mbalisana
Member
- Dec 15, 2011
- 46
- 42
Hivi inakuwaje binti ndo kwanza kamaliza chuo 26yrs,anaomba aolewe na mwanaume mwenye mke na watoto 2, kila siku anaahangaika kupiga simu mara nakupenda sana, nakumis sana,ukinioa namimi nitakuzalia watoto 2,huyo mkeo labda anatumia dawa lakini naamini unanipenda mimi zaidi kwakua tunatoka kijiji kimoja na ulikuwa na mimi kabla hujao.mimi ni mke wa huyo mwanaume, yawezekana bado wanaendelea wanapokutana, lakini najiuliza huyu binti hata kama ni upendo kweli yupo radhi kuharibu ndoa ya mtu mwingine hata kama kweli mume ndo anamfuatilia bado. Na huyu mwanaume kama bado alikuwa anampenda x-girlfriend kwa nini hakumuoa. nawashangaa sijui nianze nao vipi, maana nilimwambia mwanaume mawasiliano yao siyapendi naona ndo kwanza yanazidi.