Hizi ishu za Mungu/Dini ni very complicated

Hizi ishu za Mungu/Dini ni very complicated

Tena wanazuoni na wafia dini wanatusisitizia kabisa kuwa kuna maswali hatupaswi kuuliza kuhusu Mungu, tumeekewa na mipaka kabisa tusije kukufuru, nyiiiee!
Ila ushawahi kuwaza hayo maswali ni nani anapaswa kuulizwa na kuwa na majibu? Maana tusiangalie kwenye kuhoji ama kuuliza tu ila lazima tuangalie ni nani huyo mwenye kupaswa kuulizwa na kuwa na majibu? Maana hao wanazuoni na wafia dini hata wao wamezikuta habari za Mungu na si kwamba wao wanaishi na huyo Mungu hadi tudhani wanapaswa kujua habari zote kuhusu Mungu.
 
Swali jingine kwanini Mungu afanye kazi mpaka ACHOKE??? Na akichoka wakati wa kupumzika hufanya nini?? Analala, anakunywa maji ya baridi, sharubati au mvinyo??
Sasa mkuu wewe hapo hata sidhani kama unajua Rais Samia huwa anafanya nini na nini akiwa Ikulu ila unataka kujua Mungu akichoka anafanya nini?
 
Kweli, na kwa sababu watunzi wa hizo story washakufa ndio maana kuna maswali mengi hawa wafia dini hawawezi kujibu.
Kama bado watunzi wangekuwa hai kila siku tungeendelea kusikia aya mpya simeshushwa kutoka mbinguni kujibu maswali ya watu.
Sema kama kuna kuchanganya vitu, kwa nini unadhani point ya msingi kuhusu Mungu ni kuwa na majibu ya kila swali analojisikia mtu kuuliza au kutaka kujua kuhusu Mungu?
 
Dini zote Zina sema kuwa mungu ana wapenda binaadamu wote bila kujali rangi zao hana matabaka , dini hizo hizo zinasema mungu ndiye mlinzi wa binaadamu lakini Kwa Sasa tunashindwa kuona akitoa ulinzi huo Kwa wa Congo, na badala yake ameiacha kwenye vita kubwa ya wenyewe kwa wenyewe, kwenye mauaji ya rwanda watu walichinjwa makanisani bila Mungu kuingilia,, watu wanakufa , watoto wazee , wajane mungu yupo tu ana watizama, kama anaupendo wa kweli na ana nguvu kwanini asizuie machafuko yasiendelee kuwepo ( nimekupa huu mfano ila najua utajifanya hunielewi )
Aisee
 
Hayupo mkuu. Hilo liko wazi. Nyingine zinabaki kua stori tu ama hadithi za kidini lakini mungu anaetajwa kwenye dini hayupo.
Mungu anayetajwa kwenye dini au maelezo yenye kuhusu Mungu kutoka kwenye dini? Kwa sababu tunachoelewa wenye dini na wasio na dini wote husema Mungu ni mmoja tu hivyo wanakusudia kitu kimoja ila wanatofautiana kwenye kukielezea hicho kitu.
 
Na hata huyo binadamu mwenyewe akitengeneza kitu chochote iwe mashine au chochote kile hakiwezi kua 100% perfect yaani coefficient of machine haiwezi kua 100% hata itoke kiwandani muda huu na chochote kile kingine mpaka vyakula, lazima kitakua na kasoro fulani
Efficiency
 
Back
Top Bottom