Mbinu waliotumia kampuni ya Avis kutawala soko la magari ya kukodisha Marekani

Seif Mselem

JF-Expert Member
Oct 16, 2023
257
441
…miaka ya Nyuma nchini Marekani…

Kulikuwa na ushindani Mkali sana kwenye Soko La…

“Magari ya Kukodisha”

(Rental Cars)

Na…

Moja ya Kampuni ililokuwa Inatawala Soko hilo ilikuwa ni Kampuni ya…

“HERTZ”

Hawa ndio walikuwa Watawala wa hilo Soko kwa kipindi Kile!

Na…

Kama unavyojua Panapokuwa na…

UBER basi… BOLT nae huwa Hakosekani!

Na…

Panapokuwa na…

ABOOD basi.. BM nae huwa Hakosekani!

Kwahiyo…

Hata huko kwao Ilikuwa hivyo…

Yaani Avis na wao walitaka kuingia kwenye Soko la Kukodisha Magari ambalo Lilikuwa chini ya utawala wa hawa…Hertz!

Na…

Hapa Avis waliangaika sana kwa kutafuta Njia ya…Kutawala soko hilo lililokuwa na Ushindani mkali…

Walijaribu njia mbalimbali za Kutawala Soko bila kushindana ILA kwa bahati mbaya zote Zilibuma!

Wakaona isiwe kesi… Wakaamua kuanza kushindana na Mpinzani wao Hertz!

Unajua Nini Kilitokea?..

Walipata hasara kubwa sana kuwahi kupata…Hadi kupelekea Kampuni kutaka Kufungwa…

Kwasababu… Pesa zote walizowekeza kwenye Matangazo hazikurudi!

Kwa kifupi… Walipata HASARA Kubwa Mno!

Na…

Kupoteza kabisa Nafasi yao Sokoni.

Wakiwa wamepoteza Matumaini kabisa…Avis chini ya CEO wake makini Mr…

“Warren Avis”

Walikuja na MBINU Mpya ya kuja Kujiweka kwa mara Ingine soko…

Walikuja na mbinu Inaitwa…

“AGAINST Positining”

Ambayo ndio Iliwafanya waweze Kutengeneza zaidi ya US Dollar 5M na Kutambulika kwenye Soko la Magari ya Kukodisha hadi leo hii.

Unaweza Kujiuliza Sasa Mselem… “Against Positioning” ni nini?

Okay Ondoa Shaka… Nimekuwekea Maelezo yake Hapa Chini…

Ukweli ni kwamba…

Kwenye biashara nafasi ya Mshindani wako Sokoni ni… Muhimu kama Ilivyo nafasi ya Biashara yako.

Na…

Akili ya binadamu (Mteja) huwa haina Nafasi ya kitu KIPYA na cha TOFAUTI Isipokuwa kinahusiana na Kitu cha Zamani.

Najua utakuwa Unajiuliza Leo Mselem anaongea nini huyu…

Ondoa hofu Kabisa… Utanielewa taratibu…

Angalia Hapa…

Kwenye biashara kuna kitu huwa Kinaitwa…

“Product Ladder”

(Ngazi ya Bidhaa)

Yaani…

Wateja huwa wana Tabia ya kuzipanga bidhaa zinazofanana kwenye Madaraja…

Mfano…

Ukiangalia kwenye Akili ya mteja jinsi Soko la ma Busi lilivyo hapa Morogoro…

Utakuta…

Namba 1 ni… Abood

Namba 2 ni… BM Coach

Namba 3 ni… Al Saedy

Yaani… Bidhaa za kufanana kwenye Akili ya Mteja zinajipanga kwenye Mtindo wa Ngazi.

Maana yake ni kwamba… Kila bidhaa huwa Imepangwa kwa Mtindo flani kwenye Kichwa cha Mteja.

Na…

Hii ipo kwenye kila Aina ya bidhaa/huduma Unayotoa!

Kwahiyo…

Ukitaka kufanya “POSITIONING” kwenye Soko unaloingia… Huwa hatuingii kwa kushinda na watu walioko juu ya Ngazi…

Bali huwa tunaingia kwa Kufanya aina hii ya Positioning Inayoitwa…

“Against Positining”

Yaani…

Badala ya kushindana na Giant aliyopo Sokoni kama alivyofanya Avis mara ya kwanza… Wewe unajifananisha na Giant…

Kivipi Sasa?..

Angalia Hapa…

Kwasababu…

Tayari Abood kishakuwa wa Kwanza kwenye Soko la ma Busi… Wewe Unaingia kwa kuwa wa Kwanza kwenye Nafasi ya “PILI” kwenye Aklili ya Mteja wako.

Kwasababu…

Kwenye kila Kipande cha NGAZI kilichopo Kichwani kwa Mteja wako kuna “Brand Name” ya Mshindani wako…

Na…

Kwasababu… Tayari mshindani wako Kashika nafasi ya Kwanza wewe Unaenda kuiwahi nafasi ya Pili kwenye Akili ya Mteja wako

Na…

Sio kushindana na Mshindani wako kama wengi Wanavyodhani… bali ni kwa Kujifananisha na Mshindani wako

Kwasababu kama kutumia Nguvu ya Kushinda ili kuingia Sokoni ingekuwa ndio Strategy basi…

Chama cha Upande wa Pili… Kingeshachukua Utawala!

Kwahiyo…

Ujanja hapa ni kutumia “Against Positining” na Kuiwahi nafasi ya 2 kwenye Akili ya Mteja wako!

Na…

Alichokifanya Avis kwa… Hertz

Ndicho Kilichofanywa na…

Burger King kwenye… Fast Food!

Ndicho Kilichofanywa na…

Pepsi kwenye… Cola Drinks!

Kwahiyo…

“It’s Not About Competing… It’s About Positioning”

Uwe na Siku Njema

Gracias…

P.S: Nambie Unafikiria nini Juu ya Mbinu hii ya Ushindani kwenye Biashara (Nasoma na Kuji Comments)!

Seif Mselem
avis-ofis.jpg
 
You can see unatumia sana hizo nukta mdokezo, alafu unaweka mahali ambapo hakuna ulazima was kuweka kwa mfano;
Kwasababu ......
Kwahiyo.........
Na....
Try to fix these, Maana unaitumia kwa Kila makali. Inaweza kuwa sio mbaya kama umeamua uwe mtindo wako
Just advice and critiques.
Regards
Thanks Brother Rapha... I'm Just trying to Increase READABILITY!
 
Against position, kaka atujashiba madini. Ila Kama nimekuelewa unasema MTU akiwa smart zaidi yako mfanye awe rafiki yako ikishindikana urafiki Basi asiwe adui yako.
 
Back
Top Bottom