Marco Polo
JF-Expert Member
- Jan 16, 2014
- 13,346
- 21,244
Captain kazi yake sio kumuongoza refarii Bali kuongoza wachezaji wenzake uwanjani refa anaongozwa na Sheria za Fifa wewe wa wapi?Yaani kapten ubishane na kumshawishi refa kwa ishara? Umezoea kuangalia azam. Anza kuangalia EPL au Lalila utaelewa
Na ndio maana wazungu wamekuja na VAR hata refa akiweka kati VAR ikiona Kuna sheria imevunjwa ktka mchakato wa goli refa ataitwa bila hata wachezaji kuingilia kati kumbuka goli la pili la wale Stellaboch Simba walikuwa washakubali yaishe na mpira ulishawekwa kati wakashangaa refarii haanzishi mpira kumbe watu wa VAR walikuwa washamshtua kitambo, na hata kama captain alitakiwa kuongea na refa si unakunja tu mikono hivi kumuonyesha refa aende kwenye VAR japo na yenyewe anaweza kukataa pia.