Kyachakiche
JF-Expert Member
- Feb 16, 2009
- 983
- 207
Kwa vijana wa zamani watakumbuka jinsi huduma ya kunyoa nywele ilivyokuwa ikitolewa.
Kama siyo chini ya mti mkubwa wenye kivuli basi ilikuwa ni kwenye vibanda vidogo vidogo ambavyo kulikuwepo na kinyozi mmoja mwanaume.
Taratibu kwa kadri muda ulivyoendelea na utandawazi kushika hatamu, sasa tunashuhudia naweza kusema nyumba za kisasa kabisa zimejengwa ama kugeuzwa kuwa maeneo ya kunyolea nywele huku huduma nyingine za kuosha nywele,uso, kucha na nyingine kama hizo zikifanywa na akina dada tena warembo kweli kweli.
Baadhi ya hawa akina dada wamekuwa wanavaa nguo ambazo wakati mwingine zinaacha maswali mengi kwamba je ni huduma hii ya kufanya usafi wa nywele na uso ama ni zaidi ya hapo. Na zaidi ya hapo wakati wa hizi huduma wana minjonjo mingi tu kama kufungua vifungo vya shati ili waweke taulo/kitambaa, wasugue masikio, shingo,..nk.
Nawaulizeni wana-JF wenzangu, je kama uko na mai waifu wako akaona unayofanyiwa na hawa akina dada atakuruhusu uwe unakwenda peke yako? Au kama maiwaifu wako angekuwa anafanya kazi huko, ungemruhusu awafanyie wanaume wengine vile hawa akina dada wanafanya?
Na tujadili!
Kama siyo chini ya mti mkubwa wenye kivuli basi ilikuwa ni kwenye vibanda vidogo vidogo ambavyo kulikuwepo na kinyozi mmoja mwanaume.
Taratibu kwa kadri muda ulivyoendelea na utandawazi kushika hatamu, sasa tunashuhudia naweza kusema nyumba za kisasa kabisa zimejengwa ama kugeuzwa kuwa maeneo ya kunyolea nywele huku huduma nyingine za kuosha nywele,uso, kucha na nyingine kama hizo zikifanywa na akina dada tena warembo kweli kweli.
Baadhi ya hawa akina dada wamekuwa wanavaa nguo ambazo wakati mwingine zinaacha maswali mengi kwamba je ni huduma hii ya kufanya usafi wa nywele na uso ama ni zaidi ya hapo. Na zaidi ya hapo wakati wa hizi huduma wana minjonjo mingi tu kama kufungua vifungo vya shati ili waweke taulo/kitambaa, wasugue masikio, shingo,..nk.
Nawaulizeni wana-JF wenzangu, je kama uko na mai waifu wako akaona unayofanyiwa na hawa akina dada atakuruhusu uwe unakwenda peke yako? Au kama maiwaifu wako angekuwa anafanya kazi huko, ungemruhusu awafanyie wanaume wengine vile hawa akina dada wanafanya?
Na tujadili!