Mzee wa Gumzo
Senior Member
- Apr 21, 2008
- 197
- 5
Kila uchwao maswali mengi hujipanga kichwani mwangu mzee wa gumzo lakini huwa sipati majibu.
Jamani naomba tusaidiane hili la balali,si mnamkumbuka yule gavana wa benki kuu ya tanzania aliyepewa nafasi hiyo akitokea (kuazimwa)IFM?.
Baada ya kuibuka kwa sakata la EPA na rais kumvua ugavana tulitarajia kuona kasi,hari na nguvu mpya katika kumkamata balali na kumfikisha mbele ya pilato kama shahidi wa kwanza na muhimu katika uporaji wa mabilioni ya wadanganyika.
Lakini mpaka leo kimyaaaa!.Hatusikii chochote kuhusu mtu huyu.tuliambiwa alikuwa marekani anatibiwa lakini mpaka leo?
Hivi kwa ishu nyeti kama hii mpaka leo balali anavinjari tu mitaani?Tunahitaji nini kumkamata? au tunaogopa nini?au niseme watawala wetu wangwaya nini kumleta balali mbele ya mkono wa sheria???
Mimi wala sielewi,labda nyiye wadanganyika wenzangu mnajua zaidi yangu!haki ya nani hii nchi!
Uwanja wenu waungwana
Jamani naomba tusaidiane hili la balali,si mnamkumbuka yule gavana wa benki kuu ya tanzania aliyepewa nafasi hiyo akitokea (kuazimwa)IFM?.
Baada ya kuibuka kwa sakata la EPA na rais kumvua ugavana tulitarajia kuona kasi,hari na nguvu mpya katika kumkamata balali na kumfikisha mbele ya pilato kama shahidi wa kwanza na muhimu katika uporaji wa mabilioni ya wadanganyika.
Lakini mpaka leo kimyaaaa!.Hatusikii chochote kuhusu mtu huyu.tuliambiwa alikuwa marekani anatibiwa lakini mpaka leo?
Hivi kwa ishu nyeti kama hii mpaka leo balali anavinjari tu mitaani?Tunahitaji nini kumkamata? au tunaogopa nini?au niseme watawala wetu wangwaya nini kumleta balali mbele ya mkono wa sheria???
Mimi wala sielewi,labda nyiye wadanganyika wenzangu mnajua zaidi yangu!haki ya nani hii nchi!
Uwanja wenu waungwana