Hivi kweli uchawi upo?

Hivi kweli uchawi upo?

Issue siyo kuwepo au kutokuwepoi uchawi au majini...

issue inaanzia pale ukipatwa na matatizo yafananayo na uchawi au majini hapo ndiyo imani yako huangukia huko...

Ni mpaka yakukute...

Ni sawa na kushangaa watu wanauguaje kipindu pindu, ila siku utakapoanza kuharisha ndiyo imani itakujia kumbe kipo kweli..


cc: mahondaw
 
ndi upo kwa waganga tunaenda na hatuachi. wew shida yako ni nin au na wee mchawi mana hata matendo tu yanaonshaaaaa
 
Toka mdogo nasikiaga uchawi ,ushirikina ,,mbona sijawahi shuhudia zaidi ya kusimuliwa na msimuliaji ukimuuliza nae hajaona alisimuliwa tu,,hivi inakuwaje haoa kuaminishwa vitu ambavyo hujawah kuviona,,
Matatizo ya hapa duniani yapo tu na ni yale yale lakin utasikia unaambiwa umechezewa,nyota yako imeibiwa au umerogwa kabisa,,,
Niseme tu hivi mi nisjachoka mambo ya kusimuliwa tu vitendo sioni hata hayo madini yenu nayo hivyo hivyoo ni story ,na ushabiki hakuna cha kumuona hata mtume mmoja akatuthibitishia kuwa hiv ni kweli

Hivi kungekuwa na uchawi ambavyo binadam hatupendanii sidhan kama ningepata hata muda wa kuandika huu uzi,,ningekua nisharogwa au kuuawa kabisa,,,
Tuache imani za kishirikina hazitusaidii kabisa,
Mpaka nimekua hapa sijawah ona nasimuliwaga tu ukiuliza ulikuwepo utajibiwa hapana ila ni kweli
Na nyie mnaoenda kwa waganga hizo pesa zenu bora mnywee bia mle na nyama ,mnaibiwa tu hata hamna akili kabisa
Mnaoenda wote kwa waganga mkapimwe mikojo na vinyesi vyenu
Nasikitika wewe ni mtoto na sielewi uko Mjini au kijijini bado kabila lako silijui ,ila nakutoa wasiwasi usiwaze sana ki sheria uchawi haupo kabisa na kwa uhalisia uchawi upo kwa Tanzania na Africa yote na uamini hata ulaya uchawi upo na ndiyo maana hata vitabu vitakatifu biblia na Koran vinautaja kwa taarifa yako njoo usukumani uone jinsi MTU anakuwa na fisi wake nyoka nk usikutese utoto kuna watu wameumizwa na uchawi wanaugulia vitandani kwa magonjwa ambayo hospitalini hayana tiba KUA UYAONE
 
hapo ulipo umeshalogwa ndo nyie mnashinda mnawanga mkija hum mnajfanya mungu mungu mxiiiiii najua utatukana all the best
naanzaje kukutukana asa mrembo,najua umetumia uhuru wako wa kikatiba ipasavyo.so breath in,breath out then relax
 
Vyote hivyo story tu
Tumekua tunaaminishwa hivyo toka wadogo lakin chenga tu
Inawezaka ni story kwako lkn kwa wengine is not a story.
Maswali.
1. Ww ni dini gani?
2. Unahudhuria kwenye nyumba za ibada
3. Una amini Mungu yupo?
4. Una amini shetani yupo?
5. Unaamini Majini yapo?
6. Una amini kuna nguvu za Mungu?
7. Una amini kuna nguvu za giza?
6. Una amini vitabu vya dini?
Tuanzie hapo kwanza. Nahitaji majibu. Ukishajibu nitakupa jibu kuhusu kile unachoamini
 
hata biblia inataja uchawi Upo na WACHAWI wapo. Ila habari njema Israel hakuna uchawi wala wachawi

UCHAWI UNASEMWA KATIKA BIBLIA


1. Hesabu 23:23 Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!



2. Hesabu 24:1 Basi Balaamu alipoona ya kuwa ilimpendeza Bwana kuwabariki Israeli, hakwenda, kama hapo kwanza, ili kutafuta uchawi, bali alielekeza uso wake jangwani.


3. Hesabu 23:23 Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!


4. Hesabu 23:23 Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!


5. 1 Samweli 15:23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.


6. 2 Wafalme 9:22 Ikawa, Yoramu alipomwona Yehu, akasema, Je! Ni amani, Yehu? Akajibu, Amani gani, maadamu uzinzi wa mama yako Yezebeli na uchawi wake ni mwingi?


7. 2 Wafalme 17:17 Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.


8. Isaya 47:9 lakini mambo haya mawili yatakupata katika dakika moja siku moja, kufiwa na watoto, na ujane; yatakupata kiasi kitimilifu, uchawi wako ujapokuwa mwingi, na uganga wako mwingi mno.


9. Isaya 47:12 Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda.


10. Mika 5:12 nami nitakatilia mbali uchawi, usiwe mkononi mwako; wala hutakuwa tena na watu wenye kutabana;


11. Nahumu 3:4 Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake.


12. Matendo ya Mitume 8:9 Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.


13. Matendo ya Mitume 8:11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.


14. Wagalatia 5:20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,


15. Ufunuo wa Yohana 9:21 Wala hawakuutubia uuaji wao, wala uchawi wao, wala uasherati wao, wala wivi wao.


16. Ufunuo wa Yohana 18:23 wala nuru ya taa haitamulika ndani yako tena kabisa; wala sauti ya bwana-arusi na bibi-arusi haitasikiwa ndani yako tena kabisa; maana hao wafanya biashara wako walikuwa wakuu wa nchi, kwa kuwa mataifa yote walidanganywa kwa uchawi wako.




WACHAWI – BIBLIA INA AINISHA HAWA HAPA

Kutoka 7:11 Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao.


Mambo ya Walawi 19:31 Msiwaendee wenye pepo, wala wachawi; msiwatafute; ili kutiwa unajisi na wao; Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.


Mambo ya Walawi 20:6 Na mtu yule atakayewaendea wenye pepo, na wachawi, ili kuzini pamoja nao, nitakaza uso wangu juu ya mtu yule, nitamtenga na watu wake.


1 Samweli 28:3 Basi Samweli alikuwa amefariki dunia, nao Israeli wote walikuwa wamemwomboleza, na kumzika huko Rama, ndani ya mji wake mwenyewe. Tena Sauli alikuwa amewaondolea mbali hao wenye pepo wa utambuzi na wachawi katika nchi.


1 Samweli 28:9 Yule mwanamke akamwambia, Angalia, unajua alivyofanya Sauli, jinsi alivyowakatilia mbali hao wenye pepo wa utambuzi na wachawi katika nchi; mbona basi wanitegea tanzi uhai wangu, ili kuniua?


2 Wafalme 21:6 Akampitisha mwanawe motoni, akatazama bao, akafanya uganga, akajishughulisha na hao wenye pepo wa utambuzi, na wachawi; akafanya mabaya mengi machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.


2 Wafalme 23:24 Tena wenye pepo wa utambuzi, na wachawi, na vinyago, na sanamu, na machukizo yote yaliyoonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, Yosia akayaondoa yote, ili apate kuyathibitisha maneno ya torati yaliyoandikwa katika kile kitabu alichokiona Hilkia kuhani ndani ya nyumba ya Bwana.


2 Mambo ya Nyakati 33:6 Tena akawapitisha wanawe motoni katika bonde la mwana wa Hinomu; akatazama bao, akabashiri, akafanya uganga, akajishughulisha na hao wenye pepo wa utambuzi, na wachawi; akafanya mabaya mengi machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.


Isaya 8:19 Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong'ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?


Isaya 19:3 Na roho ya Misri itamwagika kabisa katikati yake, nami nitayabatilisha mashauri yake, nao watakwenda kwa sanamu zao, na kwa waganga, na kwa wapiga ramli, na kwa wachawi.


Danieli 1:20 Na katika kila jambo la hekima na ufahamu alilowauliza mfalme, akawaona kuwa walifaa mara kumi zaidi ya waganga na wachawi waliokuwa katika ufalme wake.


Danieli 2:2 Ndipo mfalme akatoa amri kuwaita waganga, na wachawi, na wasihiri, na Wakaldayo, wapate kumweleza mfalme ndoto zake. Basi wakaingia, wakasimama mbele ya mfalme.


Danieli 2:27 Danieli akajibu mbele ya mfalme, akasema, Ile siri aliyoiuliza mfalme, wenye hekima hawawezi kumfunulia mfalme; wala wachawi, wala waganga, wala wanajimu;


Danieli 4:7 Ndipo wakaingia waganga, na wachawi, na Wakaldayo, na wanajimu; nikawahadithia ile ndoto; wao wasiweze kunijulisha tafsiri yake.


Danieli 5:7 Mfalme akalia kwa sauti kubwa, akaamuru waletwe wachawi, na Wakaldayo na wanajimu. Mfalme akanena, akawaambia wenye hekima wa Babeli, mtu awaye yote atakayesoma maandiko haya, na kunionyesha tafsiri yake, atavikwa mavazi ya rangi ya zambarau, na kuwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atakuwa mtu wa tatu katika ufalme.


Danieli 5:11 Yuko mtu katika ufalme wako, ambaye roho ya miungu watakatifu inakaa ndani yake; na katika siku za baba yako nuru na ufahamu na hekima zilionekana ndani yake; na mfalme Nebukadreza, baba yako, naam, mfalme, baba yako, akamfanya kuwa mkuu wa waganga, na wachawi, na Wakaldayo, na wanajimu;


Danieli 5:15 Basi sasa, watu wenye hekima na wachawi wameletwa mbele yangu, wapate kulisoma andiko hili, na kunijulisha tafsiri yake; lakini hawakuweza kunijulisha tafsiri ya jambo hili.


Malaki 3:5 Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi.


Ufunuo wa Yohana 21:8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.


Ufunuo wa Yohana 22:15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
 
dada upo sahihi uchawi ni haupo,

narudia tena uchwai haupo

ambaye anasema upo naomba atetee hoja zangu..

1. wakati mkoloni anakuja africa tulikuwa na waganga na wachawi wengi lakini wazungu walitupiga sana na kutukoloni.. vita maji maji risasi hazikugeuka maji na ziliua babu zetu, hapo uchawi uliprove failure... kuna wajinga watasema wazungu nao ni wachawi na walituzidi uchawi,, swali kama ni wachawi mbona hawakuja na ungo walikuja na mitumbwi na meli,, na bunduki juu kwa nini hawakupigana kiuchawi uchawi

2. ufisadi.. mtu kama chenge anatuibia taifa zima kwa nini wachawi wasimroge ageuke paka.. kuna wajinga watasema chenge nae mchawi... je uchawi wa chenge unazidi wachawi wa nchi nzima wanaochukia ufisadi

3. michezo.. mbona africa hatuchukui kombe la dunia kama tuna uchawiii... au timu zote za tanzania tukianza na simba na yanga mbona hazichukui hata caf champions league.. mtasema nigeria wachawi sana na hata hao nigeria timu pekee kutwaa hilo kombe ni enyimba tu 2003-2004 baada ya kalu kuwekeza hela nyingi sana ,, na baada ya hapo hakuna timu yeyote nigeria imewai kuchukua na uchawi wao woteeeeee... maana yake uchawi haupo na kama upo hauna nguvu tunazoaminishwa.

4. kama uchawi upo na una nguvu kwa nini mganga maji marefu anaendaga kutibiwa india apollo.. kwa nini dawa zake au waganga wenzake wasishirikiane kumtibu mganga mwenzao.. maaana yake uchawi haupo.

5. chuma ulete kwa nini haingii benki kuiba helaaaa.... na benki kuna hela nyinngiiiii

6. zile story za jini mrefu kavaa kanzu tulizozisikia miaka ya 90 zimeishia wapi ? na popo bawa je ? smart phone na internet zimefuta hizo story maana humdanganyi mtu nowdays.... mtu anakwambia tuma picha ya jini uliyemuona au anamgoogle asipomuona google tu anajua uongooo..........uchawi ni haupo haupo haupo haupo haupo
 
Dini zipo kuna watu wanaabudu Mungu, miti, wanyama, vinyago, watu nk
Ushawahi kumuona Mungu? Km bado kwann unamuomba Mungu ilihali haujamuona?
Km ilivyongumu kuthibitisha uwepo wa Mungu ndivyo ilivyongumu kuthibitisha uchawi. Lkn vyote vipo.
Maeneo ya mjini, ni ngumu kukutana na masuala ya uchawi na vituko vyake. Nakushauri fanya research, tembea vijijini hasa vya wasukuma ili kuthibitisha km upo uliza hapo kijijino ni nani unahisi no mchawi, wakikutajia nenda ukamfanyie jambo lolote la kuudhi uone matokeo yake
 
Nina wasiwasi hapo ulipo una kinga kali na mchawi akijaribu anaondoka yeye. Acha jutudanganya eti hakuna uchawi. Na kama huna kinga subiri wenyewe waje, omba wasije utatamani ardhi ipasuke ujichimbie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna vijiujanja janja lakini kiuhalisia uchawi haupo ni ujanja wa kisaikolojia :
Anza leo kuvaa kanzu nyeusi kope zako zinyoe nyumba unayoishi fuga paka weusi 100 kisha hakikisha nje umeninginiza bundi wawili tafuta mwendo wa ajabu wa kutembea aidha usisahau kutembea barabarani na cage ya kunguru ndani mkononi na uwe na ulinzi mkali gari nzuri nakuapia utapiga hela kwa kuzuga mganga pili story za watu kudai uliwakaba usiku zitashamiri sana ,chunguza jamii zinazoamini uchawi utagundua ni masikini sana kigoma ,bagamoyo, sumbawanga ona waliojiweka mbali na mambo hayo kiasi wahaya,wachaga wapare wako vyema ,navyojua mimi ulimwengu wa kiroho upo ila hauna nguvu kivile ila unatumia saikolojia kututisha jini kama jini halina mwili hivyo haliwezi hata kuinua punje ya mchele ila linaweza chukua umbo la kukutishia ww ila ukiliona ukakomaa kulifata litapotea halina linachoweza
 
Toka mdogo nasikiaga uchawi ,ushirikina ,,mbona sijawahi shuhudia zaidi ya kusimuliwa na msimuliaji ukimuuliza nae hajaona alisimuliwa tu,,hivi inakuwaje haoa kuaminishwa vitu ambavyo hujawah kuviona,,
Matatizo ya hapa duniani yapo tu na ni yale yale lakin utasikia unaambiwa umechezewa,nyota yako imeibiwa au umerogwa kabisa,,,
Niseme tu hivi mi nisjachoka mambo ya kusimuliwa tu vitendo sioni hata hayo madini yenu nayo hivyo hivyoo ni story ,na ushabiki hakuna cha kumuona hata mtume mmoja akatuthibitishia kuwa hiv ni kweli

Hivi kungekuwa na uchawi ambavyo binadam hatupendanii sidhan kama ningepata hata muda wa kuandika huu uzi,,ningekua nisharogwa au kuuawa kabisa,,,
Tuache imani za kishirikina hazitusaidii kabisa,
Mpaka nimekua hapa sijawah ona nasimuliwaga tu ukiuliza ulikuwepo utajibiwa hapana ila ni kweli
Na nyie mnaoenda kwa waganga hizo pesa zenu bora mnywee bia mle na nyama ,mnaibiwa tu hata hamna akili kabisa
Mnaoenda wote kwa waganga mkapimwe mikojo na vinyesi vyenu
Ni nini ambacho unakusudia unaposema haujawahi kushuhudia uchawi? maana uchawi si kama jua ambalo tunaona likizama na kuchomoza.
 
Back
Top Bottom