Hivi ndivyo nilivyotapeliwa hapa JF kijinga

Hivi ndivyo nilivyotapeliwa hapa JF kijinga

Siku ya Jana kuna mdau hapa Jf Jina limenitoka kidogo alikuja na uzi wa kuuza bandle nafuu zijulikanazo kama supa bando.

Number yake ya simu ya mkononi ni 0620 434 183. SIMON MSUYA.

Dili lilikua nipewe GB 10 kwa Tshs6,000. Nikaona kwani 6k kitu gani ngoja nitume tu,.

Jamaa kanitumia link nidownload hiyo app ya super bando kwa maelezo nitumie opera mini ndio itafanya kazi.

Baba nimedownload kutumia power engines zote, sijui opra mini, Mozila fire fox, internet explorer, Chrome na zingine zote unazojua lakini app haikufanya kazi.

namrudia ananiambia nisubiri masaa manne nikajua nimeshaliwa.

Guys when the deal is tooo good think twice!!!!

Japo nilikua najaribu ila mwishowe nimejiona bwege
Mbona mimi kwangu imefanya kazi acha kulalama fuata maelkezo vizur
 
Elufu sita unapiga machine kabisa mtoto wa maana tabata poleee
 
Pole sana ila ndiyo umejifunza wakati mwingine utakuwa makini
Ila pia huenda umeepushwa huenda ungezitumia kuangalia porn maana zikiwa nyingi unakosa cha kuzifanyia
 
Daah mleta mada adi anajutia kuleta anakula mashuti ya uso tuu[emoji23][emoji23][emoji23]
Watu tunanunua GB 6 kwa 10000 wewe nani upate kwa 6000
 
Pole sana.
Watu wengi sio waaminifu tena akijua huwezi kumfanya chochote.
Na mtu ukiona hio hela ndogo unatuma tu haraka haraka kumbe mtu anakuwa anatapeli watu wengi sana na mwisho anakuwa na hela ya uhakika.
 
Kwanza nimpongeze kwa kuwa muwazi ,wako wengi humu yakishawakuta hawasemi wanaishia kuugulia tu maumivu na kujiona mafala flni hvi bila kujua makosa yao kama wangeyaleta mapema wengi wetu tusingetumbukia kwenye mitego hii ya utapeli.
Niulize tu vp wale wanafanya biashara ya kuuza bidhaa kule Instagram hasa vya kieletronics vp na wao wa kweli au nao ni mlemle
Niliuona ule uzi (thread) nakuna mtu alitoa angalizo watu wawe makini
 
ujanja ukizid unakuwa ni uboya, ndo kilichokukuta[emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom