Hivi kweli uchawi upo?

Hivi kweli uchawi upo?

Uchawi, ushirikiana, ulozi ni story za kusadikika ambazo wajinga wanadanganyana na kuziamini. Hakuna uchawi
Ni kipi ulichofanya katika kutafuta ukweli wa hili jambo hadi ukafikia kujiridhisha kuwa hakuna uchawi? unawezaje kuthibitisha maneno yako kuwa hakuna hicho kinachoitwa uchawi bali ni kitu kingine?

Mfano kuna mambo mengi yanayotokewa kwenye jamii zetu ambayo huitwa uchawi,na uhakika utakuwa umeyashuhudia je unaweza kutupa majibu kuwa hayo mambo tunayowaza ni uchawi si uchawi bali nini?
 
Kama hujaingia kwenye 18 za washirikina unaweza fikiri uchawi ni porojo tu,mimi kuna jamaa yangu ni dereva na ofisi anapofanya kazi walinunua gari mpya jamaa akapewa yeye ndiye awe dereva kumbe kuna madereva wengine pale wanaitolea macho ile gari hazikupita siku mbili jamaa mikono ikapooza wameenda hospitali kubwa zote wanacheki mfumo wa misuli majibu yanaoshesha yuko poa lakini ndio hivyo mikono aifanyi kazi tena na umetokea mtikisiko mkubwa wa uchumi kwenye familia yake kwa sababu jamaa hadi sasa ana hangaikia afya yake sasa hivi vitu hadi uingie kwenye 18 za mafundi ndio utayatambua yapo na sio porojo.

-Ndumilakuwili-
 
Habari!

Kujibu swali lako kama uchawi upo au haupo kwanza inabidi kufahamu maana ya uchawi ni nini.

Kama unamaanisha uchawi ni uwezo/maarifa kuweza kupaa kwenye ungo usiku hadi mji wa mbali kwa sekunde tu. Au uwezo kupenya kwenye ukuta na kuingia nyumbani kwa mtu na kumroga hapo ni uwongo tu. Hayo yanaitwa masimulizi ya kutunga au ngano.

Pili, kama unamaanisha uchawi ni uwezo wa kutumia miti shamba kutibu magonjwa tofauti na mgonjwa kupona basi hapo ni sawa uchawi upo na unafanya kazi.

Lakini pia kama unamaanisha uchawi ni ujuzi wa kusoma hisia za mtu kwa kiasi fulani hivyo kumshauri lipi anapasa kufanya kuboresha maisha yake, biashara yake, ndoa yake, masomo yake, basi kwa maana hii uchawi upo.

Haya mambo yanategemea na mtu anavyodhani hicho anachokiita "uchawi" kinafanya kazi.

Mwisho niseme tu umeleta swali yako kama mtu "ignorant".

Hayo mambo yakupimwa mkojo ni upuzi kwenye swali lako. Haukupaswa uyaingize.

Wakati mwingine mnafanya watu wenye mawazo mapana wasichangie mada hapa JF kwasababu wanaona watu wanaoanzisha mada hawapo kwaajili ya kujifunza.

Hili ni angalizo

Soma nyuzi za miaka ya nyuma uone mijadala ilivyopendeza.
 
Habari!

Kujibu swali lako kama uchawi upo au haupo kwanza inabidi kufahamu maana ya uchawi ni nini.

Kama unamaanisha uchawi ni uwezo/maarifa kuweza kupaa kwenye ungo usiku hadi mji wa mbali kwa sekunde tu. Au uwezo kupenya kwenye ukuta na kuingia nyumbani kwa mtu na kumroga hapo ni uwongo tu. Hayo yanaitwa masimulizi ya kutunga au ngano.

Pili, kama unamaanisha uchawi ni uwezo wa kutumia miti shamba kutibu magonjwa tofauti na mgonjwa kupona basi hapo ni sawa uchawi upo na unafanya kazi.

Lakini pia kama unamaanisha uchawi ni ujuzi wa kusoma hisia za mtu kwa kiasi fulani hivyo kumshauri lipi anapasa kufanya kuboresha maisha yake, biashara yake, ndoa yake, masomo yake, basi kwa maana hii uchawi upo.

Haya mambo yanategemea na mtu anavyodhani hicho anachokiita "uchawi" kinafanya kazi.

Mwisho niseme tu umeleta swali yako kama mtu "ignorant".

Hayo mambo yakupimwa mkojo ni upuzi kwenye swali lako. Haukupaswa uyaingize.

Wakati mwingine mnafanya watu wenye mawazo mapana wasichangie mada hapa JF kwasababu wanaona watu wanaoanzisha mada hawapo kwaajili ya kujifunza.

Hili ni angalizo

Soma nyuzi za miaka ya nyuma uone mijadala ilivyopendeza.
Ok mkuu sasa tueleze ni vp haya mambo ya kupaa na ungo na mfano wa hayo ni uongo.
 
Ok mkuu sasa tueleze ni vp haya mambo ya kupaa na ungo na mfano wa hayo ni uongo.
Kwanza nikujuze jambo.

You can't prove negative.

Kitu kama hakipo haiwezekani kukithibitisha.

Hii ni sheria ya logic.

Wewe unayesema uchawi upo ndiyo unajukumu kuonyesha huo uchawi upo.

Je hapa unanielewa? Kwamba jukumu la kudhibitisha unalo wewe na si mimi?

Kwa miaka na miaka madai ya uwepo wa uchawi hayajapata uthibitisho kokote kule.

Kama wewe unaweza thibitisha pasi shaka.

Kwa kiasi fulani naelewa psychology na vile ubongo unaweza tenda.

Niseme tu, mwanadamu huanza kuhusisha mambo fulani na uchawi pale anapokuwa hana uelewa kuhusu mambo hayo.

Kama vile watu wanavyodhani telepathy, astral traveling, remote viewing na kadhalika.

Jambo baya ni kwamba, watu wengi hawatojatibu kudadisi mambo mengi waliyosikia au kudhani yanawezekana kwa wanachokiita uchawi.

Jifunze mambo taratibu, mambo mengi tunayodhani ni kweli yanapotoshwa.
 
Mimi siamini katika uchawi..
Kama kuna mchawi humu ake PM nimpe details zangu aniroge..akifanikiwa kuna zawadi yake.

Hatuwezi kuishi kwa kudanganywa miaka yote hadi ninyi great thinkers mnaamini upuuzi kama uchawi..

Maza fanta uchawi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza nikujuze jambo.

You can't prove negative.

Kitu kama hakipo haiwezekani kukithibitisha.

Hii ni sheria ya logic.

Wewe unayesema uchawi upo ndiyo unajukumu kuonyesha huo uchawi upo.

Je hapa unanielewa? Kwamba jukumu la kudhibitisha unalo wewe na si mimi?

Kwa miaka na miaka madai ya uwepo wa uchawi hayajapata uthibitisho kokote kule.

Kama wewe unaweza thibitisha pasi shaka.

Kwa kiasi fulani naelewa psychology na vile ubongo unaweza tenda.

Niseme tu, mwanadamu huanza kuhusisha mambo fulani na uchawi pale anapokuwa hana uelewa kuhusu mambo hayo.

Kama vile watu wanavyodhani telepathy, astral traveling, remote viewing na kadhalika.

Jambo baya ni kwamba, watu wengi hawatojatibu kudadisi mambo mengi waliyosikia au kudhani yanawezekana kwa wanachokiita uchawi.

Jifunze mambo taratibu, mambo mengi tunayodhani ni kweli yanapotoshwa.
Mimi sijasema uchawi upo au haupo ila wewe unasema haupo na ndiyo maana nikashawishika kwa kutaka kujua kutoka kwako kwamba umewezaje kujua kuwa uchawi haupo?

Kwa sababu ukisema tu kuwa haijathibitishwa kuwepo huo uchawi ndiyo sababu iliyokufanya useme hakuna uchawi sidhani kama utakuwa sahihi,chukua mfano leo hii kuna watu wanasema Ben saanane amekufa/ameuliwa. Lakini haijathibitika,je ndiyo unaweza kusema kuwa Ben yupo hai kisa haithibitika kama kafa?
 
Uchawi haupo
Uchawi upo na Mungu yupo pia hivyo usijidanganye kwamba uchawi haupo hata vitabu vitakatifu vinatambua uchawi upo na mifano yake ipo kama huamini kuna siku utajua ukikanyaga sehemu mbaya.Uchawi unauzwa Sumbawanga bei kuanzia laki 3 na zaidi na watu wanaweza kuroga siku hiyo hiyo anayonunua uchawi tumewaona hatuongei tu.Tembelea Majimoto mpanda ukape historia,nenda nkansi,nenda sumbawanga vijijini ndio utajua ukitaka nikutajie vijiji ili ukafanye utalii na kwakujaribu kama kweli uchawi upo vijiji hivyo ukifika dharau wazee na kujifanya mjuaji sana ikibidi fanya maringo kama unaingia chumbani mwako majibu watapata rafiki zako uliowaaga kuwa unakwenda kutest mitambo lakini wewe wakati huo hautakuwa na feedback za kutuletea bali ni dead body ndani ya coffin

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Braza hizo mambo zisikie tu hivyo hivyo kwa watu atleast zitakuwa hazina uzito.

Katika hangaika hangaika ya kusaka life,nilienda kijiji flan katika mkoa flani ( sorry sitotaja jina). Lengo ilikuwa ni kufanya kilimo cha bustani (kipindi cha kiangazi). Kile kijiji mgeni ukifika kuanza biashara au kilimo sharti uonane na wazee wa kijiji. Nikaonana na wa kwanza,baadae nikaambiwa kuna na mwingine,after huyo pia nimaambiwa kuna mwingine yupo mlimani (alaf wazee wote hao inabidi uwafate wewe,maana hawakufati).

Badae nikaona napoteza muda tu heri nifanye mambo yangu,so nikampotezea hugo mzee aliyepo milimani maana nilishachoka kuzunguka kwa wazee kila siku.

Ila nilivyopanda matikiti alafu yakaota maboga ndio nikachoka. Ila sipendagi kujishusha sana,so nikasepa na kuwaachia kijiji chao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi siamini katika uchawi..
Kama kuna mchawi humu ake PM nimpe details zangu aniroge..akifanikiwa kuna zawadi yake.

Hatuwezi kuishi kwa kudanganywa miaka yote hadi ninyi great thinkers mnaamini upuuzi kama uchawi..

Maza fanta uchawi

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa wewe umeamua kutokuamini uchawi au unatumbia hakuna uchawi?
 
Mimi sijasema uchawi upo au haupo ila wewe unasema haupo na ndiyo maana nikashawishika kwa kutaka kujua kutoka kwako kwamba umewezaje kujua kuwa uchawi haupo?

Kwa sababu ukisema tu kuwa haijathibitishwa kuwepo huo uchawi ndiyo sababu iliyokufanya useme hakuna uchawi sidhani kama utakuwa sahihi,chukua mfano leo hii kuna watu wanasema Ben saanane amekufa/ameuliwa. Lakini haijathibitika,je ndiyo unaweza kusema kuwa Ben yupo hai kisa haithibitika kama kafa?
Unaniuliza

"Umejuaje uchawi haupo"

Sentensi yako haina mantiki katika mjadala.

Mwanzo nimekupa angalizo kwamba

You can't prove negative. Haiwezekani kuthibitisha kitu kisichokuwepo.

Kinachowezekana kuthibitishwa ni kilichopo. Sawa?

Naona unanirudisha nilipokujibu

Ni hivi, kwa sheria ya logic haiwezekani kuthibitisha kitu kisichokuwepo.

Nasema logic kwasababu ndiyo itatupa mtiririko mzuri ili wote tuelewane.

Vinginevyo inakuwa mabishano yasiyo na mantiki.

Nirudi kwenye hoja

Hii sentensi "uchawi haupo" ni ukanusho kwahiyo haiwezekani kuithibitisha sentensi hii.

Ni sawa na watu wawili wameingia kwenye chumba kitupu halafu mmoja anadai ndani ya chumba hicho kuna kiti. Mwenzake anamwambia hakuna hicho kiti unachosema kipo. Hapo jukumu la kuthibitisha ni la mwenye madai.

Logic ni ngumu twende polepole.

Kama wewe hujui uchawi upo au haupo maana yake unapaswa upate uthibitisho kwa wanaodai iwepo wake.

Je sababu za kuthibitisha uwepo wa wadai yao unakubaliana nazo?

Kama ndivyo sema ni sababu ipi hiyo? Tutaijadili.
 
Unaniuliza

"Umejuaje uchawi haupo"

Sentensi yako haina mantiki katika mjadala.

Mwanzo nimekupa angalizo kwamba

You can't prove negative. Haiwezekani kuthibitisha kitu kisichokuwepo.

Kinachowezekana kuthibitishwa ni kilichopo. Sawa?

Naona unanirudisha nilipokujibu

Ni hivi, kwa sheria ya logic haiwezekani kuthibitisha kitu kisichokuwepo.

Nasema logic kwasababu ndiyo itatupa mtiririko mzuri ili wote tuelewane.

Vinginevyo inakuwa mabishano yasiyo na mantiki.

Nirudi kwenye hoja

Hii sentensi "uchawi haupo" ni ukanusho kwahiyo haiwezekani kuithibitisha sentensi hii.

Ni sawa na watu wawili wameingia kwenye chumba kitupu halafu mmoja anadai ndani ya chumba hicho kuna kiti. Mwenzake anamwambia hakuna hicho kiti unachosema kipo. Hapo jukumu la kuthibitisha ni la mwenye madai.

Logic ni ngumu twende polepole.

Kama wewe hujui uchawi upo au haupo maana yake unapaswa upate uthibitisho kwa wanaodai iwepo wake.

Je sababu za kuthibitisha uwepo wa wadai yao unakubaliana nazo?

Kama ndivyo sema ni sababu ipi hiyo? Tutaijadili.
Mkuu twende polepole,sijakwambia uthibitishe kama uchawi haupo ila nimekuuliza umejuaje kama uchawi haupo?

Ulichotakiwa ni kunieleza tu ni jinsi gani wewe umeweza kujua kuwa hakuna uchawi?

Nachotaka ni sababu zilizokufanya useme kuwa hakuna uchawi na si kwamba nataka unithibitishie kisichokuwepo.
 
Mkuu twende polepole,sijakwambia uthibitishe kama uchawi haupo ila nimekuuliza umejuaje kama uchawi haupo?

Ulichotakiwa ni kunieleza tu ni jinsi gani wewe umeweza kujua kuwa hakuna uchawi?

Nachotaka ni sababu zilizokufanya useme kuwa hakuna uchawi na si kwamba nataka unithibitishie kisichokuwepo.
Nikueleze mara ngapi kuwa haiwezekani kuprove negative?

Nimekupa mfano wa watu wawili kwenye chumba kisicho na kitu halafu kati ya hao watu wawili mmoja akadai ndani ya hicho chumba kuna kiti. Mwenzake akakanusha kwa kusema hakuna hicho kiti. Je hapa jukumu la kuthibitisha kuwa kiti kipo ndani ya hicho chumba ni nani?

Wewe inaonyesha huelewi logic ndiyo maana unarudia jambo nalokuambia.

Mimi nitaweza vipi kusema sababu za kutokuwepo uchawi angali nimeshasema haupo?

Hapo kinachotakiwa ni mwenye kudai uchawi upo atoe hoya mimi nikosoe kwa mapungufu nitakayo baini kwenye utetezi huo.

Ni sawa wewe unituhumu nimekuibia pesa yako halafu tena unaniambie niseme kipi kimenifanya nisidhani nimekuibia.

Hapo mantiki ipo wapi?

Ukishindwa kungamua haya nitajua wewe hujaiva kwenye kuchambua mambo critically.
 
Back
Top Bottom