Soma kwenye post ya Lemutuz akijinadi kuwa anamshukuru DC rafiki yake kwa kumpa usafiri. Use your common sense. Usijibu bila kwanza kuangalia chanzo cha habari.Sasa ni dhairi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro amefanikiwa Kwa asilimia Kubwa kuwavuruga baadhi ya viongozi wa chadema ambao wameonyesha wazi kumuwinda Kwa udi na uvumba katika kipindi Cha miezi minne aliyokaa Arumeru .
Katika kile kinachoonekana kuzagaa Kwa wingi katika mitandao ya kijamii ikionyesha picha ya Mwanaharakati wa masuala ya kijamii Ndugu Le Mutuz akiwa AMEPOZI nje ya Gari linalotumiwa na Mkuu wa Wilaya Arumeru katika Hotel ya kitalii ya Masai land iliyoko Arumeru ambapo viongozi kadhaa wa juu wa chadema ambao wameamua kusambaza picha hizo kwa makusudi wakidhani wanamchongea Dc Muro Kwa Mamalaka husika na badala yake wameanza kuonekana na wao wamekuwa wapiga debe wa kumuongezea Dc Muro umaarafu tu .
Niwasaidie kuwapa ufafanuzi kidogo tu
1. Hotel ya Masai land iko Arumeru eneo la kiutawala la Dc Muro ambapo alikwenda kuwatembelea marafiki zake ambao walikuja kumuunga mkono kwa kukuza utalii wa ndani Wilaya ya Arumeru , pia hotel ya Masai land Ndio walioshukia Timu ya soka ya Yanga .
2. Le mutuz amepiga picha akiwa nje ya gari hakuwa ndani ya gari uku bendera ikiwa inapepea, hivyo Le mutuz hakuwa anaitumia gari ya Mkuu wa Wilaya ikiwa ina bendera, pia kumbukeni Le Mutuz ni mtanzania ana haki ya kupiga picha katika gari ya serikali ambayo ni mali ya Umma.
3. Le mutuz anajulikana Kwa misimamo yake inayoambatana na majigambo ya kiwango Cha kimataifa, anaposema anashukuru Kwa kupewa usafiri hivi mnajua Alipewa usafiri gani kwani Dc Muro hana gari ya kumpa Le mutuz au mnatazama hiyo picha ya gari ya Serikali tu
Kweli Le mutuz kawavuruga akili , hivyo maneno ya Le mutuz yanabaki kuwa maneno yake ambayo hayawezi kuwa maoni ya Wilaya , Le mutuz ana haki ya kuandika na kujitamba kadri awezavyo, pasipo kuharibu mahusiano yake na Dc Muro
Kumbukeni vita ya Le mutuz na makada wa chadema , sasa wamemshindwa Le mutuz mwenyewe wameanza kupambana na Dc Muro