Hizi SALON za kiume za massage na Kushave balaa

Kyachakiche

JF-Expert Member
Feb 16, 2009
983
207
Kwa vijana wa zamani watakumbuka jinsi huduma ya kunyoa nywele ilivyokuwa ikitolewa.

Kama siyo chini ya mti mkubwa wenye kivuli basi ilikuwa ni kwenye vibanda vidogo vidogo ambavyo kulikuwepo na kinyozi mmoja mwanaume.

Taratibu kwa kadri muda ulivyoendelea na utandawazi kushika hatamu, sasa tunashuhudia naweza kusema nyumba za kisasa kabisa zimejengwa ama kugeuzwa kuwa maeneo ya kunyolea nywele huku huduma nyingine za kuosha nywele,uso, kucha na nyingine kama hizo zikifanywa na akina dada tena warembo kweli kweli.

Baadhi ya hawa akina dada wamekuwa wanavaa nguo ambazo wakati mwingine zinaacha maswali mengi kwamba je ni huduma hii ya kufanya usafi wa nywele na uso ama ni zaidi ya hapo. Na zaidi ya hapo wakati wa hizi huduma wana minjonjo mingi tu kama kufungua vifungo vya shati ili waweke taulo/kitambaa, wasugue masikio, shingo,..nk.

Nawaulizeni wana-JF wenzangu, je kama uko na mai waifu wako akaona unayofanyiwa na hawa akina dada atakuruhusu uwe unakwenda peke yako? Au kama maiwaifu wako angekuwa anafanya kazi huko, ungemruhusu awafanyie wanaume wengine vile hawa akina dada wanafanya?

Na tujadili!
 
Hapa Mwenge karibia Saloon zote za kiume kuna wanawake
 
Wanatuibia tu..wanatupaka tu-chemicali ambako hata hatutujui..Wanazuga sijui facial sijui nini ..ili mradi ulipie fedha nyingi zaidi..Uwizi mtupu.
 
Kama unaona wewe inakukwaza usiende. Au ukishanyolewa usisafishwe na hao wadada kama unaona itakuharibia......
 
Wanatuibia tu..wanatupaka tu-chemicali ambako hata hatutujui..Wanazuga sijui facial sijui nini ..ili mradi ulipie fedha nyingi zaidi..Uwizi mtupu.
Pamoja na haya ya kulipa malipo makubwa, je mkeo akiona yanayoambatana na hayo malipo kutoka kwa hawa akina dada ingekuwaje?
 
Pamoja na haya ya kulipa malipo makubwa, je mkeo akiona yanayoambatana na hayo malipo kutoka kwa hawa akina dada ingekuwaje?


Kwanza wanaweza wasiamni kama malipo ni ya facial tu halafu wanavyokuwa nashikashika kasikioni utadhani mkeo wezi watu hao akina dada na waliowengi utakuta hawajaolewa kabisa.wezi watu
 
Kama unaona wewe inakukwaza usiende. Au ukishanyolewa usisafishwe na hao wadada kama unaona itakuharibia......
Swala linalojadiliwa hapa ni je, huduma hii inapofanywa na hawa akina dada, akija mkeo akashuhudia atakuruhusu uwe unaendelea kuipata? Au je, kama ni kazi nzuri kama nyingine, utakuwa radhi kumruhusu mkeo akaifanye? Sizungumzii kukwazika ama kutokwazika.
 
Mke wangu hawezi kuniruhusu,pia siwezi kukubali mke wangu afanye hiyo kazi. Omba usifanyiwe hiyo kitu. Wanatekenya vibaya madada hawa,acha kabisa.
 
Kuna jamaa yangu alienda saloon baada ya kunyolewa akaanza kufanyiwa scrub kwa jinsi alivyokuwa anaguswa mpaka kwenye masikio anapitishwa vidole kwa ufundi na binti wa saloon, mwamvuli uko chini ukaanza kukunjuka, kidogo angepiga bao.
 
Kuna jamaa yangu alienda saloon baada ya kunyolewa akaanza kufanyiwa scrub kwa jinsi alivyokuwa anaguswa mpaka kwenye masikio anapitishwa vidole kwa ufundi na binti wa saloon, mwamvuli uko chini ukaanza kukunjuka, kidogo angepiga bao.
Duh! Hapo SIPO!!!
 
Kuna jamaa yangu alienda saloon baada ya kunyolewa akaanza kufanyiwa scrub kwa jinsi alivyokuwa anaguswa mpaka kwenye masikio anapitishwa vidole kwa ufundi na binti wa saloon, mwamvuli uko chini ukaanza kukunjuka, kidogo angepiga bao.

Lazima ni wewe mwenyewe. Ulijua hili?
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom