Hofu hii inasababishwa na nini na kwanini haikuwapo wakati wa kupigania uhuru?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,266
HOFU HII INASABABISHWA NA NINI KWANINI HAIKUWAPO WAKATI WA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA?

KUSUPA HAPENDEZEWI NA KUSEMA KUWA CHIEF MKWAWA ALIKUWA MUISLAM ANASEMA:

‘’MOHAMED SAID USICHEZE NA HISTORIA YA WAHEHE, WAPO WANAOIJUA VILIVYO!
ETI MKWAWA AJIITE ABDALLAH? HIVI KWELI WEWE UNAMJUA MKWAVINYIKA?

Mohamed Said naandika haya baada ya kuisoma post yako kuhusu Abdallah Mkwawa, nami nina machache ya kukwambia;
1. Tumekunyamazia unapotoa maandishi yako juu ya historia ya TANU na mwelekeo wako wa kutaka kuwaaminisha (wanaokuamini) kwamba TANU kilikuwa chama cha Waislamu, kilianzishwa na Waislamu, kiliiamarishwa na Waislamu…’’

Jibu langu kwake Bwana Kusupa:
''Ndugu yangu Kusupa umehamaki sana.

Najua kwa nini umehamaki na kwa mbali katikati ya mistari unajaribu kunitisha.

Hayo yote niliyoandika nimeyapata Mkwawa Museum Kalenga.
Si kama mie naandika bila ushahidi.

Yuko mtaalamu wa historia ya Mkwawa hapo makumbusho unaweza ukamuuliza.

Nilimuuliza kuhusu Mkwawa kuwa Muislam.

Akaniambia ni kweli.
Nikamuuliza aliupataje?

Akamtaja Abushiri bin Salim Suriyama kutoka Pangani.

Nikamuuliza jina lake la Kiislam.

Akaniambia ni Abdul.
Nikamsahihisha nikamwambia ni Abdallah.

Sithubutu hata kidogo kucheza na historia ya Wahehe wala na ya yeyote awaye yule.

Ikiwa kuandika yale yaliyoandikwa Mkwawa Museum ni "kucheza," basi wanaochezea historia hiyo si mie bali ni wenyewe wenye dhamana ya kuhifadhi historia hii.

Angalia hapo chini imeandikwa Abushiri asili yake ni Tanga.

Ukweli ni kuwa Abushiri ni Mzanzibari na ndiye aliyemfunza Mkwawa kuandika na kusoma kwa hati za Kiarabu.

Barua hii aliyoandika Mtwa Abdallah Mkwawa kwa mkono wake ipo Mkwawa Museum.

Hapo chini inaonyeshwa barua aliyoandikwa na Mtwa Abdallah Mkwawa.

Ndugu zangu haya ndiyo niiyoyakuta Mkwawa Museum Kalenga nikayaandika na haya ndugu zangu ndiyo yaliyomghadhibisha

Bwana Kusupa na kunionya mimi nisicheze na historia ya Wahehe kama ilivyo huko juu.

Huu uoga wa majina ya Kiislam nini maana yake?

Huyo hapo juu chini jina wanalolipenda wanahistoria wetu ni Songea Mbano ingawa ukweli jina lake ni Abdulrauf Songea Mbano.

Ukieleza kuwa hilo jina mnalomwita la Songea Mbano mnalikatiza jina lake ni Abdulrauf Songea Mbano kuna watu wanaghadhibika hawalitaki jina hilo.

Halikadhalika Mkomanile jina lake ni Khadija Mkomanile lakini jina la Khadija hawalipendi.

Kote katika historia ya Vita Vya Maji Maji mashujaa hawa hawatambulishwi kwa majina yao kamili ya Kiislam.

Hii nini maana yake?

1656560188235.png
1656560263218.png
1656560236993.png
1656560338190.png
1656560308599.png
 
Mzee wangu mimi nisaidie, hivi hayo majina unayoyasema ni ua kiislamu au ya Kiarabu?

Kwa mfano wewe Mohammed Said vizazi vinavyokuja kuna ambaye atajuwa angalau jina la ukoo wako?

Mimi kwa maoni yangu hii ni mentality slave.
Matola,
Hoja iliyopo mezani ni kufutwa historia ya kweli.
 
Inaonekana purpose ya maisha yako ni kutaka kuaminisha uma kwamba TANU ni chama cha waislamu. Na wapigania uhuru wote walikuwa ni waislamu. Lakini yanakufaidisha nini haya?

Tukiwatambua tu kama Watanzania bila kuangalia dini zao kuna shida?
Pacbig,
Uislam ulikuwa na nguvu katika TANU.
Lakini si kuwa wapigania uhuru wote walikuwa Waislam.

Nini nafaidika ni kuwa historia ilipokuja kuandikwa mchango wa Waislam ukafutwa.

Hii ilikuwa kufutwa kwa historia ya wazee wangu na takriban historia ya miaka inayokaribia karne moja au na zaidi.

Faida niliyopata ni huku kuandika historia hiyo na sasa ni sehemu muhimu katika historia ya Tanganyika na Afrika.

Kleist Sykes na wanae wamo katika Dictionary of African Biography ingawa hawamo katika kitabu cha historia ya TANU kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni.
 
Matola,
Hilo swali halima maana sana kwangu kwa kuwa kila mtu ana uoni wake.
Ukitaka kujibu utasababisha majibizano bila sababu ya maana.
Nadhani kwa usomi wako na kuwa mwanahistoria mzuri bila shaka unamkumbuka makamu wa Rais wa Saddam Hussein ndugu Tariq Aziz, huyu ni mkristo mkatoliki.

Kama umetembea tembea kanda ya ziwa hasa mkoa wa Mara majina kama Abdallah na Juma yanatumiwa na wakristo wengi tu tena wengine ni wapagani hawana dini.
 

HOFU HII INASABABISHWA NA NINI KWANINI HAIKUWAPO WAKATI WA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA?

KUSUPA HAPENDEZEWI NA KUSEMA KUWA CHIEF MKWAWA ALIKUWA MUISLAM ANASEMA:

‘’MOHAMED SAID USICHEZE NA HISTORIA YA WAHEHE, WAPO WANAOIJUA VILIVYO!
ETI MKWAWA AJIITE ABDALLAH? HIVI KWELI WEWE UNAMJUA MKWAVINYIKA?

Mohamed Said naandika haya baada ya kuisoma post yako kuhusu Abdallah Mkwawa, nami nina machache ya kukwambia;
1. Tumekunyamazia unapotoa maandishi yako juu ya historia ya TANU na mwelekeo wako wa kutaka kuwaaminisha (wanaokuamini) kwamba TANU kilikuwa chama cha Waislamu, kilianzishwa na Waislamu, kiliiamarishwa na Waislamu…’’

Jibu langu kwake Bwana Kusupa:
''Ndugu yangu Kusupa umehamaki sana.

Najua kwa nini umehamaki na kwa mbali katikati ya mistari unajaribu kunitisha.

Hayo yote niliyoandika nimeyapata Mkwawa Museum Kalenga.
Si kama mie naandika bila ushahidi.

Yuko mtaalamu wa historia ya Mkwawa hapo makumbusho unaweza ukamuuliza.

Nilimuuliza kuhusu Mkwawa kuwa Muislam.

Akaniambia ni kweli.
Nikamuuliza aliupataje?

Akamtaja Abushiri bin Salim Suriyama kutoka Pangani.

Nikamuuliza jina lake la Kiislam.

Akaniambia ni Abdul.
Nikamsahihisha nikamwambia ni Abdallah.

Sithubutu hata kidogo kucheza na historia ya Wahehe wala na ya yeyote awaye yule.

Ikiwa kuandika yale yaliyoandikwa Mkwawa Museum ni "kucheza," basi wanaochezea historia hiyo si mie bali ni wenyewe wenye dhamana ya kuhifadhi historia hii.

Angalia hapo chini imeandikwa Abushiri asili yake ni Tanga.

Ukweli ni kuwa Abushiri ni Mzanzibari na ndiye aliyemfunza Mkwawa kuandika na kusoma kwa hati za Kiarabu.

Barua hii aliyoandika Mtwa Abdallah Mkwawa kwa mkono wake ipo Mkwawa Museum.

Hapo chini inaonyeshwa barua aliyoandikwa na Mtwa Abdallah Mkwawa.

Ndugu zangu haya ndiyo niiyoyakuta Mkwawa Museum Kalenga nikayaandika na haya ndugu zangu ndiyo yaliyomghadhibisha

Bwana Kusupa na kunionya mimi nisicheze na historia ya Wahehe kama ilivyo huko juu.

Huu uoga wa majina ya Kiislam nini maana yake?

Huyo hapo juu chini jina wanalolipenda wanahistoria wetu ni Songea Mbano ingawa ukweli jina lake ni Abdulrauf Songea Mbano.

Ukieleza kuwa hilo jina mnalomwita la Songea Mbano mnalikatiza jina lake ni Abdulrauf Songea Mbano kuna watu wanaghadhibika hawalitaki jina hilo.

Halikadhalika Mkomanile jina lake ni Khadija Mkomanile lakini jina la Khadija hawalipendi.

Kote katika historia ya Vita Vya Maji Maji mashujaa hawa hawatambulishwi kwa majina yao kamili ya Kiislam.

Hii nini maana yake?

View attachment 2277103View attachment 2277106View attachment 2277105View attachment 2277108View attachment 2277107
Mkwawa alipewa hilo jina ki utani tu na swahiba yake Abushiri waliokuwa wanafanya wote biashara...lakini Mkwawa hakuwa muislamu.....kujua kiarabu, hakukufanyi uwe muislamu
 


Mkwawa alipewa hilo jina ki utani tu na swahiba yake Abushiri waliokuwa wanafanya wote biashara...lakini Mkwawa hakuwa muislamu.....kujua kiarabu, hakukufanyi uwe muislamu
Vito...
Linapokuja suala la Uislam akili zinakataa kukubali ukweli.

Mkwawa alikuwa na ndugu yake jina lake Yusuf na alikuwa ni jemadari katika jeshi lake.

Kuna ukoo Iringa ambao una uhusiano makhsusi na nyumba ya Mkwawa.

Familia hii ipo hadi leo.

Hawa babu yao alipewa uongozi wa kijiji kwa sharti kuwa asilimu.

Wajukuu wa ukoo huu walinitafuta kunieleza historia hii.

Hawa waliniambia kuwa toka enzi na enzi wao wanaiheshimu familia ya Mkwawa kuanzia Mtwa Abdallah, Sapi, Adam hadi Abdul.

Wakati naelezwa historia hii mpashaji wangu habari Abdul Sapi Mkwawa ndiyo alikuwa Mtwa na mimi nilikuwa rika hilo hilo.
 
mbona kama mnajipa tabu sana! chain ya chifu Mkwawa si bado ipo(wajukuu zake) kwanini msiwaulize wao ndio watakuwa wanajua zaidi kuhusu imani ya babu yao...mwandishi yeye kafanya hivyo kwa kufika eneo husika la historia ya chifu na kutuletea historia hiyo kwanini kabla ya kumbishia mwandishi nanyi mnaobisha msifanye utafiti na kutuletea majibu kama alivyofanya mwandishi
 
mbona kama mnajipa tabu sana! chain ya chifu Mkwawa si bado ipo(wajukuu zake) kwanini msiwaulize wao ndio watakuwa wanajua zaidi kuhusu imani ya babu yao...mwandishi yeye kafanya hivyo kwa kufika eneo husika la historia ya chifu na kutuletea historia hiyo kwanini kabla yao kumbishia mwandishi nanyi mnaobisha msifanye utafiti na kutuletea majibu kama alivyofanya mwandishi
Ukoo wa Mkwawa upo..na sio waislamu....Sasa itakuwaje Mkwawa awe muislamu?.....Iringa waislamu ni wachache sana...kumejaa makanisa na wakristo kila kona
 
Ukoo wa Mkwawa upo..na sio waislamu....Sasa itakuwaje Mkwawa awe muislamu?.....Iringa waislamu ni wachache sana...kumejaa makanisa na wakristo kila kona
duh...haya bana nashkuru ila nikuulize umefanya utafiti kabla hujajibu au umeandika kwa hisia?japo mwandishi hakuzungumza kuhusu wingi au uchache wa waislamu au imani ingine kwa mkoa huo alicgizungumza ni imani
ya chifu huyo, unamjua mrithi wa uchifu wa Mkwawa wa hivi sasa yule kijana mdogo,unafahamu imani yake?
 
Ukoo wa Mkwawa upo..na sio waislamu....Sasa itakuwaje Mkwawa awe muislamu?.....Iringa waislamu ni wachache sana...kumejaa makanisa na wakristo kila kona
Vito...
Wapo Mkwawa ambao si Waislam hili linafahamika lakini uchifu umebakia kwa ukoo wa Mtwa Abdallah Mkwawa.

Ingia Google utaisoma historia hiyo tena kutoka vyanzo vya kuaminika.

Fika Kalenga Mkwawa Museum utajifunza mengi.
 
Mzee kilizi aliyefungwa kwa tabia zake za hovyo amejaa udini na chuki zidi ya wakristo wakati elimu na ufahamu kapewa na shule za kanisa wakupuuzwa hafai hata kusikilizwa.

Anataka kupotosha historia ya nchi na kuondoa umoja wa watanzania kutoka na illusion zake.

Mpotoshaji na mzushi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom