Hivi kwanini klabu ya Yanga inashindwa kuheshimu logo za klabu nyingine?

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Hili jambo sasa limetamalaki mno kwa Viongozi, pamoja na Graphic Designer wa Yanga, kutoheshimu logo maalum za timu nyingine, jambo ambalo si sahihi kwakweli tukiweka ushabiki pembeni.

Wenye mamlaka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, BMT, TFF mko wapi katika hili mbona kimya? Kulikoni.

Mbona kampuni ya simu Vodacom na GSM ambao ni wadhamini wenu wamewaheshimu na kukubali kubadili rangi zao nyekundu na kuweka rangi zenu, kwanini Yanga haiheshimu logo ya timu zingine?

Logo ni sehemu muhimu sana ya utambulisho wa brand yoyote ikiwa ni klabu, Kampuni au Taasisi, ambayo inakuwa na rangi maalum tofauti tofauti ambayo inapaswa kuitambua na kuiheshimu, lakini kwa Yanga hili jambo wameshindwa kabisa na kulitambua kulifanyia kazi.

Kama wapinzani wao wa jadi Simba wanatumia rangi nyekundu ambayo kwa mila za Yanga hawawezi kuiweka hiyo haina shida, lakini je timu nyingine za Azam FC, Ruvu Shooting, Mbeya City? Kwanini mnaharibu logo za timu zao?

Huu ni ushamba uliopitiliza ambao hausaidii chochote katika maendeleo ya soka la Tanzania, haiwezekani timu takriban 20 kwenye VPL hawafanyi huu ujinga halafu Yanga pekee ijione iko sawa katika hili, kwingineko hii ni kesi kubwa sana ambayo inaweza kuigharimu klabu, lakini hapa wahusika wanachukulia kawaida tu.

Nawasilisha

IMG_20200213_145853_554.jpeg
IMG_20200213_120512_566.jpeg
IMG_20200213_120609_781.jpeg
IMG_20200213_120651_857.jpeg
 
Viongozi wa yanga ni wapumbavu, utafikir watu ambao hawajenda shule, heshimuni logo za watu kama wanavyo heshimu ya kwenu, huu ujinga hata watu wa mtaani wasio kuwa na elimu hawafanyi, kwani mkiweka logo ya team zingine kama inavyotakiwa mtakuwa mmepungukiwa nini, au ndio mashabiki watakuwa wamehamia hizo team, vitu vidogo kama hivi vinaweza kufanya muonekane Viongozi wote akili hamna akili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa hapo utadhani CITY nao wanatumia kijani ilhali ni Zambarau na hapo lazima kuna waliokerwa kwa logo yao kuwekwa rangi ya kijani hii kitu haikubaliki kwakweli, hivi hizi PHD zinafanya kazi wapi?

Pengine ni uzembe tu wa ''vijana wao'' wa idara ya habari na mawasiliano hasa wale wanao handle social media accounts zao.
 
Waache ujima ambao hauwezi kuwafikisha popote, Na wale akina Sibonike mbona hawaji hapa kutuambia kutoheshimu brand au trademark?
Hakuna klabu ya ajabu duniani kama yanga. Kulialia ni wao. Aleji ya rangingi nyekundu ni wao kila sarakasi ni wao du!!! hii yapaswa iwekwe kwenye maajabu ya dunia.

Hakuna maendeleo miaka yote watakayo yapata kama wasipobadilika fikra zao, klabu inaendeshwa kisiasa sana badala ya utaalam. Yanga putuuuuu ni shida sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Viongozi wa yanga ni wapumbavu, utafikir watu ambao hawajenda shule, heshimuni logo za watu kama wanavyo heshimu ya kwenu, huu ujinga hata watu wa mtaani wasio kuwa na elimu hawafanyi, kwani mkiweka logo ya team zingine kama inavyotakiwa mtakuwa mmepungukiwa nini, au ndio mashabiki watakuwa wamehamia hizo team, vitu vidogo kama hivi vinaweza kufanya muonekane Viongozi wote akili hamna akili

Sent using Jamii Forums mobile app
Muulizeni Uchebe sehemu au club yenye viongozi waongo wasioenda shule.

Club ambayo viongozi wake na mashabiki ni maboya fuata upepo.

Mkifungwa mechi moja tu, kocha hafai. Kesho mkishinda, mnajidai hata aje Barca hatoki.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom