Hivi mnaiona hii Speed ya MeTL kwenye soko?

mandella

JF-Expert Member
Oct 29, 2011
3,048
3,227
Habari.

Kwa ufupi kabisa niseme tu binafsi nilifika Dsm miaka 6 nyuma nilizikuta na kuzifahamu products kutoka kwa Barharesa almaarufu Azam tu, huku Mo akiwa anatetea taaratibu,ila kwa sasa naweza sema speed ya Mohamed Enterprise ni ya kasi ya ajabu.

Sasa naona mapinduzi makubwa ya bidhaa za MeTL sokoni, aisee kalishika soko kisawasawa tena rapidly sana , bidhaa za Azam zinaonyesha kuporomoka kimauzo taaratibu.
Si kwa bidhaa hizi za vinywaji na vyakula tu , jamaa sasa kaenda mpaka kwenye Friji,na Vifaa vingine vya majumbani.
Ukipita pita mijini huko Ukipepesa huko na huko lazima utakutana na neno MO ama MeTL.

My take
Yapo mengi ya kujifunza katika ushindani wa soko kutoka kwa huyu mtu.

NB: Sijamtumia Bakhresa kwa maana mbaya(anaweza pia kujitafakari kutokana na maoni ya wateja wake tunavyoona kudhibiti ushindani huu), bali nimemtumia kama Refference ya Mshindani mkubwa kibiashara zidi ya Mo..

Hongera sana Mo..
 
Sasa naona mapinduzi makubwa ya bidhaa za MeTL sokoni, aisee kalishika soko kisawasawa tena rapidly sana , bidhaa za Azam zinaonyesha kuporomoka kimauzo taaratibu.
Si kwa bidhaa hizi za vinywaji na vyakula tu , jamaa sasa kaenda mpaka kwenye Friji,na Vifaa vingine vya majumbani.
Ukipita pita mijini huko Ukipepesa huko na huko lazima utakutana na neno MO ama MeTL.


Huyo MO si ndiye alikuwa na kashfa ya mchele mbovu miaka kadhaa iliyopita!!
Kuto shine kwa Azam kunakuuma nini, andiko lako limekaa ki promotion zaidi
 
Uko sahii kabisa jana mchana nilikuwa na ubao nikapita uswahilini kununua mihogo ni kadaka na kisoda cha MO kile cha jero nishushie duh!!!yaani chemiko unaisikua kabisa mdomini na inaacha na rangi kwenye mdomo.
mo najua upo jf tunaomba punguza sukari kali kwenywe vinywaji vyako vibaki na uhalisia kama juic za azam...
 
hayo ma mo cola,azam cola,mo embe,n.k mi sijawahi kabisa kuwaza kama ntakunywa mmeshikwa nyinyi tu na poleni sana
 
shida ni kwamba board yetu ya viwango hawana utaalam sana huwa wanasubiri mpaka waone madhara ndo watoe tangazo kuwa bidhaa x haifai kwa matumizi ya binadamu wakat huo wewe ushaji dose concentration ya kutosha
 
Hua nawasikia sana watu wakijaribu kulinganisha utajiri wa Mo na Sheikh Bakhressa, watu wanasema Bakhressa kamwacha mbali sama Mo. Nakaa nacheka tu.

Huyu jamaa nilikutana nae mwaka jana ofisini kwake pale Golden Jubilee Tower, aisee huyu Mo ni kichwa, tena kichwa cha motooo. Kila anachozongumza kinarelate 1 kwa 1 na biashara. Tofauti na sisi ambao muda wote tuko kwenye simu, nilivyokua nae alitumia calculator mara nyingi zaidi ya simu.

Huyu Mo ana MBA ya Georgetown University, na alikuwa president of students' Organization (tena mwafrika wa kwanza kushika hiyo nafasi pale Georgetown). Hii inaonesha jinsi gani jamaa alivyo smart. Nakumbuka kwenye interview yake 1 na CNBC alisema yeye ndio largest producer na trader wa sisal duniani. Yani sisal anayoproduce kwa siku anaweza kuizungusha na ikafunika dunia mara 3 hivi.

Dewji kwa E. Africa yeye ndio trader mkubwa zaidi wa commodities in and out. Huyu jamaa ananunua korosho huko Mtwara kwa $1 kwa kilo then bei ya korosho ktk global market ni $12, ona hapa anavyopiga pesa ya wazi - na huko wamakonde msimu wa korosho niliwakuta wameneeka haswa, watu wamegonga mamilioni kwenye mashamba ya Korosho, TPDC walikua wanawanyenyekea vibarua wa kuchimba mifereji ya bomba la gesi, maana watu walikua na pesa ya korosho huwezi kuwa convince kufanya vibarua kwa ujira wa buku 3 kwa metre 1.

Ana export peagon peas, mbaazi, choroko, ufuta, mtama, nk kwa tones kwa tones... Huyu jamaa alinunua viwanda vingi sana vya serikali ambavyo vilishaanza kufa, akauziwa kwa bei ya dagaa, karenovate saivi anazalisha karibia kila kitu, sabuni, viberiti, chumvi, baking powders, karibu kila kitu.

Kiufupi huyu Mo yuko very smart, kazaliwa anamuona baba'ke mzee Gulam Dewji anafanya biashara, kakulia kwenye biashara, kaenda best schools hapa duniani kusomea biashara. Yani hafanyi vitu kwa mazoea, anafanya vitu kwa modern trend, na yeye ndio anaintroduce hizo modern trends hapa Bongo, so rivals wake kina Zacharia, Bakhressa wote wanakua wanacheza ngoma yake.

Kuna watu wanasema jamaa ni kwamba alikuta tyr home kuna utajiri so yeye akaendeleza... ukweli ni huu - Dewji alikuwa wall street ndio Mzee wake akamuomba arudi Bongo kurun business, mzee alishaona kazidiwa vby na kina Bakhressa, wakati huo MeTL ina utajiri wa $30 mil. Sasa huyu kichaa akapewa rungu. Ndani ya miaka 11 akabadilisha $30 mil kuwa $1.1 bil. Kitu ambacho hakuna Mwafrika anaweza kukifanya, labda tu Dewji aanze upya. Nakumbuka Dangote alikopeshwa pesa na mjomba ake (ambae alikua the richest man in W. Africa back then) pesa hiyo kwa kipindi hiko ingeweza kununua luxury Mercedes Benz 550... lkn ilimchukua dangote miaka 30 kukamata $1 bilioni - tofauti na Mo ambae ilimchukua decade 1 tu.

This boy is a Beast!!
 
Hua nawasikia sana watu wakijaribu kulinganisha utajiri wa Mo na Sheikh Bakhressa, watu wanasema Bakhressa kamwacha mbali sama Mo. Nakaa nacheka tu.

Huyu jamaa nilikutana nae mwaka jana ofisini kwake pale Golden Jubilee Tower, aisee huyu Mo ni kichwa, tena kichwa cha motooo. Kila anachozongumza kinarelate 1 kwa 1 na biashara. Tofauti na sisi ambao muda wote tuko kwenye simu, nilivyokua nae alitumia calculator mara nyingi zaidi ya simu.

Huyu Mo ana MBA ya Georgetown University, na alikuwa president of students' Organization (tena mwafrika wa kwanza kushika hiyo nafasi pale Georgetown). Hii inaonesha jinsi gani jamaa alivyo smart. Nakumbuka kwenye interview yake 1 na CNBC alisema yeye ndio largest producer na trader wa sisal duniani. Yani sisal anayoproduce kwa siku anaweza kuizungusha na ikafunika dunia mara 3 hivi.

Dewji kwa E. Africa yeye ndio trader mkubwa zaidi wa commodities in and out. Huyu jamaa ananunua korosho huko Mtwara kwa $1 kwa kilo then bei ya korosho ktk global market ni $12, ona hapa anavyopiga pesa ya wazi - na huko wamakonde msimu wa korosho niliwakuta wameneeka haswa, watu wamegonga mamilioni kwenye mashamba ya Korosho, TPDC walikua wanawanyenyekea vibarua wa kuchimba mifereji ya bomba la gesi, maana watu walikua na pesa ya korosho huwezi kuwa convince kufanya vibarua kwa ujira wa buku 3 kwa metre 1.

Ana export peagon peas, mbaazi, choroko, ufuta, mtama, nk kwa tones kwa tones... Huyu jamaa alinunua viwanda vingi sana vya serikali ambavyo vilishaanza kufa, akauziwa kwa bei ya dagaa, karenovate saivi anazalisha karibia kila kitu, sabuni, viberiti, chumvi, baking powders, karibu kila kitu.

Kiufupi huyu Mo yuko very smart, kazaliwa anamuona baba'ke mzee Gulam Dewji anafanya biashara, kakulia kwenye biashara, kaenda best schools hapa duniani kusomea biashara. Yani hafanyi vitu kwa mazoea, anafanya vitu kwa modern trend, na yeye ndio anaintroduce hizo modern trends hapa Bongo, so rivals wake kina Zacharia, Bakhressa wote wanakua wanacheza ngoma yake.

Kuna watu wanasema jamaa ni kwamba alikuta tyr home kuna utajiri so yeye akaendeleza... ukweli ni huu - Dewji alikuwa wall street ndio Mzee wake akamuomba arudi Bongo kurun business, mzee alishaona kazidiwa vby na kina Bakhressa, wakati huo MeTL ina utajiri wa $30 mil. Sasa huyu kichaa akapewa rungu. Ndani ya miaka 11 akabadilisha $30 mil kuwa $1.1 bil. Kitu ambacho hakuna Mwafrika anaweza kukifanya, labda tu Dewji aanze upya. Nakumbuka Dangote alikopeshwa pesa na mjomba ake (ambae alikua the richest man in W. Africa back then) pesa hiyo kwa kipindi hiko ingeweza kununua luxury Mercedes Benz 550... lkn ilimchukua dangote miaka 30 kukamata $1 bilioni - tofauti na Mo ambae ilimchukua decade 1 tu.

This boy is a Beast!!
Mkuu umeanza vizur ila umekuja kumalizia vibaya,hizo modern trends si kwa vinywaji vyake,na ulipomfananisha na bakhresa ndo umeharibu kabisa,modern trend kwenye MO passion?? Azam bado wako juu kwenye vinywaji..
___Leroy
 
Mo anafanya vizuri. Uchunguzi wangu unaomyesha retailer wengi wanapendelea Mo products (hasa maji na soft drinks) kwakuwa zinauzika zaidi. Azam walikuwa wameshika soko miaka 2 nyuma sijui tatizo ni nini? Nahisi kama kuwa na azam tv/decoder kumewapotezea focus kwenye products? Kiufupi inabidi wajipange upya.
 
Mkuu umeanza vizur ila umekuja kumalizia vibaya,hizo modern trends si kwa vinywaji vyake,na ulipomfananisha na bakhresa ndo umeharibu kabisa,modern trend kwenye MO passion?? Azam bado wako juu kwenye vinywaji..
___Leroy
Boss unaongea nini?!
Wewe unasema Bakhressa anakimbiza mwenzio anatama hata Mo afe kesho. Ingia mtaani uone kama kuna maji ya Uhai kama zamani, Ukigeuka kushoto unakutana na Maisha, ukigeuka kulia unakutana na Masafi. Hivi tuseme ukweli kati ya Mo energy na Azam energy ni ipi makopo yake yametapakaa mtaani. Yani huyu jamaa ana mavinywaji mengi hata ukumbuki majina.

Angalia mashamba aliyonayo Dewji mashamba ya Chai, Kahawa, Palm oil, korosho karibia hekari mil 2 kwa ujumla... utamfananisha na kina Bakhressa?! Dewji mwenyewe anakwambia by 2018, yani mwakani anataka ashike $5 bil.

Usione Vodacom ipo hewani na inasimamia ukucha, Dewju ana mkono wake pale, umewahi kusikia Zefona Cellines - hiyo ni mali ya Dewji. Dewji anatoa financial services kupitia ile kampuni yake ya Mo Assurance mabenki kibao, mwaka jana mwanzoni kama sichanganyi Mo alikua na plans za kununua Barclays Bank Africa. Unaijua kampuni inaitwa Genrich, inahusika na usafirishaji... boss acha kumlinganisha Mo na wazee wetu wa zmn ambao tunawaheshimu sana.

Unafahamu kuwa Dewji ana kampuni ya Real estate kubwa sana, anamiliki properties ambazo zinaweza kumchukua Bakhressa miaka 20 kua nazo kutoka leo. Khaki complex ni mali ya Dewji, JV complex ni mali yake, kule Kigamboni kadaka Plot ya kufa mtu - tusubiri mavitu atakayoshusha hapo, yeye anakwambia anajenga 5 star hotel hadi Serena wataomba Poo, pia kuna makazi ya mid class people anajenga Mbezi na Kitunda km sikosei...

Katika vitu ambavyo namheshi Bakhressa ni Azam Tv... Hapa alijua kumnyoosha Dewji, lkn Dewji ndio Baba la capitalism, ngoja aibuke na maving'amuzi ya 6000 kwa mwezi.

Boss huyu jamaa achana nae tu.
 
Mo anafanya vizuri. Uchunguzi wangu unaomyesha retailer wengi wanapendelea Mo products (hasa maji na soft drinks) kwakuwa zinauzika zaidi. Azam walikuwa wameshika soko miaka 2 nyuma sijui tatizo ni nini? Nahisi kama kuwa na azam tv/decoder kumewapotezea focus kwenye products? Kiufupi inabidi wajipange upya.
Sidhani, TV na decorder wanadeal wengine, unga wengine, vinywaji wengine, Kuna divisions mbalimbali.

Biashara Ni ushindani, mwenzio anaangalia SWOT zako anazitumia kukupiku. Mo Ni Mjanja mno.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom