Hofu yatanda Jijini Mwanza, wakazi wajifungia ndani ya nyumba zao siku nzima ya leo

MSAGA SUMU

JF-Expert Member
May 25, 2015
6,482
20,428
Katika hali ya kustaajabisha siku ya leo jumamosi, jiji la Mwanza hasa maeneo ya Buzuruga, Nyasaka, Mahina, Mhandu, Gedeli na maeneo mengine ya jirani hali imekuwa tofauti na ilivyozeleka.

Katika maeneo tajwa katika siku nzima ya leo anga limekuwa kama lina vumbi au ukungu au vyote kwa pamoja na hivyo kuzua sintofahamu.

Kwa kawaida huwa hakuna ukungu na jua likawepo kwa wakati mmoja. Baadhi ya watu nilioongea nao wamezitaka mamlaka husika kufanya uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo na wengine wakidai labda ni wananchi wanapiga nyungu kwa ujumla siku ya leo.

Picha na maoni zaidi ya wakazi yanakuja kadri nitakavyoyapokea.
 
Wekeni picha haraka tuone ili kama kuna uwezekano, tutume haraka ndege za serikali ili zije ziwaokoe.

Nyinyi watu ya Kanda ya Ziwa ni viumbe muhimu sana. Mmetuletea Marais wawili kwenye nchi yetu. Hivyo hatutokubali kuwaacha muangamie.
 
Hebu fanya uchunguzi kama siyo kitu kingine basi watakuwa nzige wanapita hama wanatafuta eneo watue wafanye uharibifu.
 
Ni karibu Kanda ya ziwa yote. Idara ya hali ya hewa itoe ufafanuzi. Nipo Mkoa mmojawapo wa Kanda hii. Eneo lote Kuna hiyo hali
Wametoa jana
IMG_20210220_174234_442.jpg
 
Back
Top Bottom