Hivi ni nani aliye msafi?

Hivi ni nani aliye msafi?

bnhai

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2009
Posts
2,846
Reaction score
2,402
Ndugu wana JF tumekuwa tukilaumu saana serikali yetu kwa mambo mbalimbali nakujiaminisha kabisa kuwa sasa ni wakati muafaka wa kukitoa Chama Tawala Madarakani. Nimekuwa nikijiuliza na hatimaye nikaona ipo haja ya kuileta hoja hii jamvini. Tukiitoa CCM madarakani, nani anafaa kuchukua madaraka kama Rais wa Tz. Anatoka Chama gani? Ameifanyia nini nchi yake? Je ni msafi? Hana kashfa au ufisadi wa aina yoyote? Si mbaguzi? Au nani anamfano wa watu wachache wazalendo wanaoweza kuongoza nchi yetu. Kwa maoni yangu naona hakuna mbadala katika kizazi cha sasa. Labda tuwaandae watoto wetu. Tukae kimya tujipange kwa miaka ijayo. Kwa sasa tukemee ufisadi. Nawakilisha!
 
Ndugu wana JF tumekuwa tukilaumu saana serikali yetu kwa mambo mbalimbali nakujiaminisha kabisa kuwa sasa ni wakati muafaka wa kukitoa Chama Tawala Madarakani. Nimekuwa nikijiuliza na hatimaye nikaona ipo haja ya kuileta hoja hii jamvini. Tukiitoa CCM madarakani, nani anafaa kuchukua madaraka kama Rais wa Tz. Anatoka Chama gani? Ameifanyia nini nchi yake? Je ni msafi? Hana kashfa au ufisadi wa aina yoyote? Si mbaguzi? Au nani anamfano wa watu wachache wazalendo wanaoweza kuongoza nchi yetu. Kwa maoni yangu naona hakuna mbadala katika kizazi cha sasa. Labda tuwaandae watoto wetu. Tukae kimya tujipange kwa miaka ijayo. Kwa sasa tukemee ufisadi. Nawakilisha!


Huu ni udaku nadhani hapa si pake jamani tuleteni hoja za maana hapa mbona siku hizi kila kitu kinajirudia rudia tuuuuuuuu???
 
Huu ni udaku nadhani hapa si pake jamani tuleteni hoja za maana hapa mbona siku hizi kila kitu kinajirudia rudia tuuuuuuuu???
Nadhani inawezekana kabisa hufaham tafsiri ya udaku. Nadhani kuna ukweli ndani yake. Mawazo lazima yatofautiane. Ukiweza thibitisha kama ni udaku
 
bnhai,
Naamini umeuliza maswali yako kwa roho nzuri kabisa. Kwa maoni yangu tatizo si personalities. Jambo la kujiuliza ni nani atakayeisaidia Tanzania kujenga strong institutions zitakazosimamia kasoro zilizojitokeza zilizopelekea kukithiri kwa rushwa. Mwalimu Nyerere alianza vizuri kwa kuwawekea viongozi miiko ya maadili. Mwinyi akaingia akaiua hiyo miiko pamoja na azimio la Arusha. Nadhani hapo ndipo tunaweza kuanzia. Kwa mtazamo wangu, turudishe miiko ya uongozi. Tuimarishe sheria juu ya rushwa na kuhakikisha vyombo simamizi vina meno ya kupambana na wala rushwa bila kuwaangalia nyuso zao. Baada ya hapo tuunde timu ya Ukweli na Upatanishi na kila mtu anayetuhumiwa kuhusika na ufisadi apelekwe pale ili tujue mizizi ya ufisadi iivyoanza tuweze kuing'oa. Tusimwonee yeyote aibu. Ni kumkoma nyani giladi tu na let the chips fall where they may. Badala ya kutafuta personalities tutafute mwongozo utakaotutoa hapa tulipo. Baada ya hapo ndipo tuseme Sikonge anaweza kusaidia hiki na hiki na Bubu ataka Kusema hiki na kile etc. etc. It can be done. Yes, we can!
 
Kwa maoni yangu naona hakuna mbadala katika kizazi cha sasa.

Hayo ni maoni ya kifisadi - ndivyo wasemavyo wang'ang'anizi wa madaraka siku zote.

Labda tuwaandae watoto wetu.

Nani awaandae - kizazi cha sasa tayari umekihukumu.

Tukae kimya tujipange kwa miaka ijayo. Kwa sasa tukemee ufisadi. Nawakilisha!

Kizazi cha sasa kikae kimya au kikemee - mbona hueleweki ?
 
bnhai,
Naamini umeuliza maswali yako kwa roho nzuri kabisa. Kwa maoni yangu tatizo si personalities. Jambo la kujiuliza ni nani atakayeisaidia Tanzania kujenga strong institutions zitakazozimamia kasoro zilizojitokeza zilizopelekea kukithiri kwa rushwa. Mwalimu Nyerere alianza vizuri kwa kuwawekea viongozi miiko ya maadili. Mwinyi akaingia akaiua hiyo miiko pamoja na azimio la Arusha. Nadhani hapo ndipo tunaweza kuanzia. Kwa mtazamo wangu, turudishe miiko ya uongozi. Tuimarishe sheria juu ya rushwa na kuhakikisha vyombo simamizi vina meno ya kupambana na wala rushwa bila kuwaangalia nyuso zao. Baada ya hapo tuunde timu ya Ukweli na Upatanishi na kila mtu anayetuhumiwa kuhusika na ufisadi apelekwe pale ili tujue mizizi ya ufisadi iivyoanza tuweze kuing'oa. Tusimwonee yeyote aibu. Ni kumkoma nyani giladi tu na let the chips fall where they may. Badala ya kutafuta personalities tutafute mwongozo utakaotutoa hapa tulipo. Baada ya hapo ndipo tuseme Sikonge anaweza kusaidia hiki na hiki na Bubu ataka Kusema hiki na kile etc. etc. It can be done. Yes, we can!

Mkuu, kwa kuongezea hapo, tubadilishe katiba, tupate viongozi kwa ridhaa ya wananchi, Raisi apunguziwe madaraka ya kufanya teuzi mbali mbali, kwani kama ni mbovu na anafanya teuzi za kishikaji ndo kabisaaa kama tunayo yaona! lakini laiti hao wateule wangekuwa wazuri wakawa watendaji, hata raisi akiwa mbovu, walau mambo yanakwenda!

Lakini hata hivo raisi mwenye kuthubutu, kulisema kosa hadharani, kuita a sped kwa jina lake, huenda wapo wengi, lakini kwngu mimi Dr.Slaa comes first!
 
bnhai,
Naamini umeuliza maswali yako kwa roho nzuri kabisa. Kwa maoni yangu tatizo si personalities. Jambo la kujiuliza ni nani atakayeisaidia Tanzania kujenga strong institutions zitakazosimamia kasoro zilizojitokeza zilizopelekea kukithiri kwa rushwa. Mwalimu Nyerere alianza vizuri kwa kuwawekea viongozi miiko ya maadili. Mwinyi akaingia akaiua hiyo miiko pamoja na azimio la Arusha. Nadhani hapo ndipo tunaweza kuanzia. Kwa mtazamo wangu, turudishe miiko ya uongozi. Tuimarishe sheria juu ya rushwa na kuhakikisha vyombo simamizi vina meno ya kupambana na wala rushwa bila kuwaangalia nyuso zao. Baada ya hapo tuunde timu ya Ukweli na Upatanishi na kila mtu anayetuhumiwa kuhusika na ufisadi apelekwe pale ili tujue mizizi ya ufisadi iivyoanza tuweze kuing'oa. Tusimwonee yeyote aibu. Ni kumkoma nyani giladi tu na let the chips fall where they may. Badala ya kutafuta personalities tutafute mwongozo utakaotutoa hapa tulipo. Baada ya hapo ndipo tuseme Sikonge anaweza kusaidia hiki na hiki na Bubu ataka Kusema hiki na kile etc. etc. It can be done. Yes, we can!


Mkuu Jaususi huyu mtu sikutaka kupoteza muda naye sana kumpa maneno ya maana maana yeye hana la maana .Umeona comments zake ? Nilihisi tu huyu yuko kazini sasa angalia majibu yake .
 
bnhai,
Naamini umeuliza maswali yako kwa roho nzuri kabisa. Kwa maoni yangu tatizo si personalities. Jambo la kujiuliza ni nani atakayeisaidia Tanzania kujenga strong institutions zitakazosimamia kasoro zilizojitokeza zilizopelekea kukithiri kwa rushwa. Mwalimu Nyerere alianza vizuri kwa kuwawekea viongozi miiko ya maadili. Mwinyi akaingia akaiua hiyo miiko pamoja na azimio la Arusha. Nadhani hapo ndipo tunaweza kuanzia. Kwa mtazamo wangu, turudishe miiko ya uongozi. Tuimarishe sheria juu ya rushwa na kuhakikisha vyombo simamizi vina meno ya kupambana na wala rushwa bila kuwaangalia nyuso zao. Baada ya hapo tuunde timu ya Ukweli na Upatanishi na kila mtu anayetuhumiwa kuhusika na ufisadi apelekwe pale ili tujue mizizi ya ufisadi iivyoanza tuweze kuing'oa. Tusimwonee yeyote aibu. Ni kumkoma nyani giladi tu na let the chips fall where they may. Badala ya kutafuta personalities tutafute mwongozo utakaotutoa hapa tulipo. Baada ya hapo ndipo tuseme Sikonge anaweza kusaidia hiki na hiki na Bubu ataka Kusema hiki na kile etc. etc. It can be done. Yes, we can!
Asante kwa uchambuzi mzuri lakini suali la msingi kwa sasa tukitaka kuunda nani yupo wa kuziendesha katika kipindi hiki cha mpito? Maana system nzima imeoza na watu wengi hata wenye heshima zao sasa hivi wanatuhumiwa. Tunaanzeje. Nadhani hii inatusaidia kuona tunaundaje serikali bila ya kuwaza vyama uchwara vya siasa
 
Wasafi wengi tu bwana!kama huna hoja ya msingi tuondokee hapa bwana!we bnhai vipi?
 
Wasafi wengi tu bwana!kama huna hoja ya msingi tuondokee hapa bwana!we bnhai vipi?
Jamani hao waliomadarakani wanasema walijiandaa kwa miaka 10. Honestly hoja zetu zinapelekwa na upepo. Leo likitokea la dini wana JF wanasambaratika na kuanza kukashifiana wao kwa wao. Mara ikiibuka ishu nyingine tunapoteana mpaka upepo utulie hakuna lilieleweka. Wengine wakiamini kabisa wenzao wametumwa pale wakiona mawazo hayafanani au wakipewa changamoo. Mie nadhani nilazima kuwa na watu wakutusemea kama tunawaamini. Tujiwekee malengo na tujipime kwa malengo. Labda nitoe mfano wa kwanini nina mashaka. Nilikuwa ninamwamini saana mh Jaji Warioba lakini hivi karibuni naye amekuwa akitajwa kwenye Tangold. Hapo ndio mashaka yanaongezeka nani tumkabidhi nchi yetu? I stand to be corrected
 
Asante kwa uchambuzi mzuri lakini suali la msingi kwa sasa tukitaka kuunda nani yupo wa kuziendesha katika kipindi hiki cha mpito? Maana system nzima imeoza na watu wengi hata wenye heshima zao sasa hivi wanatuhumiwa. Tunaanzeje. Nadhani hii inatusaidia kuona tunaundaje serikali bila ya kuwaza vyama uchwara vya siasa

The answe is not in the leaders but the voters. Kuna msemo usemao "Leaders are a reflection of those who voted for them". Mabadiliko yoyote huleta na wananchi wenyewe na hayo mabadiliko uyasemayo wewe hayata badilika mpaka watu wabadilike kwanza.
 
bnhai,
Naamini umeuliza maswali yako kwa roho nzuri kabisa. Kwa maoni yangu tatizo si personalities. Jambo la kujiuliza ni nani atakayeisaidia Tanzania kujenga strong institutions zitakazosimamia kasoro zilizojitokeza zilizopelekea kukithiri kwa rushwa. Mwalimu Nyerere alianza vizuri kwa kuwawekea viongozi miiko ya maadili. Mwinyi akaingia akaiua hiyo miiko pamoja na azimio la Arusha. Nadhani hapo ndipo tunaweza kuanzia. Kwa mtazamo wangu, turudishe miiko ya uongozi. Tuimarishe sheria juu ya rushwa na kuhakikisha vyombo simamizi vina meno ya kupambana na wala rushwa bila kuwaangalia nyuso zao. Baada ya hapo tuunde timu ya Ukweli na Upatanishi na kila mtu anayetuhumiwa kuhusika na ufisadi apelekwe pale ili tujue mizizi ya ufisadi iivyoanza tuweze kuing'oa. Tusimwonee yeyote aibu. Ni kumkoma nyani giladi tu na let the chips fall where they may. Badala ya kutafuta personalities tutafute mwongozo utakaotutoa hapa tulipo. Baada ya hapo ndipo tuseme Sikonge anaweza kusaidia hiki na hiki na Bubu ataka Kusema hiki na kile etc. etc. It can be done. Yes, we can!



very very good point,
 
Ndugu wana JF tumekuwa tukilaumu saana serikali yetu kwa mambo mbalimbali nakujiaminisha kabisa kuwa sasa ni wakati muafaka wa kukitoa Chama Tawala Madarakani. Nimekuwa nikijiuliza na hatimaye nikaona ipo haja ya kuileta hoja hii jamvini. Tukiitoa CCM madarakani, nani anafaa kuchukua madaraka kama Rais wa Tz. Anatoka Chama gani? Ameifanyia nini nchi yake? Je ni msafi? Hana kashfa au ufisadi wa aina yoyote? Si mbaguzi? Au nani anamfano wa watu wachache wazalendo wanaoweza kuongoza nchi yetu. Kwa maoni yangu naona hakuna mbadala katika kizazi cha sasa. Labda tuwaandae watoto wetu. Tukae kimya tujipange kwa miaka ijayo. Kwa sasa tukemee ufisadi. Nawakilisha!

ndgu yangu umeuliza swali zuri japo kidogo mtizamo wako nadhani si sawa. haiwezekani Tanzania nzima tukakosa watu wa kuongoza halafu hapo hapo unasema tuwaandae watoto wetu. . . kama wote wachafu nani amwandae nani? cha msingi Tanzania ya leo tumekosa kuwa wakweli, yaani tatizo linaonekana lakini watu wanalazimishwa kuamini hakuna tatizo. unafiki umejaa kwa wengi wa watendaji wa serikali na mkuu wa kaya ameshindwa kuwa na say kiasi kwamba hamna team work kila mtu anaamua anavyotaka! waziri mkuu anasema anapinga rushwa hapo hapo anachukua hatua ya kutetea watuhumiwa wa rushwa! what a double standard, a great sign of failure! tuna haja ya kubadilisha utaratibu kwa kweli, miiko ya uongozi pamoja na sheria ya rushwa ikitiwa nguvu, alafu tukaon waheshimiwa kadhaa wapo keko na segerea(achilia mbali maigizo ya kina mramba na liyumba) nadhani nchi itasimama tuu! nenda china utaona wala rushwa wanafanywa nini!
 
Sasa hivi unavuma upepo wa waraka, OIC na mahakama ya kadhi. Watu wamegeukia huko. Wanasahau mipango mingine. Unadhani tunakwenda au tupo palepale.

Kuna mchangiaji Mwanafalsafa kaonyesha tuwaondoe kwa voters, nimeipenda hiyo Falsafa. Suali nani wakureplace?

Labda nikuulize suali dogo tu. Ni nani kutoka upinzani aliyejitokeza mpaka sasa na kuhitaji kugombea urais ambaye tunamuani?
 
Back
Top Bottom