Kukutafuta haimaniishi kuwa anakupenda. Anakukejeli tu, na wewe kwake ni spear tyre. Wewe ndiyo unamshobokea ila yeye hana muda na wewe.
Mwanamke ananayekupenda kwa dhati
1. Yupo active sana. Atakupigia simu au kukutumia meseji kila muda. Hata km yupo bize kiasi gani atakutumia meseji, haiwezi kupita hata siku moja bila kukutumia meseji au kukubipu. Huwa wanakuwa wasumbufu sana kwenye mawasiliano. Km hutafutwi habari yako iliisha kitambo
2. Hulalamika sana usipompigia simu au meseji. Lawama zinakuwa nyingi sana
3. Anakuwa na wivu sana na wewe yaani atataka wasiliane na wewe ajue upo na nani wakati huo.
4. Anakuheshimu sana kwa kuhofia kumuacha
N.B
Ushaachwa kitambo sana, hapo alikuwa anatest mitambo km mnyanga wake yupo ila hana shida na wewe kwasababu yupo anayempenda na wanawasiliana. Huenda kuna visenti anataka. Km unabisha siku moja chukua simu, utaona kuna namba moja hivi wanawasiliana sana.
Siku wakikorofishana na jamaa au akipigwa chini huko atakuja kwako kwa muda na siku akipata mtu anayempenda atakuacha.
Nilishapita huko, najua. Mwanamke ambaye hakupendi wala hana muda na wewe kwenye mawasiliano huwa anapuuzia. Ukimtumia meseji anaweza asijibu au akikujibu ni kwa mkato, huwa inachukua masaa 7 au 10 wakati mwingine. Ukimtumia meseji asubuhi anaweza kukujibu saa 10 na huwezi kuchati naye kwa dk 45. Hata akikuta missed zako hakutafuti, wewe ndiyo unakuwa bize kumtafuta kuliko yeye. Siku akikutafura basi anashida ya hela