Hizi ni hasira au kitu gani jamani.......!!??

Mmh! nahisi kuna jambo linamsibu... badala ya kuelekeza nguvu zako kuondoa hasira zake... Jua kwanza ni nini kinamsibu. Kwani alikuwa hivyo siku zote???

sikaonai haka kabatani hapa
The Following User Says Thank You to Mom For This Useful Post:Masikini_Jeuri
 
...Kobe hivi unaweza kuamini last week end niliongea nae na nikamuomba tutoke tuka-spend night moja nje ya kiwanja chetu cha nyumbani lengo likiwa huenda tukiwa katika mazingira tofauti tunaweza kuzungumza na may be kumshawishi anieleze kama ana jambo linalomsumbua hiki ndicho alichonijibu.." Huko kwenye mahoteli na magesti unakopeleka mademu zako nenda mwenyewe sio kunipeleka mimi". nilibaki hoi jamaa yangu..!

Alishawahi kukutuhumu kuwa una cheat hata kwa hisia tu?
 
Lugha gani inatumika hapa; nachotaka kusema ni kuwa kama hivyo inaonekana unapoint makosa kwake! je unajaribu kutake part of the blame? Badalaya kusema "Mwenzangu una matatizo" sema (naona tuna matatizo); Kuwa msikivu na sikiliza how does she feel? je yeye haoni mnayo matatizo? Mpe vigezo kwa kuitazama hali yenu ya zamani na ya sasa! Also make haer fell proud kwa yale mazuri yaliyopo sasa na hilo kosekana linalokosekana liwe ni jambo la kumalizia!

Kama nakufananisha vile....mwaga nondo.
 
MMh pole labda akiwa na wewe anasikia hasira!! je ulishawahi chunguza ukimpigia simu anaact hivyohivyo??
..Mkuu nami nahisi kitu cha namna hiyo kwa huenda anapokuwa na mimi ni kama mtu anayejawa na hasira. Niliongea na mdada mmoja wanafanya kazi ofisi moja akadai hata yeye hamuelewi kwakuwa mtu mwenyewe ni mkimya sana so huwezi kum-define kama ndio ukimya wa kawaida au vipi? Kwenye simu yuko so lovely, polite ingawaje kuna wakati anawaka from no where na hasa ukimuuliza swali ambalo aidha hana uhakika jibu lake. Yeye anakimbilia "ah! mi sijui bwana"
 
Alishawahi kukutuhumu kuwa una cheat hata kwa hisia tu?
..Kiukweli hajawahi ila kuna ile lugha ya wanawake sijui kama inatokana na simulizi au inakuwa vipi kuwa eti sisi wanaume hatuaminiki ingawa mtu ukimuhoji hana ushahidi wa kuthibitisha anachosema!
 
Lugha gani inatumika hapa; nachotaka kusema ni kuwa kama hivyo inaonekana unapoint makosa kwake! je unajaribu kutake part of the blame? Badalaya kusema "Mwenzangu una matatizo" sema (naona tuna matatizo); Kuwa msikivu na sikiliza how does she feel? je yeye haoni mnayo matatizo? Mpe vigezo kwa kuitazama hali yenu ya zamani na ya sasa! Also make haer fell proud kwa yale mazuri yaliyopo sasa na hilo kosekana linalokosekana liwe ni jambo la kumalizia
..Nakubaliana na wewe na unachosema. Kiukweli mtu muungwana huwezi moja kwa moja ukaelekeza lawama na matatizo kwa mwenzio. Ingawa kiukweli huwa namuuliza sana kwanini kila anapojibu kitu inakuwa katika hali ya ukali. Kwa mfano mmepanga kutoka outing kwa hulka za akina dada siku zote wao muda huwa hautoshi unapojaribu kumuhimiza ajitahidi kuchangamka katika kujiandaa kwake unakutana na majibu "kama una haraka unaweza kwenda tu"
 
..Mkuu nami nahisi kitu cha namna hiyo kwa huenda anapokuwa na mimi ni kama mtu anayejawa na hasira. Niliongea na mdada mmoja wanafanya kazi ofisi moja akadai hata yeye hamuelewi kwakuwa mtu mwenyewe ni mkimya sana so huwezi kum-define kama ndio ukimya wa kawaida au vipi? Kwenye simu yuko so lovely, polite ingawaje kuna wakati anawaka from no where na hasa ukimuuliza swali ambalo aidha hana uhakika jibu lake. Yeye anakimbilia "ah! mi sijui bwana"

Inaelekea umeshajijengea PROTECTIVE MODE ; yaani kila unapoongea naye you want to detect the unkowns! Hii si nzuri! Ah sijui inaweza kuwa jibu la mkato na lisiwe na maana yoyote! Take it easy man!
 
..Kiukweli hajawahi ila kuna ile lugha ya wanawake sijui kama inatokana na simulizi au inakuwa vipi kuwa eti sisi wanaume hatuaminiki ingawa mtu ukimuhoji hana ushahidi wa kuthibitisha anachosema!

Kosa la kwanza ni hayo mahojiano!

hebu jaribu kuligeuza kuwa utani; na wakati mwingine jifanye kama hukulisikia; ignore the thorning words in her sentences!
 
Kaangu hilo tatizo la wifi kwa kiasi kikubwa limesababishwa na wewe mwenyewe jinsi unavyo mtreat.
Nakushauri nawe ujaribu kubadili life style yako labda aweza badilika.
Ama ikishindikana zungumza na rafikize wa karibu nao waweza kuwa na msaada.

Una uhakika we hata hujauliza mwenzio anamtreat vp shemeji yetu umeshamhukumu aaargh!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mapenzi yanagusa moyo wake moja kwamoja ndugu yangu ndo maana unaona ni kwenye mapezi tu! Mapenzi ndiyo yanampa amani; furaha na kujiamini pia! Nenda naye kwa hadhari sana! Kitu cha kwanza amabacho nakiona kwako ni kwamba unajihesabia kuwa uko right! well hili linaweza kuwa la kwanza; siku zote ukishajihesabia haki madhara yake huwa kutoona kabisa kasoro zako ama kutokuwa tayari kuzitambua kuwa ni kasoro! Hilo laweza kumtia ghadhabu mwenzio na kwa kuwa tumetofautiana kama ni mtu wa kukasirika haraka basi unaweza kutopata muafaka kwani ambacho ni kasoro kwake kwako sio!

Hujatueleza ikiwa mshawahi kuongelea hali hii bila wewe kulalamika; kwa sabu sipati picha kuwa Unaanza kwa upole ama unalalamika kukosa na kumnyooshea vidole kila siku?
...Unajua mtu anaweza kuona kama vile mimi ni mtu wa kumtupia shutuma yeye. Kifupi ni kuwa nilipohisi anakuwa tofautia nilichofanya ni kuongeza ukaribu wangu kwake kwani niliamini there must be something wrong..Lengo ni kujua kama kuna tatizo na nilikuwa wazi kwake kwa kuwa mimi ni mtu wake wa karibu nawajibika kujua ili kama kuna msaada nitoe. Hapo ndipo shida iliposhika kasi. Pia jambo lingine tunalotofautiana nae sana ni ile tabia ya kugeneralize behavior za wanaume anazosimuliwa kama ni ofisini kwake au saloon sijui. Huwa namuelwesha kuwa kila binadamu ana mapungufu na tabia zake so yeye anichukulie mimi kama mimi basi ya wengine hayana nafasi...!
 
Mpenzi wangu amekuwa na hali inayonichanganya sana. Nashindwa kuelewa kama ni hasira za kawaida au kuna jambo zaidi. Kila mnapokuwa katika maongezi chochote atakacho-comment mara zote ni katika tone ya ukali..Mwanzoni nilidhani huenda kuna mambo yanayomtinga akilini hadi kumfanya awe hivyo lakini ni zaidi ya mwaka sasa hata mazungumzo ya kawaida tu huwa katika hali ya ukali usiokuwa na sababu. Rafiki yangu mmoja akanishauri kuwa nitafute mtaalamu wa ushauri nasaha ili aweze kupata kitu wanaita wenyewe " anger management class". Hivi wataalamu wa aina hii wapo hapa Tanzania kwa anayefahamu anijulishe maana sipendi kwa kweli kumpoteza huyu honey wangu lakini hili tatizo laweza kunifanya ni-act differently!!!.

Kweli una true love kwa mwenzio..hicho ni kipindi cha mpito.....hebu jaribu kumuuliza kwa upole zaidi na katika mazingira tulivu anasumbuliwa na nini ..mie wakati mwingine nikiwa na jambo linanitatiza au linaniboa huwa najikuta nakuwa na hasira na kila mtu.kitu nachofanya huwa nakaa kimya alone kwa muda mpaka niwe normal .ila huyo mwenzetu mwaka mmoja ni muda mrefu sana kuwa hivyo..
 
..Nakubaliana na wewe na unachosema. Kiukweli mtu muungwana huwezi moja kwa moja ukaelekeza lawama na matatizo kwa mwenzio. Ingawa kiukweli huwa namuuliza sana kwanini kila anapojibu kitu inakuwa katika hali ya ukali. Kwa mfano mmepanga kutoka outing kwa hulka za akina dada siku zote wao muda huwa hautoshi unapojaribu kumuhimiza ajitahidi kuchangamka katika kujiandaa kwake unakutana na majibu "kama una haraka unaweza kwenda tu"

Mie hujibiwa hivyo wakati mwingine; kwani jokes aside hawa wenzetu kwenye kujiremba ITS BIG DEAL; na kuanzia sasa ipe priority shughuli hii!

Pamoja na kuwa hapaswi kujibu hivyo wakati wote; nawe pia using'ang'anize kupewa majibu yako kila utapo kujua; Waswahili wanasema funika kombe mwanaharamu apite!
 
Kosa la kwanza ni hayo mahojiano!

hebu jaribu kuligeuza kuwa utani; na wakati mwingine jifanye kama hukulisikia; ignore the thorning words in her sentences!
MJ, hapa umenena yanayompasa mwenye hekima, hata mimi umenisaidia sana. Unajua sometimes tunaweza kuhisi wenzetu wana makosa lakini maswali na maneno yetu wenyewe ni ya kukera na kukatisha tamaa sana.
 
Kweli una true love kwa mwenzio..hicho ni kipindi cha mpito.....hebu jaribu kumuuliza kwa upole zaidi na katika mazingira tulivu anasumbuliwa na nini ..mie wakati mwingine nikiwa na jambo linanitatiza au linaniboa huwa najikuta nakuwa na hasira na kila mtu.kitu nachofanya huwa nakaa kimya alone kwa muda mpaka niwe normal .ila huyo mwenzetu mwaka mmoja ni muda mrefu sana kuwa hivyo..
..Teh! teee! Kwanza umependezesha na hiyo avatar yako umekata nywele!!! Huwezi kuamini upole ninaotumia katika mazungumzo yangu na huyu mdada kiasi kwamba kuna wakati unafikia nadhani hata yeye mwenyewe huruma inamjia anabadirika. Tatizo kwa nini hizi hasira hasira zisizo na mpango ziwepo tu kilal wakati. Katika mapenzi jamani mikwaruzano ipo mtu asiniambie eti mwanamke akifanya jambo lisiloeleweka usimuulize au mtu usimshauri kama unaona unakwenda wrong...au nasema uongo wajameni??
 
..Teh! teee! Kwanza umependezesha na hiyo avatar yako umekata nywele!!! Huwezi kuamini upole ninaotumia katika mazungumzo yangu na huyu mdada kiasi kwamba kuna wakati unafikia nadhani hata yeye mwenyewe huruma inamjia anabadirika. Tatizo kwa nini hizi hasira hasira zisizo na mpango ziwepo tu kilal wakati. Katika mapenzi jamani mikwaruzano ipo mtu asiniambie eti mwanamke akifanya jambo lisiloeleweka usimuulize au mtu usimshauri kama unaona unakwenda wrong...au nasema uongo wajameni??

Unayo kila aright ya kujua na ni wajibu wako kujua; tatizo ni how ,and when she is ready!
Nikupongeze na usikate tamaa; wala usianze kumuona kiumbe wa ajabu ama ulikosea kumchagua kama mdau alivyosema huwa ni PHASE zinatujia tofauti hivyo hata reaction zetu ni tofauti! Bear with her! take one step at a time! by the way how long have you been maried ..... do you have kids? labda nimeoverlook ikiwa ulieleza.
 
Mpenzi wangu amekuwa na hali inayonichanganya sana. Nashindwa kuelewa kama ni hasira za kawaida au kuna jambo zaidi. Kila mnapokuwa katika maongezi chochote atakacho-comment mara zote ni katika tone ya ukali..Mwanzoni nilidhani huenda kuna mambo yanayomtinga akilini hadi kumfanya awe hivyo lakini ni zaidi ya mwaka sasa hata mazungumzo ya kawaida tu huwa katika hali ya ukali usiokuwa na sababu. Rafiki yangu mmoja akanishauri kuwa nitafute mtaalamu wa ushauri nasaha ili aweze kupata kitu wanaita wenyewe " anger management class". Hivi wataalamu wa aina hii wapo hapa Tanzania kwa anayefahamu anijulishe maana sipendi kwa kweli kumpoteza huyu honey wangu lakini hili tatizo laweza kunifanya ni-act differently!!!.


Pole mwenzangu!

Mara nyingi ni stress za Maisha, wakati huu mgumu sana, pengine mwenzio Deal zake nyingi haziingiani, na majukumu yanzidi, jaribu kumchukulia rahisi na kum-mbembeleza mwisho atafungua Moyo wake akijiona mkosa!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom