Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,679
- 218,188
Ikiwa kama Paulo Makonda ametenda unyama uliotajwa na Serikali ya Marekani na ambao umepelekea kudhalilisha nchi yetu kuliko ilivyowahi kudhalilishwa tangu Mungu aumbe mbingu na ardhi, nina swali dogo sana la kuuliza.
Je alipokuwa anatenda uhalifu huo viongozi wakuu wa nchi hii akiwemo Rais, Makamu wake na Waziri Mkuu hawakujua ? Je viongozi wa idara za Usalama wa Nchi nao hawakujua? ikiwa kama raia ambaye hakuwahi hata kuhudhuria mafunzo hata ya JKT au Mgambo anaweza kutenda mambo mabaya kiasi hiki na vyombo vya usalama vikashindwa kumuona hadi waone wazungu basi nchi yetu inahitaji huruma ya Mungu.
Vinginevyo Serikali ya Tanzania ikanushe jambo hili na kuitangaza Marekani kama Taifa la waongo wakubwa ili dunia ituelewe
Hhaiwezekani jambo kubwa la kudhalilisha nchi kama hili likapita bila kujadiliwa, hatulengi kutukana wala kuhatarisha chochote, hii ni kwa sababu kilichotajwa kufanywa na Makonda ndio cha hatari zaidi kwa Taifa letu kuliko kuhoji
Naomba kuwasilisha
Je alipokuwa anatenda uhalifu huo viongozi wakuu wa nchi hii akiwemo Rais, Makamu wake na Waziri Mkuu hawakujua ? Je viongozi wa idara za Usalama wa Nchi nao hawakujua? ikiwa kama raia ambaye hakuwahi hata kuhudhuria mafunzo hata ya JKT au Mgambo anaweza kutenda mambo mabaya kiasi hiki na vyombo vya usalama vikashindwa kumuona hadi waone wazungu basi nchi yetu inahitaji huruma ya Mungu.
Vinginevyo Serikali ya Tanzania ikanushe jambo hili na kuitangaza Marekani kama Taifa la waongo wakubwa ili dunia ituelewe
Hhaiwezekani jambo kubwa la kudhalilisha nchi kama hili likapita bila kujadiliwa, hatulengi kutukana wala kuhatarisha chochote, hii ni kwa sababu kilichotajwa kufanywa na Makonda ndio cha hatari zaidi kwa Taifa letu kuliko kuhoji
Naomba kuwasilisha