UHURU JR
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 17,463
- 8,750
Nikueleze mara ngapi kuwa haiwezekani kuprove negative?
Nimekupa mfano wa watu wawili kwenye chumba kisicho na kitu halafu kati ya hao watu wawili mmoja akadai ndani ya hicho chumba kuna kiti. Mwenzake akakanusha kwa kusema hakuna hicho kiti. Je hapa jukumu la kuthibitisha kuwa kiti kipo ndani ya hicho chumba ni nani?
Wewe inaonyesha huelewi logic ndiyo maana unarudia jambo nalokuambia.
Mimi nitaweza vipi kusema sababu za kutokuwepo uchawi angali nimeshasema haupo?
Hapo kinachotakiwa ni mwenye kudai uchawi upo atoe hoya mimi nikosoe kwa mapungufu nitakayo baini kwenye utetezi huo.
Ni sawa wewe unituhumu nimekuibia pesa yako halafu tena unaniambie niseme kipi kimenifanya nisidhani nimekuibia.
Hapo mantiki ipo wapi?
Ukishindwa kungamua haya nitajua wewe hujaiva kwenye kuchambua mambo critically.
Tatizo mkuu hatuelewani kwa sababu unanipeleka ambapo mie sipo. Haya madai ya kuwepo uchawi tumezaliwa na kuyakuta,sasa wewe pia unadai kuwa hakuna huo uchawi ambao watu wanadai kuwa upo.
Kwahiyo mie nilichotaka kwako ni sababu zilizokufanya kuona hili jambo la kuwepo uchawi si la kweli na ndiyo maana ukasema hakuna uchawi,maana umepinga madai ya kuwepo uchawi hivyo lazima utakuwa na sababu zilizokufanya ukatae hayo madai ya kuwepo uchawi na ndiyo hicho nachotaka.
Hivyo sio kwamba mie nataka ueleze kwanini hakuna uchawi kama ulivyosema.