.

Ni kweli?
si kweli,,,,,maana sisiem hapo ilipo inatumia rafu tu kukaa madarakan ila hata wenyewe wamechoka
 
Kama nimekusoma vizuri Mzee Mwanakijiji umesema "Anaweza kushinda" mimi nadhaini yeye ndiye angalau hajachafuka sana kama hao wengine so anaweza kuleta upinzani!! Ingawaje kwakweli magamba wasahau 2015
 
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"

CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.

Ni kweli?

kwa sisi watu wa intelejensia tunafahamu fika kuwa wewe mwana kijiji ni mpambe wa karibu wa membe, hapa jukwaani umekuja kupima upepo wa huyo rafiki kipenzi chako, kwa taarifa yako ni heri mara mia ya lowasa kuwa rais kuliko an hypocrite in born character benny membe. Naomba umwambie rafiki yako pengine mtaonana US leo au kesho kuwa mmekwama na mipango yenu tunaifahamu tunasubiri muda tu tuwalipue.
 
Membe amekosa uthubutu katika uongozi wake.Tanzania ya sasa inahitaji kiongozi jasiri katika kukabiliana na maamuzi na changamoto mbalimbali ziilizopo.Aina ya watu kama Membe ni wa kupokea maagizo tu na kutumwa siku zote.
 
Kaka mara hii umeishakachuliwa hadi kuwa kuwadi wa mafisadi kama si nepi yao?

Huyo Membe amekupa nini hadi umzimie na kumuabudia hivyo ndugu yangu? Kweli adui yako muombee njaa na penye udhia penyeza rupia. Yaani mihemko yako yote ya miaka yote umeishia hapo? Kwanini siku hizi watu wanashabikia uchanguuu hadi kwenye mawazo yarabi?

Heri ungenyamaza kuliko kuvua nguo mtoni usijue kuna watu. Heri kuamini kwenye unachohubiri hata watu wakakucheka kuliko kuramba matapishi yako. Pole sana bwana mdogo. Je huduma yako unauza bei gani?
 
Mzee Mwanakijiji,

Sintopendekeza mtu isipokuwa kwa manufaa ya taifa na japokuwa Membe ni kichwa, muweza ukiachana na habari za Ufisadi wake maana huko CCM hakuna msafi kihivyo. Wayahudi walilaaniwa tena na Mungu mwenyewe lakini bado wanaitawala dunia.

Hivyo pamoja na utetezi wako bado nakuhakikishia kwamba CCM wataweza tu kushindana ikiwa watamsimamisha Asha Rose Migiro na hii itatokana na WANAWAKE kutumia kauli mbiu ya TUKIWEZESHWA TUNAWEZA. Itakuwa sio swala la chama bali wanawake against the rest...Na amini maneno yangu watu hawatatazama tena nyuma wala kutazama uwezo wa AshaRose isipokuwa ni mageuzi ambayo kwao yatawalemaza akili..

Kwa upande wa ushindani na hasa Chadema wanatakiwa kuanza mapema sana kumtafuta na kumwandaa mgombea japo kwa siri lakini nawatahadharisha mapema - KAZI IPO 2015 wajipange mapema na vizuri sana laa sivyo itakuwa aibu maana elimu ya Uraia haijazama vichwani mwa wananchi hivyo SHIDA na MATATIZO yanatangulia Mapenzi yao..
 
Mtazamo wangu juu ya Mh. Membe kama chaguo la ccm kwa nafasi ya Urais-2015 nilishautoa hapa toka 27th December 2011 13:56:


Katika orodha ya wanaotajwa kuwania uteuzi wa ccm kwa nafasi ya urais wa JMT-2015, namba mbili (2) katika nisio shawishika nao ni Mh. Bernard Membe. Mh. Membe hanishawishi kuwa anastahili nafasi hiyo kwa sababu zifuatazo:


  1. 1. Historia halisi ya utendaji wake kama Mbunge na Waziri haina matokeo yanayosimama kumshuhudia Mh.Membe kama mtu wa kuleta mabadiliko chanya au maendeleo.

Asiyeweza katika dogo, ataweza katika makubwa? Mbele ya wapigakura wa Jimbo la Mtama, Mh. Membe anaonekana kama mtu aliyeshindwa kutimiza ahadi zake za muhula wa kwanza (2005-2010). Na walio wengi hawaoni umuhimu/mchango wa ukaribu wake na serikali katika kuwaletea mabadiliko. Ndo maana Mh. Membe alipata wakati mgumu sana kutoka kwa mgombea wa TLP, mtu ambaye hakuwa na jina, mali wala pesa bali support ya wananchi. Lakini kwa kutumia utaalamu aliojaaliwa, Mh. Membe aliweza "kumshughulikia" na kumdhibiti mpinzani huyu pekee na kuhakikisha wapiga kura wanakosa chaguo mbadala wakati wa uchaguzi. Ninashawishika kufikiri kuwa hata mpinzani mmoja angepenya na kusimama, matokeo ya Jimbo la Mtama yangekuwa sawa na ya Nyamagana.

Kuna jambo moja ambalo Mh. Membe ameshiriki na watu wasio na kumbukumbu nzuri au wafupi katika kuchambua mambo wanaweza kusema kalifanikisha. Ni suala la kurejeshwa kwa fedha za rada kupitia serikali badala ya NGOs kama wezi walivyotaka. Hii haiwezi kuhesabika kama jitihada ya Mh. Membe wala serikali ya Tanzania. Hili silielezi kwa ufasaha ili watu wajadili……………………..


  1. 2. Misingi ya mbinu anazotumia Mh. Membe katika kusaka kuungwa mkono na makundi yenye ushawishi mkubwa katika jamii haina maslahi kwa Taifa na inatengeneza viporo vya uporaji wa rasilimali za nchi na migogoro mikubwa ya kijamii hapo baadae.
Mathalani, katika suala la serikali kuanzisha na kuendesha Mahakama ya Kadhi na serikali ya JMT kujiunga na OIC, Mh. Membe akiwa mbele ya waandishi wa habari amekuwa akiwaondoa hofu wahusika kuwa haya mambo hayana shida na serikali iko katika hatua mbalimbali za kuyatekeleza. Mara tu upande wa pili wakianza kupaza sauti za kupinga, Mh. Membe hu-haha na hukimbia kimya kimya kwenda kwa viongozi wakuu wa upande wa pili "kutuliza mambo" kwa kificho. Katika hili, Mh. Membe anataka kuuma na kupuliza na ni ndumila kuwili. Ni vema, si kwa Mh. Membe tu, bali wanasiasa wote kuimarisha msingi wa msimamo ambao umekwishafikiwa na serikali katika suala hili nyeti.

Mh. Membe anasimama miongoni mwa viongozi wa Bara la Afrika waliosimama kidete kuomboleza kifo cha Shujaa wetu Mummar Gadaff. Lakini nyuma ya kilio na maombolezo ya msiba huu, kumefunikwa giza totoro la vitendawili juu ya nini haswa "majonzi" ya Mh. Membe? Wako wanaotoa nuru ili kutegua vitendawili kwa hadithi tofauti tofauti ambazo kwa ujumla wake ukizikusanya kwa ushambuzi makini unapata picha pana juu ya makubaliano/fadhila za utawala uliongushwa Libya kwa mgombea mtarajiwa. Watanzania tunapaswa kuwa tumejifunza madhara ya wagombea wetu kufadhiliwa na matajiri (nchi au mtu binafsi). Tutumie 2015 kuepuka kurudi chini ya utawala wa waliofadhili wagombea katika chaguzi kuu.

Mh. Membe anapigania uraia wa nchi mbili. Kwa faida ya nani? Binafsi sioni kama hili jambo lina tija kwa Taifa lenye uchumi unaomilikiwa na asilimia mbili (2%) ya wananchi wake na ndio asilimia tisini na nane (98%) ya hao hao tayari wana uraia wa nchi zaidi ya mbili. Hapa Mh. Membe hasimami kutetea rasilimali watu za Watanzania walioko nje bali kutafuta kuongeza wigo wa kuungwa mkono na watu wasiokuwa na uchungu wa nchi hii. Hawa tunaowaita "Watanzania wenye asilia ya Kihindi" ambao ndo wanashawishi sana suala hili tayari wanao uraia Uswizi, Canada, Marekani na hapa kwetu kutokana na udhaifu wa idara zetu za uhamiaji wanaishi na kufanya wanalotaka kwa jeuri ya pesa yao.

Nahitaji kushawishiwa kwa historia na utendaji upi Mh. Membe anastahili kuomba ridhaa ya kubeba bendera ya ccm katika uchaguzi mkuu 2015. Michango yenu ikiwemo matusi na dhihaka vinakaribishwa. Na kuwa na hakika, nitavipokea vyote kama vilivyo. Kwa namna ya pekee nausubiri mchango wa MBOPO, mtu ambaye mara nyingi hujitahidi kujibu hoja na si kujadili mtoa hoja katika kumtetea Mh. Membe.


Nawatakia Mwaka Mpya Mwema na Wenye Mafanikio.

Omutwale kutoka Kanyigo.
 
Wala haifanani na issue ya Zitto.
Dah! yaani mtu unakuwa hater hata nikiambiwa wewe ni mlozi sitakataa.
Waachie vijana wapete, we kaa pembeni na vikongwe wenzio ..... time's up!!
 
Hivi huyu Membe hayupo kwenye list!
 
Omutwale asante sana umedadavua fresh kabisa mdau,,,,mimi kila siku huwa napochangia kuhusu membe huwa siach kugusia suala la MTAMA,,,,ukitaka maoni kwamba agombee asigombee waulize wana mtama
 
Mzee Mwanakijiji,
Sintopendekeza mtu isipokuwa kwa manufaa ya taifa na japokuwa Membe ni kichwa, muweza ukiachana na habari za Ufisadi wake maana huko CCM hakuna msafi kihivyo. Wayahudi walilaaniwa tena na Mungu mwenyewe lakini bado wanaitawala dunia.

Hivyo pamoja na utetezi wako bado nakuhakikishia kwamba CCM wataweza tu kushindana ikiwa watamsimamisha Asha Rose Migiro na hii itatokana na WANAWAKE kutumia kauli mbiu ya TUKIWEZESHWA TUNAWEZA. Itakuwa sio swala la chama bali wanawake against the rest...Na amini maneno yangu watu hawatatazama tena nyuma wala kutazama uwezo wa AshaRose isipokuwa ni mageuzi ambayo kwao yatawalemaza akili..

Kwa upande wa ushindani na hasa Chadema wanatakiwa kuanza mapema sana kumtafuta na kumwandaa mgombea japo kwa siri lakini nawatahadharisha mapema - KAZI IPO 2015 wajipange mapema na vizuri sana laa sivyo itakuwa aibu maana elimu ya Uraia haijazama vichwani mwa wananchi hivyo SHIDA na MATATIZO yanatangulia Mapenzi yao..

unamaanisha nini kuwa KICHWA,,,,,
USHAHIDI????
 
Back
Top Bottom