Hivi Msukuma halisi huwa anatokea wapi?

Mkuu naweza sema kwamba hayo maeneo ndiyo yalikaliwa na wasukuma mwanzon na kwa mda mrefu sana kumbuka walikua wanatoka upande wa maghalibi ng'weri na kuelekea mashariki ambapo walienda kukumbana na wamaasai na kuweza kupata mikikimikik hasa watoto wa kiume (hapa staliweka wazi sana ) lakin ushawahi fatilia kwenye maholelo ya kwetu chanzo cha kuwa wanapandwa na mizim na kuongea kimasai/ama kitaturu chanzo nin???

Kwain hifadhi ya maswa kwenye milima kuna nyumba nyingi za kale hata makaburi ya watu maalufu kama vile Nyendwa, Sita (huyu mpaka leo kuna nyumba ake na mabak ya ziz na ng'ombe wake waliobadilika na kuwa mawe na kisima chake na alisafir mpaka Butiama na alitabiri mpaka kuzaliwa kwa nyelele) mtemi wa mwisho wa meadu (ngwesa) .

Lakin pia fatilia story ya Ng'witulo gwa Ng'wawilyamu miaka ya 1950.
Kwa kifupi wasukuma wamegawanyika kuanzia zaman na hasa kufatana na utawala wao na hata maeneo yao na kuweza kuunda makundi yaliyopo mpaka sasa kama nilivyo yataja.

Na ikumbukwe kwamba kikwetu asili aridhi yote ni yawanawake na ndio walikua watawala japo kulingana na wakati walikua wanapinduliwa na waume zao .

Lakin ti kwa hekima mpaka leo tunawaanzi hao watawala wa mwanzo kwa salam japo sku izi watu hawajui ata maana ya hizo hekima za salam (lwimbo) na kwa hawa watawala kunawaliokuwa na maeneo makubwa sana na wanaonekana kuwanaidadi kubwa ya watu kama vile MINZA,( wanatumia EMINZA), Wengine ni akina.

NKWAYA,SEGA,NKWIMBA,SABHE,NG'WASHI,n.k
Na kuna hawa wanasalimiwa NG'WAKADILU walifata kwa huyu mama KADILU hakuwa mtemi na alizaliwa tu kwa kufata jua na asubuhi na alipaya pia wa kumuunzi kwa salam
Big up mkuu
 
Kwa uzoefu wangu bhanyantuzu ndo jamii ya wasukuma ambayo ina elements za ubaguzi.
 
Lakini kumbuka wanyantunzu ni mchanganyiko wa wasukuma na wanyiramba, ndio maana hata baadhi ya majina wanachangia, kama Mangu mnyantunzu oia Mangu mnyiramba.@Kungu Kayuki,
 
Tawala za wasukuma kabla na wakati wa ukoloni zilikuwa 52. Mwenyekiti wa machifu wa mwisho wa wasukuma hadi Tanganyika inapata uhuru aliitwa Mtemi Majebele wa Mwagala. Kabla ya huyo Mwenyekiti alikuwa Makwaya wa Busia. Hilo ndilo eneo amblo wakoloni waliliita Sukumaland. Kwa sasa eneo hilo ni mkoa wa Mwanza isipokuwa wilaya ya ukerewe, mkoa wote wa Simiyu, mkoa wa Shinyanga isipokuwa wilaya ya Kahama na mkoa wa Geita isipokuwa wilaya za Bukombe, Mbogwe na Chato.
Mkuu kwa kawaida tu head state ya Wasukuma wote ipo USUKUMA Mwanza na hata zile shelehe na bhulabho zilikua zinafanyikia mara nyingi maeneo yale na huko ndiko mtemi wa kabila lote aliteuliwa japo anaweza kutoka sehem yeyote wasasa sijajua ametokea eneo gan japo wamwisho mie kumfahamu alikua Majebhele toka Busia.
 
Usipotoshe watu. Sengerema ilikuwa wilaya ya Geita hadi mwaka 1976 ilipofanywa nayo kuwa wilaya. Aidha, Geita ilianza kuwa wikaya mwaka 1950 kabla ya hapo Geita na sengerema zilikuwa wilaya ya Mwanza siyo kwimba kama unavyopotosha wasomaji.
Wasukuma original ile OG wanapatikana Kwimba, hii wilaya imezaa wilaya za Magu, Missungwi na Sengerema na imebaki kuubwa tuu. Huko ndiyo Wasukuma OG tunatokea.
 
Nani kakwambia wazinza,wasumbwa,wakonongo ni Wassukuma? Kwa huku kwetu tuna Bhanantunzu,bhadakama(wanyamwezi), Bhanang'wagala, Bhasumabhu na Bhanabhulima ndio hao wanaform kabila la WASUKUMA ambapo kuna wengine huwagawa kwa pande kuu nne za dunia.

Na kwa nyongeza tu hatujawahi kubaguana hata siku moja siye tukikutana na kujuana tunaanza na kubonga kikwetu iwe ndan ama nje ya mikoa tunayopatikana kwa wingi .
Umeandika sahihi kabisa Nyanda subi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wyatt Mathewson, Ukiona wengi wapo against nawe jitahidi kusoma kipi kipya wanaweza kukuongezea mfano usichoelewa kuhusu ni kuwa Ethiopia haikukaliwa na jamii na hii inathibishwa na location yake ambapo magharibi kulikuwa na mchanganyiko wa wabantu & waarabu Masharik wasomalis kusini wabantu & Nilotes kaskazini waarabu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom