Uchaguzi 2020 Hizi ndiyo sababu zilizompa Dkt. Magufuli ushindi wa kishindo

Kwanza natoa pale kwa upinzani hasa CHADEMA kuwa uchaguzi huu sio kama 2015 ambapo kila mtanzania alikuwa amechoshwa na CCM.

Na kila raia alikua tayari kwa lolote ikisubiriwa kauli tu kwamba sasa tuingie barabarani tukichafue.

1. Baada ya Magufuli kuingia 2015 akafuta kazi migambo wote. Hapa wale vijana wasiokuwa na ajira walijiajiri na kufanya kazi kwa uhuru bila bugdha(2015 walikuwa tayari hawa n ni wengi mno)

2. Amefanikiwa kudhibiti matumizi makubwa ya serikali na kubana matumizi.

3. Kuanzisha miradi mingi ya maendeleo. Reli,anga,kuhamia Dodoma, ujenzi wa barabara nyingi

4. Kuondoa baadhi ya urasimu katika ofisi za serikali pamoja na kuwa karibu wananchi. Hii imemfanya aonekane raisi wa wanyonge kweli kweli.

5. Kuleta heshima serikalini,hakuna tena mambo ya "unanijua mm ni nani"? Kila ofisi ya umma unayoenda unapata heshima na kuthaminiwa kuwa ww ndio boss.

6. Kuwapa watu uhuru wa kufanya biashara popote bila shida( ukikimbizwa na 🐕 rusha mifupa kwa nyuma) kwa sasa hakuna vijana wengi wasio na kazi mtaani kama zamani,kila mtu ana mishe zake utamwambia nani aandamane akusikilize?

Suala la kuandamana linahitaji watu wengi wenye hasira kweli kweli.

MY TAKE:
Magufuli sio malaika au Mungu kwa hiyo ana mapungufu yake. Mapungufu yake hayamnyimi heshima yake ya kuongoza awamu ya pili. Vijana wengi kwa sasa wako huru kufanya kazi au biashara zao bila bugdha yeyote toka serikalini kwanini wahangaike na kuandamana?

Ana mke ana majukumu mbalimbali anawaza kuhusu kesho yake akipigwa kwenye maandamano? Uhalisia wa maisha ya mtanzania ni mitaani na sio kwenye mitandao. Mtu anaishi US eti ana hasira na utawala 🤪! Umemkosea nini
Then why
Azuie access to internet and socia media kama alikuwa anajua anacho kibali kikubwa kwa waTZ dhidi ya Upinzani. Pia hawajatuambia hiyo efficiency ya tume ya Uchaguzi kumaliza kutangaza wabunge within 24 hours walitumia technolojia gani kipindi hiki maana hata wamarekani hawana hiyo technolojia.

Tukubali mchezo mchafu ulichezwa na damu zimemwagika na watu kubaki na machungu sana ya kuumizwa. Dama hizi zinalia mbele za Mungu na mungu atapatiliza kisasi juu ya walioamuru na waliofanya na kusababisha unyama huu
 
Watoto wa maskini kitambulisho cha mmachinga kitamhusu kiroho safi.
Faida ya vile vitambulisho wamachinga wana ijua ndo mana wanatamani aendele tuu
Walikua wanalipa karibia 100k kwa mwezi kwa sasa vidogo vyao na ushuru wa halimashauri imekua ni 20k tuu.unadhan kuna machinga ata mruka uyo mwambaa
 
Bado so evidence hiyo
Thibitisha hilo
Unataka evidence gani? Mfano wa pili ni mitandao kuzimwa ili wizi usiripotiwe. Mfano wa tatu no mauaji ya wapinzani Zanzibar na kwingineko Kama tarime waliokuwa wanajaribu kuzuia Kura zisiibiwe. Mfano mwingine no mabox ya Kura zilikwishapigwa zilizokamatwa kawe polisi wakawa smart kuzificha lakini tayari clip zimeshanasa.
 
Now it's all about diplomatic win win situation
Wakiweka vikwazo watapata wapi izo malighafi
Ndio hapo sasa!! Yan wao wanatutegemea sisi bila sisi wao watakwama. Tanzania ni tofauti na Zimbabwe
 
Ndio hapo sasa!! Yan wao wanatutegemea sisi bila sisi wao watakwama. Tanzania ni tofauti na Zimbabwe
Mnaongea Kama mmekatwa vichwa. Walimtaka Mari gafi wanachukua tu Nani wa kuwazuia. Kama gadafi na uchumi wake mkubwa walimchomoa shimoni Kama kuku.
 
Then why
Azuie access to internet and socia media kama alikuwa anajua anacho kibali kikubwa kwa waTZ dhidi ya Upinzani. Pia hawajatuambia hiyo efficiency ya tume ya Uchaguzi kumaliza kutangaza wabunge within 24 hours walitumia technolojia gani kipindi hiki maana hata wamarekani hawana hiyo technolojia. tukubali mchezo mchafu ulichezwa na damu zimemwagika na watu kubaki na machungu sana ya kuumizwa. Dama hizi zinalia mbele za Mungu na mungu atapatiliza kisasi juu ya walioamuru na waliofanya na kusababisha unyama huu
😁Kwaio mna mwachia Mungu!! Aya basi msililie mitandaoni sasa fanyeni maombi kwa bidii
 
Mnaongea Kama mmekatwa vichwa. Walimtaka Mari gafi wanachukua tu Nani wa kuwazuia. Kama gadafi na uchumi wake mkubwa walimchomoa shimoni Kama kuku.
Gadafi yeye aliingiliwa kijeshi sasa Tanzania kama ni vikwazo hazina madhara kwetu Ila wao ndio wana shida na sisi
 
Gadafi yeye aliingiliwa kijeshi sasa Tanzania kama ni vikwazo hazina madhara kwetu Ila wao ndio wana shida na sisi
Kwani sisi watashindwa kutuingilia kijeshi na hili jeshi letu dhaifu la kuonea wapinzani tu. Mi naomba hata kesho watuingilie kijeshi Mana mapolisi na akina mabeyo wanatunyanyasa sna na wameua Sana wapinzani
 
Kwani sisi watashindwa kutuingilia kijeshi na hili jeshi letu dhaifu la kuonea wapinzani tu. Mi naomba hata kesho watuingilie kijeshi Mana mapolisi na akina mabeyo wanatunyanyasa sna na wameua Sana wapinzani
Sasa hiyo itakuwa hasara kwa wote ni siyo CCM peke yao
 
Faida ya vile vitambulisho wamachinga wana ijua ndo mana wanatamani aendele tuu
Walikua wanalipa karibia 100k kwa mwezi kwa sasa vidogo vyao na ushuru wa halimashauri imekua ni 20k tuu.unadhan kuna machinga ata mruka uyo mwambaa
Faida za kile kitambulisho ni nyingi sana mkuu maana hata mikopo bank unaweza kuombea,hakika mwamba ametisha sana.

Mitano tenaaaaaaaaaaaaa.
 
Kwanza natoa pale kwa upinzani hasa CHADEMA kuwa uchaguzi huu sio kama 2015 ambapo kila mtanzania alikuwa amechoshwa na CCM.

Na kila raia alikua tayari kwa lolote ikisubiriwa kauli tu kwamba sasa tuingie barabarani tukichafue.

1. Baada ya Magufuli kuingia 2015 akafuta kazi migambo wote. Hapa wale vijana wasiokuwa na ajira walijiajiri na kufanya kazi kwa uhuru bila bugdha(2015 walikuwa tayari hawa n ni wengi mno)

2. Amefanikiwa kudhibiti matumizi makubwa ya serikali na kubana matumizi.

3. Kuanzisha miradi mingi ya maendeleo. Reli,anga,kuhamia Dodoma, ujenzi wa barabara nyingi

4. Kuondoa baadhi ya urasimu katika ofisi za serikali pamoja na kuwa karibu wananchi. Hii imemfanya aonekane raisi wa wanyonge kweli kweli.

5. Kuleta heshima serikalini,hakuna tena mambo ya "unanijua mm ni nani"? Kila ofisi ya umma unayoenda unapata heshima na kuthaminiwa kuwa ww ndio boss.

6. Kuwapa watu uhuru wa kufanya biashara popote bila shida( ukikimbizwa na 🐕 rusha mifupa kwa nyuma) kwa sasa hakuna vijana wengi wasio na kazi mtaani kama zamani,kila mtu ana mishe zake utamwambia nani aandamane akusikilize?

Suala la kuandamana linahitaji watu wengi wenye hasira kweli kweli.

MY TAKE:
Magufuli sio malaika au Mungu kwa hiyo ana mapungufu yake. Mapungufu yake hayamnyimi heshima yake ya kuongoza awamu ya pili. Vijana wengi kwa sasa wako huru kufanya kazi au biashara zao bila bugdha yeyote toka serikalini kwanini wahangaike na kuandamana?

Ana mke ana majukumu mbalimbali anawaza kuhusu kesho yake akipigwa kwenye maandamano? Uhalisia wa maisha ya mtanzania ni mitaani na sio kwenye mitandao. Mtu anaishi US eti ana hasira na utawala 🤪! Umemkosea nini
Hizi zako Ni Sababu-Nadharia,
Ila Sababu halisi za kushinda kwa Kishindo ni hizi hapa
1) Polisi
2) Tume
3) Wakurugenzi
 
Back
Top Bottom