Hivi wanaume wote wako hivi?

Pole sana mkuu kwa msongo wa mawazo.kwa mishale niliyoikwepa mpaka sasa nasikitika kukwambia kuwa una tatizo kubwa kuliko udhaniavyo,sababu haiwezekani ukose raha na usijue sababu mkuu.Ila nitakusaidia

Kwanza hakuna dini inayosema uzae watoto 7 ndani ya miaka 8,msisome mistari ya vitabu vitakatifu kama mnavyosoma hadithi za shigongo,popote utakapoanzia basi unaelewa kuanzia hapo ulipoanzia.dini ipi ambayo inasisitiza ukatili kwa mke wako? Maana huwezi kumchosha mwenzio hvyo halafu ukasingizia dini,lakini pia hata kwa malezi ya watoto hiyo sio sahihi sababu hutoweza kuwapa attention inayotakiwa wote.

Pili nirudi kwenye tatizo lako,kinachokupa mawazo ni watoto mkuu utake usitake,hata kama una hela sana na hauna ugomvi na wife.Binadamu kaumbwa na kiasi ,limitation ya kuhandle mambo kulingana na umri,una miaka 33 watoto 6 kwa mama mmoja hata uwe bilionea lazima uumie kichwa sababu malezi sio pesa otherwise watoto wa matajiri wasingekuwa wavuta bangi,ndio maana unakumbuka maisha yako kabla ya kuwa na watoto sababu kulikuwa hakuna kero ya kuhudumia watoto wanaofuatana

Funga kizazi dili na hao ulionao sasa wanatosha.
 
Mkuu usikate tamaa kilichobaki sasa hv ni kuwa karibu na Mungu zaidi ya awali nakutafuta namna ya kuifanya familia yako kuwa bora, nakuomba usifikirie tofauti na hata siku moja kuikimbia familia yako!!!
Real Man & gud dady ni yule anaeface matatizo yanapomkabili,
usilegeze kamba na kukubali kushindwa kilahisi ur a man you born to fight.
Kaa chini ongea na mkeo jinsi ya sasa hv kuweza kuishep familia yenu kuwa imara, i believe in God mtashinda.
 
Hapana nakupa ukweli wa mambo

Kama sio kweli kwanini unakumbuka maisha yako ya zamani kabla hujawapata hao watoto

Majukumu yameongezeka maradufu.

Alafu umesema mkeo ana uja uzito wa miezi miwili bila shaka atakuwa mtoto wa 7.Muonee mkeo huruma jamani atakosa nguvu.

Alafu hivi mtu utakuwa na mawazo usijue yamesababishwa na kitu gani??

Hebu muonee huyo mkeo huruma..hata kama kuzaa ni amri ya mungu wewe unaspidi kalii. Kaka unatatizo la kupenda mechi ya kwenye 6x6 yaelekea...umesena hutumii kilevi hahahaaa...sasa huu unaoufanya ni zaidi ya ulevi...au una wivu na mkeo...hapumui .kwa style hii mkeo akitoka 40 huwa ushamjaza mimba.. Halafu huijui nyota ya kijani. Kwani unafanya kazi gani . Huna watu wanaokuzunguka ukaiga hata upangaji wa familia? Mtoto mdogo ana umri gani na mkubwa ana umri gani. Mawazo yapunguze maana hako ka team kanatakiwa kusoma jipange erooo....
 
Ukiwa muongo uwe na kumbukumbu,your post is fake one with unrealistic information,miaka 7 ya ndoa watoto 6?jipange!halafu unataka tukushauri nini na jibu unalo?sio lazima kufungua thread.
 
Mawazo yako yanasababishwa na ukubwa wa familia yako mkuu. Kaa na mkeo mlijadili hilo na mjue jinsi mtakavyo i care hiyo idadi ya watoto. We unazani kuwa na pesa ndio kuzaa tu kwasababu pesa zipo? Marezi bora niyale ya intensive feelings of caring for your family while human being is created with limitation level of caring. Huyu utampenda zaidi na mwingine tofauti. Jipange
 
Huwa unatindikiwa na aina gani ya mawazo?

Halafu mkuu miaka 33 una watoto 6, hao watoto ni mapacha pair tatu au kila mtoto mmoja alizaliwa kipeke yake ndani ya miaka hiyo 7?

Serious huyu jamaa hajui hata kutunga t doesn't make sense kabisa dah
 
Kamanda kama una kazi chapa kazi ipasavyo! Kama huna kazi tafuta kazi na ongeza kipato! Kuwa na watoto wengi kiasi hicho siyo tatizo kwangu binafsi maana hata mimi ninao wengi lakini sioni cha kunikosesha amani. Tena zaidi umesema mnapendana na mkewe sasa msongo wa mawazo ni wa nini? Au umepata mwingine hivyo upo njia panda kufikiria uongeze mke mwwingine?

Mwanaume lazima uwe mtu wa kuwajibika siyo kulalamika na kujikosesha amani bure, watoto ndo hao umewapata sasa utafanyaje; au unafikiri kuwapunguza ndo uwe na amani? Tutakutia hatiani ukiua hata mmoja. Wapo watu wengi katika jamii wanasaka watoto hata kwa sala na Ndagu lakini they proved nothing! Unapaswa ujisikie fahari kuwa na makamanda hao na uweke mikakati mizuri ya kuwapatia elimu na maisha bora in future.
 
Watoto 6 ndani ya miaka 7 halafu utegemee utaishi kwa raha?? Hata kama una kila kitu usingemzalisha mkeo kwa kasi ya ajabu hivyo. Acha mawazo ya kunywa pombe kwani siyo solution. Anza kutoka out na familia yako mara kwa mara kuanzia sasa.
 
Ukiwa muongo uwe na kumbukumbu,your post is fake one with unrealistic information,miaka 7 ya ndoa watoto 6?jipange!halafu unataka tukushauri nini na jibu unalo?sio lazima kufungua thread.

Stori za kutunga imekuwa fasheni humu kwa hiyo usishangae mtu kujichanganya %http://
 
33 watoto sita afu uishi kwa raha imekula kwako wakati wenzio ndo wanaanza kuinjoy ujana we unaota mvi lol hata huyo nkr unafikiri atakuhali zaidi anawazia watoto wakati wote.

Au we mpemba nini?
 
Watoto sita ndani ya miaka saba?ndio maana unamsongo wa mawazo....sasa imeshatokea hauna cha kufanya inabidi tu ukubali kwamba wewe ni baba wa watoto sita at the age of 33...bt inabidi upunguze au kuacha kabisa hiyo biashara ya kupata watoto usiku na mchana.lol kwa dunia hii only two kids wananitosha....tule bata vizuri.
 
Kweli hata kama una pesa hao watoto wamefuatana sana,halafu ni wengi ,,,,inawezekana wanakuongezea msongo,i can Imagine 6 kids in 7 years,labda kama uliwapata kabla ya kuoa,,,,,but bado ni wengi sana
 
Watoto 6 ndani ya miaka 7 lazima uwe na woga; ndani ya miaka 14 utakuwa na watoto 12;

mwenzio niko ndani ya ndoa miaka 19 nina watoto 2 tu; nina amani kupita kiasi kwani watoto hao ni kama wadogo zangu.
 
KIRANGWA uposahihi nahisi baada ya watoto kuwa wengi na mkewe kuwa ni mjamzito wa miezi miwili sasa yuko njia panda anawaza kuongeza bibi mwingine ndio mawazo yayomkosesha amani, jitahidi mkuu kama dini inaruhusu na uwezo wa kifedha umesha declare kwamba sio mbaya, ongeza ila uwe makini nahuyo mwingine usizae nae dizaini hii ya mke wa kwanza
 
Nina miaka 33 nimeoa miaka 7 iliyopita nimejaaliwa watoto 6, hali yangu ya kimaisha sio mabaya ninao uwezo wa kifedha.

Turudi kwenye topic nimekuwa ni mtu mwenye mawazo kila wakati Nafsi yangu haina raha nasijui tatizo ninini.

Tuna maelewano mazuri sana na mke wangu hatuna ugomvi, tatizo hili limeanza kama mwaka mmoja umepita na siku zinavozidi kwenda ugonjwa huu naona unazidi kuwa Mkubwa kwangu.

Situmii kilevi cha Aina yoyote ile Jamani embu nisaidieni natamani sana kufurahia maisha.

WE jamaa una akili kweli wewe?miaka saba watoto 6?uwiiiiii mimi,usiogope ila anza kuwasomesha wakipata elimu nzuri watakujali na hii furaha ya ujanani uliyo ikosa utaipata uzeeni sababu watakutunza sana tu huo msongo wa mawazo mkuu utaisha,utafurahi uzeeni muda huu zaa na kuwaleatu kama ulivyoanza natumaini ukifika 45 watakuwepo kumi na tano hivi mkuuu,hongera ila
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom