Hivi walimu ni wajinga au wapumbavu?

Hivi walimu ni wajinga au wapumbavu?

Unaweza ukafundishwa na mpumbavu na ukawa mwerevu na hii ni kitu ya kawaida kabisa kwani kazi ya mwalimu ni kujenga base tu ila maarifa huwa yanapatikana kulingana na mazingira tulionayo

Mfano mitaala yetu haifundishi staudy za kopyuta hadi ufike elimu ya vyuo lakini tunajua kopyuta na alichosaidia mwalimu ni kutufundisha kusoma na kuandika tu tena kwa kalamu

ww sio mtu makin kabisa..
 
si ndo hapo? Kama mwlm anashida mwache na shida zake yeye kakubaliana na hali halisi..

Wengi wanaropoka humu lakn kumbe wanalishwa na mashemeji zao lakn wakikaa nyuma ya keyboard dharau zmewajaa.

Na bandle wananunuliwa na shemeji zao kama sio kubana change, mim ndio maana nawadis maana wengi hata salary slip hawaijui ipoje ila midomo kama chuchunge.
 
Unaweza ukafundishwa na mpumbavu na ukawa mwerevu na hii ni kitu ya kawaida kabisa kwani kazi ya mwalimu ni kujenga base tu ila maarifa huwa yanapatikana kulingana na mazingira tulionayo

Mfano mitaala yetu haifundishi staudy za kopyuta hadi ufike elimu ya vyuo lakini tunajua kopyuta na alichosaidia mwalimu ni kutufundisha kusoma na kuandika tu tena kwa kalamu

umekiri mwalimu anajenga base (msingi). hakuna mtu mhimu kama anayekujengea misingi ktk maisha. hakuna jambo linalosimama bila kuwa msingi. Washukuruni walimu na sio kuwatukana huku mkiendela kuwarundikia watoto wenu wawafundishe. Na itapendeza kama mtawaelimisha jinsi ya kutatua kero zao na sio kuwatukana.
 
Sio.kila anaejenga base ni mwelewa licha ya kazi anayofanya mwalimu bado mwenyewe hajapanga mipango ya kujikomboa mwenyewe
 
mwandishi unataka kusema cwt means chama cha wapuuzi tanzania?walimu wakeup ndugu zangu
 
tena hii cwt kwa wilaya ya kahama ni kama haipo upuuzi mtupu
 
sasa mkuu hapa na wewe umeandika nini..? au na wewe ni mwalimu..?
maana naona hakuna "concordial relationship".

Mkuu, hujaelewa nini? Alitaka kukuonesha kwamba na yeye lugha ya malkia anaifahamu, hilo tu hayo mengine wala hukupaswa hata kusoma.
 
hii CWT naonA kamA vilE ni tawI la CCM ,na palipo CCM ufisadI hauepukikI cha msingI ni walimU wotE washirikianE kufanyA maamuzI magumU ya kuwaondoA hawA CCM .kwanI natambuA kuwA walimU ni wengI na wakishirikianA wao kwaO na siye tusiokuwa walimu tutawezA kufanyA hyo ktU.kinyumE chA hapO walimU wataendeleA kulalamikA mpakA mpakA bhaaasss kwanI hakunA wakuwasikilizA
 
Mtoa mada naomb nikuambie jambo kwamba kama kwel ni mcha Mungu waombe radh walimu kwa kuwa hizo lugha mbil ulzotumia si za kiungwana. usimdharau mwinzako kwa kaz anayofanya tunaish kwa kutegemeana kwa kila idara pale unapoona kuna mapungufu katika idara ya mwenzako una nafasi ya kushauri na si kutumia lugha mbovu kiasi hcho kwan hata Mungu sidhan kama inampendeza. mwenzako anatoa sadaka yake kwa kazi anayofanya kwa nini umtukane?

Wewe unafikiri kazi gan iliyo bora hapa Tanzania? Then utambue USIACHE MBACHAO KWA MSALA UPITAO. Kwa kwel lugha uliyotumia ni ya kukatisha tamaa lakini okay nakubaliana na falsafa inayozungumzia kwamba "hakuna kweli moja"
mueleze! hajitambui, shuleni alienda kusomea ujinga tu! hawezi kutukana wazazi wetu ovyoovyo! kumbuka salary hiyo imetusaidia sisi kutusomesha hadi chuo!
 
Hii kitu sio kama anavyoeleza huyu ndugu, ukweli ni kuwa hawa CWT ni taasisi kweli inayoshughulika na walimu lkn sio wote kwnza ilikuwa lazma kujiunga na kuanza kukatwa lkn baadae walimu walianza kuhoji kuwa kama mifuko ya kijamii inakuja kushawish wafanyakaz wapya kujiunga ktk mifuko yao, kwann na cwt wasje kutoa elimu na kuvuna wanachama bdala yke wanalazimisha tu.

Basi baada ya kubanwa sana na walimu hasa wa shahada ya kwnza waliamua kufanya opption ktk kujiunga. Hivyo kwa sasa kuwa mwanachama wa CWT ni lazma ujaze fomu zao za uanachama na wala co utaratib wa zaman kuwa sku utakayopangiwa kituo cha kazi ya ualimu basi tayari unakuwa umeshakua MWANACHAMA WA CWT na utaanza kukatwa tangu mshahara wa kwanza.

CWT unajiunga moja kwa moja...kujaza form ni ili upate kitambulisho
 
Mwalimu kupata huduma ya chama haina ulazima wa yeye kujua ofisi za CWT wilaya au mkoa. Kubwa ni kushiriki katika shughuli za chama tangu ngazi ya tawi (shule) hadi Taifa. Uwepo wa chama cha wafanyakazi ni kwa lengo la kujenga mshikamano na siyo kufahamu maeneo yalipo maofisi ya chama. Kasome vizuri ELRA NA. 6 OF 2004 uelimike. Unawaita walimu wajinga/wapumbavu!! Watake radhi ndg yangu.

Mkuu kweli umetoa shule ya Maana.

Usishangae mleta Mada anataka watu waanze ku mention CCM hapo,maana wana style nyingi hawa wenye mihemko
 
"Mjinga hujifunza mpumbavu hubisha "
Katika nchi yetu ya Tanzania kundi kubwa la wafanya kazi ni walimu, lakini kwa maoni yangu ni kundi ambalo halijitambui kabisa na ni kinyume na lilivyotarajiwa.

Kero kubwa kwa walimu sio serikali bali ni chama chao kinachiotwa (CWT) ambacho kipo kwa ajili ya kuwaplease walimu pale wanapokuwa na lengo la kudai maslahi yao kwa Serikali.

Na chama hiki kimewafanya walimu kama mazombi na mtaji wa maisha ya wachache wanaojiita CWT, na hata hivyo uzombi huo wa walimu unadhihirika siku hadi siku.

Kwani wapo walimu hawajui hata ofisi ya CWT katika wilaya zao na hata kazi ya chama katika maisha yake ya kazi lakini anakatwa mchango wa CWT,

Je, walimu ni wajinga au wapumbavu?

Unaonesha ni jinsi gani ulivo na fikra finyu. Kama unafikra pana ungefikisha ujumbe/ushaur wako ktk lugha ya kistaarabu.

Isingekua hao waalimu unaowatusi ungetoa wapi hata huo ujanja wa kuandika hapa? Unakua kama hujaingia darasan bhana
 
Wakati nimemaliza kidato cha sita,nikiwa natafakari naangalia nikasomee nini cha kuisaidia jamii! Kuna Mwalimu mmoja aliniambia "kijana wangu ukiamua kua mwalimu maisha yako yote yatakua ni kuvaa suti moja tu na tai kila siku,kusubiria mshahara kwa ajili ya kulipa madeni,utazaa watoto wako wanne na kujenga kijumba kimoja cha vyumba vitatu basi na usubirie hela ya kustaafu" Mpaka leo sijafanikiwa kuipata vizuri kauli ya mwalimu huyo aliyekua amebakiwa na miaka 5 kustaafu alimaanisha nini.

Swala la umaskini wa mfanyakazi hapa Tanzania ni kwa nyanja zote na sio kwa waalimu tu.

Tofauti yao ni kwamba wengine wana upenyo wa kufanya ujanja(kupiga dili) wakati waalimu hawana.
 
ujinga sio tusi kutojua suala lolote ni ujinga pesa zinakusanywa sana lakini hatujui zinako kwenda.
 
Inawezekana una lengo zuri sana la kueleza kile kinachokukera au kutaka kujua kile usichofahamu na pia inawezakana hata unachotaka kukieleza kimekupotea. Labda naomba nikuulize swali moja; je, unafahamu matatizo ya walimu? au kwa mtazamo wako walimu wana matatizo gani kadri ya hisia zako?

Inawezekana ni mwalimu ameamua kulalamika
 
Lugha kali za hovyo kwa walimu siyo stahili yao, iweni na shukurani walimu wamewatoa umbumbumbu. CWT ipo kwa maslahi ya wachache na siyo walimu uliowatukana hapa. Ni tawi la unyonyaji kama yalivyo matawi ya unyonyaji mengine. Kukwepa ufisadi wa CWT siyo rahisi kama unavyofikiria. Walimu wengi hawakujaza form za kujiunga, kujaza form labda ni kupata kitambulisho tu, kukwepa kujaza form haizuii kukatwa. Suluhisho ni kurekebisha juu huko kulikozaa CWT.
 
sasa mkuu hapa na wewe umeandika nini..? au na wewe ni mwalimu..?
maana naona hakuna "concordial relationship".

Mkuu, tatizo liko wapi hapo?

Hilo limelenga kueleza wapiga kura sio waalimu peke yao,taasisi zote zinahusika kwa ujumla wake....
 
Back
Top Bottom