Hizi ni dalili 7 kuwa una Uraibu (Addiction) ya matumizi ya Simu

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
1709895775350.png

Simu ni Kifaa muhimu cha mawasiliano kwa binadamu yeyote lakini haitakiwi kuwa sehemu ya mwili wako kiasi cha kukufanya uwe kama mtumwa kifaa hicho.

Wataalaamu wa Saikolojia wanasema, ukitaka kubaini kama umepata Uraibu (Addiction) ya matumizi ya Simu, anza kuangalia ni kwa muda gani unaweza kukaa bila kushika Simu yako hasa muda ambao uko peke yako bila shughuli nyingine.

Inashauriwa ukibaini umepata Uraibu wa Simu, anza taratibu kwa kujizuia kwa kupunguza matumizi yake ambapo unaweza kuweka muda maalumu 'Time Limit' kwenye 'App' unazozipenda zaidi mfano, Instagram, Twitter, TikTok n.k. ziwe zinajifunga kila baada ya dakika kadhaa.

Vipi Mdau, umeweka Tiki kwenye dalili ngapi hapo?
 
Simu inakufanya utume emoji za upendo na simanzi na kilio bila kuonana na watu
Hii inakufanya uwe mpweke wa bila kujijua
Huwezi hata kusafiri kuwaona watu kisa uliwasalimia kwa simu
Simu inakuweka mbali na watu, kama mtanielewa
 
imgonline-com-ua-dexifcfcOWK9Y1pC9.jpg

Tokea Jan 1, simu yangu natumia saa 6 kwa siku. Mwaka jana nilikua natumia saa 5.

Mwaka huu nimeongeza saa 1 la kujipongeza kwa mafanikio ya mwaka jana
 
Back
Top Bottom