Elon Musk kuleta Intaneti ni tishio kwa mitandao ya simu, atapora wateja wenye matumizi makubwa na kuteka soko sehemu ambazo network inasumbua

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,040
4,081
images (46).jpeg


Bei ya vifaa vyote na kuwekewa ni shilingi laki 9.

kifurushi kinadumu kwa mwezi, nadhani anapanga bei kwa kuangalia uchumi wa nchi, Marekani ni 230,000/= , Nigeria ni 98,000, Hapa Kwetu si ajabu ikawa 70,000.

Ni internet ya kisasa, Speed yake ni kubwa sana, unaweza kushusha file la gb 1 speed ikiwa chini dakika 3 na speed ikiwa poa ni sekunde 50 tu, kwenye kuperuzi ni kugusa tu hakuna kusubiri, kucheki video ama video call hakuna mambo ya kuganda ganda.

Haina kikomo, ukitumia hata gb 20 kwa siku ni wewe.

Inaweza kupatikana mpaka mbugani, milimani, kwenye makorongo na sehemu remote ambazo mitandao ya simu haijaweza kufikia, Ni kama vile dstv.
.....................................................................................

ujio wake unaweza kupora wateja wengi wenye matumizi makubwa, hii ni hatari kwa makampuni ya simu na kama mjuavyo kuna watu wana hisa zao huko. Mbaya zaidi kifaa kimoja kinaweza kutumika hata kwa watu 50 kwa mpigo maana speed ni kubwa hata ikigawanywa, ni hatari ukizaliwa utamaduni wa watu kujichanga huku wakiacha kununua mabando,

Kwa kuwa internet ni ya Satelite hapa itaweza kufika hadi maporini na vijijini ambako maeneo hayo mengi internet huwa ni changamoto, hii itakuwa changamoto kwa mitandao ya simu hasa katika miji inayokuwa wakitaka kuweka minara watakuta tayari watu wameshazoea starlink.
..............................................................................

HITIMISHO

Kwa hali hii nadhani naanza kuelewa kwanini vibali vinacheleweshwa, sitashangaa njia ya kumuondosha ikiwa ni tozo nzito sana zitazofanya hata kifurushi kuwa bei sawa na mitandao ya simu, dana dana za kusaini documents kila uchwao au tukaja sikia kisingizio kwamba huduma inaharibu mazingira, ni hatari kwa usalama, n.k.
 
vifaa na Installation ni milioni 1.

kifurushi inayegemeana na nchi, kwa Marekani ni 220,000 kwa mwezi, kwa nchi zenye uchumi wa kati kapunguza kidogo mfano Nigeria ni laki 1 kwa Mwezi, Hapa Kwetu yawezekana ikawa hata elf 60 kwa mwezi.

Speed yake ni kubwa sana unaweza kushusha file la gb 1 si chini ya sekunde 20.

Haina kikomo

Inaweza kupatikana mpaka mbugani, milimani, kwenye makorongo na sehemu remote ambazo mitandao ya simu haijaweza kufikia.
Aisee analeta lini hii? Ili tuachane haraka na hawa makampuni wezi wenye ubia na CCM
 
Hawawezi kushindana na wakati. Wakithubutu wataishia kupata maumivu.
Unajua solution ni rahis tu ili usipoteze mapato wakubaliwe tu wakifanya tofaut na hivyo wataikosesha serikali mapato unajua watu watakua wanaenda nje kama Kenya wananunua vifaa hivyo anakuja kufunga kwake alaf analipia kila mwezi hapo serikali itakua inakosa mapato kizembe sanaa kisa kukunja
 
Back
Top Bottom