Hivi kwanini Mwl. Nyerere hakupewa PhD?

Hivi kwanini Mwl. Nyerere hakupewa PhD?

Ritz nataka nikuone hapa JF ukiendelea kuongea kwa majigambo kama ufanyavyo sasa baada ya 2016.
 
Mkuu huyo mwandishi aliondika hiyo habari alikuwa anamuita Nyerere Dr ni James Robbins wa BBC.

Sijui kama anatoka pwani labda Pwani ya Bristol Uingereza.

Nadhani umejifunza kitu.

Mkuu ni Pwani ya Bagamoyo! Hapo hakuna cha kujifunza kwani wazungu wakiandika ndiyo kusema basi? Hebu jaribu kujiamini mwenyewe kwani baada ya miaka 53 ya uhuru hutakiwi kuwatukuza wazungu kama wewe na ndugu zako mnavyofanya! Aibu hi kabisa.
 
Kaka, wakati tumepondaponda betri za National kisha tukaziweka kwenye bati la nyasi mchana kutwa ili zipigwe na jua charge iongezeke ili baadaye saa mbili kamili tuweze kupata ngoma za Morris Nyunyusa kabla Jacob Tesha hajatuletea taarifa ya habari kwenye ile radio ya mbao, ni lini ulishawahi kusikia jina la Dr Nyerere likitamkwa?
Kweli kaka, ndilo ninalomweleza huyu kiu.no tazama namba 72. hapo juu
 
Mkuu nikuwekee akiitwa dr kabla ya kifo chake?

Mkuu usijifanye hamnazo; hivi wewe utanizuia kukuita Dr. fulani? Tatizo linakuja pale utakapofurahia na kukenua meno kwa sifa ambazo huna. Nyerere (very very rarely) aliitwa; hakujiita na wala hakuona kuitwa huko ni kitu cha maana cha kufungamana nacho au miongoni mwa visifa vyenye maana kwake. Jamani, title ya President ni heshima ya juu kabisa katika nchi; ile kuwa tu Rais huhitaji vikorombwezo vingine.

Watu wanakuwa na mashaka kwamba Rais wetu anafurahia hizo titles to Dr. na Prof. kwa sababu badala ya kuitwa na wengine ndiye anayeongoza kujiita hivyo. Unataka ushahidi? Huu hapa:Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Tovuti Rasmi ya Ikulu; kwenye hiyo tovuti rasmi ya Ikulu hakuna bandiko linalomhusu Rais ambalo halianzi na hiyo title; hiyo ni Ofisi yake mwenyewe ukumbuke.

Cha kushangaza hata wasifu wake (taz. picha yake kushoto) wameandika "Dr. Jakaya M Kikwete - Wasifu". Neno "Rais" wala halipo kwa kupapatikia cheo cha Dr. Ingependeza kama ingesomeka "Rais Jakaya M Kikwete - Wasifu" yaani kwa haraka haraka au kwa mgeni sio rahisi kujua kwamba ndiye rais wa nchi. Hebu waambieni "Kurugenzi ya Mawasiliano ..." irekebishe hiyo kitu bana; heshima kwa Rais ni u-Rais wake sio u-Dr. au u-Prof.

Cc: MpigfilimbiwaHamelin, lendila, swanga, Jumong S, inter, ifweero, Simiyu Yetu, Chabruma, kiboko ya mengi, et. al.
 
Last edited by a moderator:
Unajua ulikuwa ni utashi wa mwandish kumu-adress hivyo kama ni kweli. Lakini hiyo sio official way ya kumu-address. Official addreasing yake ilikuwa ni Mwl. Julius K. Nyerere. Hakuna sehemu yeyote alipokuwa address officially km dr. au Prof. Lakni hawa wauza nchi wamelazimisha kuwa addressed kwa vyeo feki. Ndio maana unaona kila sehemu wanaojipendekeza wanamwita Dr. Prof.Jakaya.
 
Hii nchi inawasomi wengi: Dr.Kikwete, Dr.Slaa,Dr.Leakey,Dr.Ndodi na wengine kibao
 
Kwanini mwalimu nyerere akupewa heshima ya profesa? Inamaana jakaya ni rais bora kuliko nyerere?

Nyerere Ni Bora Kuliko Hata Hao Wazungu Pori Wenzio Watoa Hizo Academic Titles. Na Ukiona Watu Wanakusifu Sana Huku Wakikupamba Na Kukutukuza Jua Kwamba Umeshafikia Kiwango Chako Cha Mwisho Cha U.P.U.M.B.A.V.U. Na Sasa Unaelekea Kuwa CHIZI Kama Siyo Useless. Tafakari! Nyerere Anafananishwa Labda Na Akina Aristotle, Hobbes, Kant, Locke Na Marx ( Philosophers Wa Heshima Hapa Duniani Ambao Mawazo Yao Ya Kale Ndiyo Leo Tunayaishi ).
 
Chanzo cha jk kupewa uprofesa china. Ni baada ya kusaini mikataba 21 kwa dakika moja. Bila hata kuipitia means alijua kilichomo. Rais wa uchina akasitaajabu uwezo wa jk fasta akampatia uprooo

Kama uliyo andika ni ya kweli basi na mimi nawaomba wana jf kwa hisani yenu nimtunuku wadhifa mwingine raisi wetu muelewa.
 
Mkuu usijifanye hamnazo; hivi wewe utanizuia kukuita Dr. fulani? Tatizo linakuja pale utakapofurahia na kukenua meno kwa sifa ambazo huna. Nyerere (very very rarely) aliitwa; hakujiita na wala hakuona kuitwa huko ni kitu cha maana cha kufungamana nacho au miongoni mwa visifa vyenye maana kwake. Jamani, title ya President ni heshima ya juu kabisa katika nchi; ile kuwa tu Rais huhitaji vikorombwezo vingine.

Watu wanakuwa na mashaka kwamba Rais wetu anafurahia hizo titles to Dr. na Prof. kwa sababu badala ya kuitwa na wengine ndiye anayeongoza kujiita hivyo. Unataka ushahidi? Huu hapa:Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Tovuti Rasmi ya Ikulu; kwenye hiyo tovuti rasmi ya Ikulu hakuna bandiko linalomhusu Rais ambalo halianzi na hiyo title; hiyo ni Ofisi yake mwenyewe ukumbuke.

Cha kushangaza hata wasifu wake (taz. picha yake kushoto) wameandika "Dr. Jakaya M Kikwete - Wasifu". Neno "Rais" wala halipo kwa kupapatikia cheo cha Dr. Ingependeza kama ingesomeka "Rais Jakaya M Kikwete - Wasifu" yaani kwa haraka haraka au kwa mgeni sio rahisi kujua kwamba ndiye rais wa nchi. Hebu waambieni "Kurugenzi ya Mawasiliano ..." irekebishe hiyo kitu bana; heshima kwa Rais ni u-Rais wake sio u-Dr. au u-Prof.

Cc: MpigfilimbiwaHamelin, lendila, swanga, Jumong S, inter, ifweero, Simiyu Yetu, Chabruma, kiboko ya mengi, et. al.
Usiwe punguani wewe niwekee ushahidi wapi Rais Kikwete kajiita Dr au Prof.

Usipende kuokota maneno kwenye vijiwe vya mbege na kuleta JF.

Weka ushahidi usipoweka nakuweka kwenye orodha yangu ya mapunguani wa JF.
 
Last edited by a moderator:
Chanzo cha jk kupewa uprofesa china. Ni baada ya kusaini mikataba 21 kwa dakika moja. Bila hata kuipitia means alijua kilichomo. Rais wa uchina akasitaajabu uwezo wa jk fasta akampatia uprooo

Mkuu wengine hatuna bima ya afya, nimecheka kiasi kwamba mbavu zangu sasa zinaleta mgogoro wa maumivu. You made my day.
 
Unajua si Mwalimu Nyerere tu ambaye amepata lundo la hizi tuzo,wapo wengi lakini hawajawahi zitumia na kujiita ma-doctor wala professor! Tanzania baada ya Nyerere,Mwinyi na Mkapa tunapitia kipindi kigumu sana ambacho mtawala wa nchi anajipachika titles za kijinga kama akina Iddi Amin na Bokassa!
unamiaka mingapi sister? sisi tulivaa matairi ya magari miguuni, mama zetu walivaa kaniki, tulipanga foleni kununua chunvi, sabuni, mafuta ya taa, kiberiti na vinavyofanania na hivyo. ilifikia kipindi tulifua hata nguo zetu kwa magombe ya miti. halafu wewe teenager-senge unapost ujinga humu. usiandike vitu ambavyo huvijui. boring.
 
Usiwe punguani wewe niwekee ushahidi wapi Rais Kikwete kajiita Dr au Prof.

Usipende kuokota maneno kwenye vijiwe vya mbege na kuleta JF.

Weka ushahidi usipoweka nakuweka kwenye orodha yangu ya mapunguani wa JF.


Hivi mimi na wewe nani punguani? Nimekuwekea link hapo; Ofisi yake (Ikulu) ndiyo inayoongoza kumwita hivyo; kama hapendi kwanini asiwaagize waache kufanya hivyo? Niletee statement hata moja kutoka Ofisi ya Rais ikimwita Nyerere Dr. au Prof enzi zake pamoja na kuwa na lundo la hayo ma-title; haipo na haitakaa iwepo.
 
Usiwe punguani wewe niwekee ushahidi wapi Rais Kikwete kajiita Dr au Prof.

Usipende kuokota maneno kwenye vijiwe vya mbege na kuleta JF.

Weka ushahidi usipoweka nakuweka kwenye orodha yangu ya mapunguani wa JF.

Umegoma kutafakari na kujifunza toka kwa wengine??hivi kwako wewe kujiita ni mpaka asimame juu ya jukwaa la siasa ajitape au kuagiza aitwe dr au prof huku akijipiga piga kifua kwa madaha ndio utatafsiri kuwa kajiita?kitendo cha kuitwa au kuandikwa hivyo hasa na vyombo vya habari rasmi vya serikali au ikulu au vingine vyovyote na kuendelea kukenua nako ni kujiita tu.
Kwa hili weka ujuaji pembeni na ukubali 'in good faith' ujifunze toka kwa wenzio.muungwana akivuliwa nguo huchutama hata wale wasio na hekima wamelihubiri hilo
 
Hivi mimi na wewe nani punguani? Nimekuwekea link hapo; Ofisi yake (Ikulu) ndiyo inayoongoza kumwita hivyo; kama hapendi kwanini asiwaagize waache kufanya hivyo? Niletee statement hata moja kutoka Ofisi ya Rais ikimwita Nyerere Dr. au Prof enzi zake pamoja na kuwa na lundo la hayo ma-title; haipo na haitakaa iwepo.
Ndiyo maana nakuita punguani kumbe anaitwa mimi nilidhani anajiita umeona upunguani wako.
 
Wakati wa Nyerere elimu ilikuwa na thamani. Wakati wa kikwete watu wanamaliza chuo hawawezi kuandika hata essay, unategemea ma professor watakuwa wa viwango gani?

Nyerere aliamini katika matokeo kuliko maonyesho.

Kikwete ni janga la AFrica.

Hahahaha....tabby..hawajui hata kuandika essay...
 
Usiwe punguani wewe niwekee ushahidi wapi Rais Kikwete kajiita Dr au Prof.

Usipende kuokota maneno kwenye vijiwe vya mbege na kuleta JF.

Weka ushahidi usipoweka nakuweka kwenye orodha yangu ya mapunguani wa JF.

Mmh..kweli ishi kwingi uone mengi..nlijuaga wapo fb tu. ..
 
Ebu changamsha kidogo tu akili yako, rudi kwenye hoja! Lema na Mbowe wanahusikaje na hili?
Haya chukuwa hii bayana takuwekea na picha hii wakati Dr Nyerere yupo hai.

President of Tanzania, Dr. Julius Nyerere (3rd-L) looks at French President General Charles de Gaulle (C) after their meeting 29 June 1965 at Elysee Palace in Paris. Standing (2nd-L) Louis Jacquinot, Minister of French Overseas Territories, and Maurice Couve de Murville (3rd-R), French Foreign Minister. Nyerere, the first Tanzanian President (1962-85), reorganized the Tanzanian nationalists into the Tanganyika African National Union (1954) and in 1960 he became chief minister. Nyerere was premier when Tanganyika was granted internal self-government (1961), and president of independence 08 December 1962. He led his country on a path of socialism and self-reliance, but his policies failed, and he retired in 1985. (Photo credit should read -/AFP/Getty-
 
Ndiyo maana nakuita punguani kumbe anaitwa mimi nilidhani anajiita umeona upunguani wako.

Wewe akili huna. Anaitwa na nani? Unaitwa na ofisi yako halafu unachekelea? Mbona kwa Nyerere haikuwa hivyo? Au yeye Nyerere hakuwa na hizo shahada? Punguani kweli wewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom