Moto ni chanzo cha mwanga ambacho kimetumika sana hasa katika historia ya binadamu. Kwa kawaida
moto una mchanganyiko wa vitu vingi, molekuli za hydrocarbon na oksijeni zinazoungua, kaboni daioksaidi na mvuke wa maji unaozalishwa kutokana na muungano huo, pamoja na uchafu kama masizi, moshi na mafuta ambayo hayajashika moto kikamilifu.
Mwanga wa njano ambao kwa kawaida tunauhusisha na moto, kwa kweli, hutengenezwa wakati vipande vidogo vya masizi vinapopata joto kali kiasi cha kuanza kung'aa. Mioto hii ya njano huitwa
luminous flames (mioto inayotoa mwanga), na masizi hayo yote ya ziada yanamaanisha kuwa moto huo haupati oksijeni ya kutosha kubadilisha mafuta yote kuwa kaboni daioksaidi.
Hata hivyo, mioto isiyotoa mwanga wa njano (
non-luminous flames) ina hali tofauti. Kwa sababu hii inapata oksijeni ya kutosha, huwaka kwa usafi zaidi (bila masizi) na ina joto kali zaidi. Pia, mioto hii huwaka kwa rangi ya bluu badala ya njano ya asili.
Je, Moto Una Kivuli?
Tovuti ya
Discover Magazine inaeleza kuwa kadiri moto unavyokuwa na uchafu mwingi unaoonekana kama masizi, au pengine nta ya mshumaa iliyogeuka kuwa hewa ndivyo uwezekano wa kuona kivuli chake unavyoongezeka.
Bila shaka, hata moto unaowaka kwa usafi una aina fulani ya kivuli. Hii kawaida huonekana kama mawimbi hafifu yanayocheza, na ni uwakilishi wa picha wa molekuli za gesi zenye joto kali sana zinazocheza ndani ya moto kwa sababu molekuli hizo zina joto kali kuliko hewa inayouzunguka moto, hupinda au kutanua mwanga (diffract).
Wapiga picha wanaweza kuitambua hali hii kama sayansi ileile inayoruhusu lenzi ya kamera kuelekeza mwanga sehemu moja.
Jaribu kumulika tochi dhaifu kwenye moto mkubwa, na kuna uwezekano mkubwa usione kivuli chochote. Ili moto (au chanzo chochote cha mwanga) utengeneze kivuli kinachoonekana kwa jicho la binadamu, ni lazima uwe unazuia chanzo cha mwanga ambacho ni king’avu zaidi yake kama vile mwanga wa jua.
Zingatia kwamba kivuli chochote si matokeo ya mwanga unaoingia kutawanywa na mwanga unaozalishwa na moto.
Moto unaweza kutoa kivuli ikiwa utazuia au kupindisha mwanga mwingine unaoupita, sawa na jinsi unavyoweza kuona kivuli cha mtu au mti. Hali hii inasababishwa na kuwepo kwa hewa ya joto kali na masizi (moshi mweusi) ndani ya ule mwali. Hewa hiyo ya moto hupindisha miale ya mwanga, na ndiyo maana wakati mwingine ukiangalia kivuli cha moto unachokiona ni mawimbi yanayocheza-cheza, kama yale unayoyaona barabarani kwenye lami wakati wa jua kali.
Ili uweze kuona kivuli hicho vizuri, unahitaji mwanga mwingine wenye nguvu zaidi kuliko ule wa moto wenyewe, kama vile mwanga wa jua la mchana. Kama ukiwasha tochi ndogo ya simu pembeni ya moto mkubwa wa kuni, huwezi kuona kivuli kwa sababu mwanga wa ule moto utafunika kila kitu. Kumbuka, kivuli hakitengenezwi na mwanga wa moto kupigana na mwanga wa jua, bali kinatengenezwa na kile kinachofanya moto uwake—yaani hewa ya moto na masizi.
Kwa ufupi, moto hautengenezi kivuli kama unavyoweza kufanya wewe au mimi kwa kuzuia mwanga wote usipite. Ili kuepuka hali ya moto kutokuwa na kivuli nyumbani kwako, hakikisha unamulika muale mkali wa mwanga au mwanga wa jua wa moja kwa moja kwenye moto wa njano wenye masizi au moshi mwingi.