Hivi Lissu ana dini kweli?

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu amewashangaza Watanzania kuhoji uwezo wa Mungu katika uponyaji wa janga la corona nchini.
Kauli hiyo ya Lissu pia imeenda mbali zaidi alipowashangaa Waislamu na Wakristo kwenda kanisani na misikitini kuombea corona huku akiwaita ni wajinga.
Lissu ametoa kauli hizo tata zinazozidi kutoa tafakari ya afya yake ya akili akihojiwa na Radio Maisha ambapo amesema Mungu kwamba hawezi kuponya magonjwa na ana muda wa kuhangaika na wajinga.
“Kama alivyosema rais mwenyewe hii kitu dawa yake ni kwenda msikitini na makanisani kuomba Mungu, katika karne ya 21 rais anayesema ana PHD katika Kemia kuamini kwenye mambo kwamba unaweza kutibu ugonjwa kwa maombi ya Mungu,” amesema Lissu.
Mtangazaji wa kipindi hicho alimuuliza Lissu; “Kwa hiyo hujapendezwa kabisa kwa namna rais anavyoshughulika na hii ishu ya covid19 pale nchini?”
Lissu akajibu: “Mungu ana mambo mengi sana hana muda wa kuhangaika na wajinga.”
Kauli hii ya Lissu inaacha maswali kwamba je; ana dini? Kama kweli angekuwa na dini basi angekuwa na hofu ya Mungu.
Lissu anasahau kama ni Mungu amemponya na kumfikisha hapo alipo leo badala yake alianza kutukana watu kama vile haitoshi amehamia kwa muumba na watumishi wa wake.View attachment 1611348
Hivi wewe nguchiro wale wote waliokufa Italy, Spain, Marekani, China, etc etc Mungu hawapendi? kwa nini mnakufur. Lisu kasema kweli Mungu haangaiki na wajinga

jisaidie mwenyewe kwanza Mungu atakusaidia.
 
Hivi wewe nguchiro wale wote waliokufa Italy, Spain, Marekani, China, etc etc Mungu hawapendi? kwa nini mnakufur. Lisu kasema kweli Mungu haangaiki na wajinga

jisaidie mwenyewe kwanza Mungu atakusaidia.
Maana ya ujinga ni NECCCM Tumeccm Polisiccm kuidhoofisha kuihujumu chadema, maana ingine ya ujinga ni ile Tabia ya hovyo ya CCM kuwabambikia kesi kuwapiga risasi wapinzani
 
Binafsi sina tabu na imani ya Lissu kuwa hata kama haamini Mungu kabisa,ila kwa haya maelezo yake inaonesha si mtu kuamini sana kwa Mungu kama kweli anaamini na pengine ndio maana sio mtu wa kumtaja sana Mungu.

Na wale mnaomsemea Lissu kuwa Mungu kumuepusha na kifo au sijui kapona lile shambulizi kwa msaada wa Mungu,ni kwamba muache kumsemea maana mwenyewe imani ya kuponywa na Mungu.

Anachoamini Lissu kimemfanya kuwa hai katika lile shambulizi ni hiki hapa.
 
Huyo jamaa hata ukiangalia tu wajihi wake unakuja na conclusion kuwa kuna nati imelegea kichwani.
 
Sasa mbona yeye Lissu hatumuoni kuvaa mask na anashikana mikono na watu hovyo tu kwa kifupi hana hofu na corona,sasa ushamuuliza huo ujasili wa kutofuata taratibu za kujikinga na corona anaupata wapi wakati hapo Kenya watu wanaumwa?
Ndugu suala la Corona ...Tanzania, kuvaa mask, sijui Nini... tusimkufuru Mungu, Kama katuponya Basi ashukuriwe .... Ila binafsi naogopa Corona!

Kuhusu Lissu kuvaa au kutovaa Hilo anajua yeye!

Ila uhalisia kuwa Kama Mungu ametuondokea Corona... Basi uitishwe upimaji nchi mzima tujiridhishe!

Pili, hivi hizi nchi nyingine Hazina Mungu!😲😲
 
Never discuss things that are beyond your capacity

Below cartoons and cat show how your brain is limited

You can not prove things that are beyond your Brain

Maendeleo ya teknolojia ndio yanayofanya baadhi ya mambo ya kidini na kiimani watu kuyaacha

Leo unatumia I Pad au Simu smart kudownload vitu

Lakini Nabii Musa alizidownload enzi hizo

View attachment 1611351View attachment 1611352View attachment 1611353View attachment 1611354
Kuna mtu aliwahi niambia Mungu ndiye mwanasayansi wa kwanza,

Mfano mdogo tu ni namna ile sadaka ya Eliya ilivyoteketezwa kwa moto wakati sadaka ili miminiwa maji,

Akadai nguvu za aina ile ni za kinyuklia , hehe kuna mambo unaweza sema ni kamba ila ni vitu vilivyo juu ya uwezo wa kawaida wa kifikiri.
 
Aisee, hili asingeliongelea,
Imani na siasa vyote vina frequency sawa,
Asicheze na maisha ya imani
 
Kura za ubunge na uraisi zitasafirishwa kwenda kuhesabiwa jimboni, hazitahesabiwa kwenye vituo vya kupigia kura

Kura za udiwani zitasafirishwa kwenda kuhesabiwa makao makuu ya kata (katani)

Wapinzani hampati kitu.

Kuweni makini


Trust none
Hata wewe mwenyewe
 
Ndugu suala la Corona ...Tanzania ,kuvaa mask,sijui Nini...tusimkufuru Mungu, Kama katuponya Basi ashukuriwe ....Ila binafsi naogopa Corona!
Kuhusu Lissu kuvaa au kutovaa Hilo anajua yeye!
Ila uhalisia kuwa Kama Mungu ametuondokea Corona...Basi uitishwe upimaji nchi mzima tujiridhishe!
Pili ,hivi hizi nchi nyingine Hazina Mungu!
Sasa tupime ili kujua athari za Corona Tz au tupime tu ili tujue ni kiasi gani cha watu Tz wana hivyo virusi ila wanaendelea na shughuli zao bila kuuguwa?

Kwa sababu tulikuwa na watu ambao walikuwa wanasema Tz watu wanakufa kimya kimya kwa corona kwamba hali ni mbaya ila serikali inaficha, ila sasa hao watu tunaona hawafuati taratibu za kujikinga na corona wamejichanganya kama wengine wenye kuamini Tz hakuna corona.
 
Akili kichwani! Mtu anaombea kitu hakionekani halafu alishindwa kuweka ulinzi maeneo ya wanayoishi wabunge, hata kuzuia shambulio na pia hata baada ya shambulio ameshindwa kuwatia nguvuni waliojaribu kufanya jaribio la mauaji yapata miaka mitatu sasa!

Ana Mungu huyo au umuhimu wa dini uko wapi hapo? Tafakari hayo
 
Ni ujinga wa hali ya juu kusema imendoka Tanzania kwa sababu ya kusali. Na ni ujinga wa hali ya juu kufikiri Mungu anaweza kuchezewa na mtu mwenye tuhuma za mauaji kama Magufuli.
Hivi Magufuli ana dini kweli? Hebu aeleze kuhusu jaribio la kumuua Lissu kwa risasi! Mwenye dini aweza kufanya hivyo? Kuwepo au kutokuwepo Covid19 Tz hakuna uhusiano wowote na Magufuli.
 
Never discuss things that are beyond your capacity

Below cartoons and cat show how your brain is limited

You can not prove things that are beyond your Brain

Maendeleo ya teknolojia ndio yanayofanya baadhi ya mambo ya kidini na kiimani watu kuyaacha

Leo unatumia I Pad au Simu smart kudownload vitu

Lakini Nabii Musa alizidownload enzi hizo

View attachment 1611351View attachment 1611352View attachment 1611353View attachment 1611354
Wewe Brain yako ndiyo iko Blind kabisa.

Kama wewe huamini Mungu basi usifanye watu wote wawe kama wewe, ilikuwa haina haja ya Lissu kupinga suala la imani ya watu moja kwa moja hata kama ni kweli.

Wasomi wengi na wadadisi wa mambo tunajua kuwa kuwepo kwa Mungu kunathibitika katika nadharia tu na nadharia hizo huwa zina weakness zake ndiyo maana sayansi inaziona kama nadharia za miyeyusho, lakini sasa lissu hakupaswa kwenda kuongea kitu kama kile kwa watanzania wenye imani zao maana wenye imani zao watakuona kweli labda ushapata mental defect baada ya kushambuliwa kwa risasi.
 
Back
Top Bottom